Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Hizi unasema ni tuhuma (sikatai kuwa jamaa ni mchafu na corrupt sana). Lakini kisheria/kikatiba hawezi kuwa yeye ndiye mwajibikaji/mwajibishwaji kwa tuhuma walizotoa.Wangeanza/wangejumuisha na viongozi wa vyombo vya usalama kama ndiyo hivyo.
 
Huyo hapo...kasema wasipoondoa hivyo vikwazo basi serikali yetu nayo itajibu kwa kwenda kuwachukua na kuwarudisha akina Nyani Ngabu nchini.View attachment 1343585

Lol, “tutawachukua”
As if hao raia wanataka kurudi.
Nikiwa mmoja wa hao raia nasema hata kwa juju sirudi kwenye upuuzi unaofanyika Tanzania. Eti makonda akawe kiongozi wangu wakati nna akili mara mia zaidi yake. Ja!
 
HUYU KABUDI ASI HARIBIE WATU MAISHA YAO. MA UBISHI YAKE ASIUNGIZE WATU WENGUNE.
MAGUFURI TUMBUA HUYU KABUDI MAMBO YASIZIDI KUHARIBIKA.
 
Haki ya kuishi maana yake ni kuua, kujeruhi, kuonea na kutesa.
 
Hukuona jinsi alivyovamia clouds na mtutu wa bunduki?Issue ni abuse of power,hatujui mengine ni yapi ambayo USA wana ushahidi nayo!Huenda wamenasa hata walioorganize shambulio la Lissu au watu wengine!
Jamani jaribuni kunielewa. Mimi hata siku moja sikatai kuwa jamaa anatumia madaraka vibaya, ni msanii na hakuna kazi yoyote anayofanya zaidi ya kujionyesha, na pia amelewa madaraka. Issue yangu ni kuwa pamoja na haya madhambi yoooote asingekuwa ameropoka suala la ushoga wala wasingemgusa.
 
Lol, “tutawachukua”
As if hao raia wanataka kurudi.
Nikiwa mmoja wa hao raia nasema hata kwa juju sirudi kwenye upuuzi unaofanyika Tanzania. Eti makonda akawe kiongozi wangu wakati nna akili mara mia zaidi yake. Ja!
KABUDI HANA AKILI KABISA . HUYU JAMAA NI BOMU
 
Bashite akishikwa na hali ngumu huibukia kanisani mara moja..

Najiuliza kesho ataibukia madhabahu ipi kati ya hawa wachungaji wapambe nuksi Kakobe na Mwingira ili kuombewa pepo wabaya wanayemwandama?

Kesho pia naamini Rais Magufuli ataibuka popote kwa ajili ya kufanyiwa maombi.

Tutawafuatilia mguu kwa Mguu na tutawapa habari

Stay tuned in!
 
Kumweka Magufuli kundi moja na kina Lumumba, Nkrumah, Nyerere, Thomas Sankara ni uzwazwa wa kiwango cha lami! Magufuli anaweza fananishwa na kina Mobutu, Bokassa, Kagame, Nkurunziza na labda Museveni.
Magufuli hajafanya hata sehemu moja ya mia ya aliyoyafanya Nyerere. Na bado Nyerere hakuwekewa!
Nyerere alitaifisha migodi yote na kuifunga akidai kufanya hivyo 'hadi watakapopatikana Watanzania wenye ujuzi wa kuchimba kwa faida yangu vizazi vijavyo', alitaifisha mashamba makubwa, majumba yaliyojengwa kwa mapato ya 'kinyonyaji' aliifanya Tanzania kuwa ngome ya wapigania Uhuru na mengine kibao lakini hakuwekewa vikwazo wala kunyimwa misaada ikiwemo mikopo alipoihitaji!
Leo JPM kukamata kontena kadhaa za mchanga awe adui wa kuwindwa na 'Mabeberu'? Ni Ulaghai wa mchana kweupe.
Sababu za vikwazo imewekwa wazi kwa yeyote anayejua lugha, ni 'Human Rights abuse', yaani uvunjifu wa haki za Binadamu na kuwanyima watu haki ya uhai, ndiyo 'The right to life'! Kwa tafsiri rahisi ni 'Muuaji'! Na Marekani wanadai kuwa na ushahidi usiotiliwa shaka!
Bado unataka kutulaghai eti ni kwa sababu za uzalendo? Uzalendo upi? Wa kuteka, kutesa na kuwapoteza watu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
BBC ambalo ni shirika la utangazaji la Uingereza limeweka wazi kuwa mkuu wa mkoa wa Dares salaam amezuiwa kuingia Marekani kwa sababu ya juhudi zake za kupambana na ushoga nchini Tanzania.

Ikumbukwe Mara baada ya Paul kuanzisha vita ya madawa ya kulevya na ushoga alianza kushambuliwa na kupokea vitisho kutoka kwa chadema na mabeberu kutoka kote duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aacheni ujnga
Makonda mwenyewe hajulikani ni jinsia gani. Hebu someni tuhuma zake. Wala la ushoga halimo. By yhe way Makonda ana. Nguvu gani kwenye issue ya ushoga??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM mnajua kutufunga magoli, ndiyo maana mnatupa bora elimu bure ili tuzidi kudumaa. Pompeo ameandika wazi kuwa Paul Makonda anazuia haki ya binadamu kuishi.

Huo ushoga mbona Museveni na Uhuru Kenyatta wanaupinga lakinihawajapigwa pini ya kwenda duniani. Tunashukuru shule zadini kutufundisha this is an apple tumeweza kumuelewa Pompeo.
 
Hayo maelezo waambie BBC

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani ni habari nyingine! Waliwahi kumkamata Rais wa nchi nyingine na kumsweka mahabusu kwao Marekani. Wameanza na Makonda. Hatua tutakayochukua ndio aidha itafanya adhabu iwe yake pekee au ipanue wigo kwa viongozi wengine.

Heri nusu ya shari kuliko shari kamili. Marekani haifanyi maamuzi ya kubahatisha ina ushahidi na imesema! Makonda ajiuzulu. Apangiwe ubalozi na aapishwe kimya kimya! Vinginevyo itakuwa balaa kubwa. Chachu ndogo itachachusha donge zima
 
Taarifa Rasmi ilitolewa na pompeo na USA, hiyo ya waandishi wa habari ipeleke Facebook
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…