Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Wanabodi, Taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani inaonyesha Paul makonda amedhulumu watu haki ya kuishi hapa Tanzania

Je, anahusika na mauaji, utekaji wa watu na kushambulia Raia?

Je, hayo majina kwanini kama Taifa tusiletewe ili kujua idadi kamili

Idadi ya waliopotea au kufanyiwa mauaji inyojulikana ni ya wanasiasa tu na waandishi wa habari

Je, watu ambao ana chuki nao au wanapishana kimtazamo kazini nao anawanyima haki ya kuishi kimya kimya

Makonda kama mtu smart yampasa kuanza kutafuta nchi au makazi ya kwenda kuishi nje ya nchi, Hapa Tanzania kwake alishachafuka ni suala la muda tu

Je, ni nani Makonda anashirikiana nao kuwatoa watu uhai?
 
Mheshimiwa Rais,

Natambua kwamba wewe unayo mamlaka ya kutambua na kutumbua. Natambua pia kwamba wewe unatambua uwezo wa taifa la Marekani katika kupata intelijensia ya yanayojiri katika taifa lako ikiwamo tuhuma dhidi ya Makonda.

Wewe kama Mkuu wa nchi unayo nafasi ya kuhakikisha kwamba unaionyesha dunia kwamba wewe huungi mkono matendo ambayo ndugu Makonda anatuhumiwa na kuhusishwa nayo. Natambua pia kwamba unao uwezo wa kumpa hata kaubalozi huko nchi za mbali ambako ataweza kuwa salama na mbali na siasa za hapa nchini.

Iwapo yote aliyofanya ni kweli au si kweli ama ulimtuma au hukumtuma nakusihi sana uchukue hatua ya kuonesha kwamba wewe humlindi ili matukio haya anayotuhumiwa haya yasiendelee kuonekana kwamba ni matendo yaliyotendwa na Serikali bali yawe ni kwa utashi wake binafsi.

Wakati wa kutengua uteuzi wake ni sasa.Ni kama unaona kwamba hujapata mtu sahihi wa kuendesha jiji la Dar es salaam wapo wengi tu.Unaweza hata kumteua Polepole maana naye ameanza kupoteza mvuto kwenye nafasi yake ya uenezi, au unaweza kumleta yule Mrembo aliyeko Kisarawe.

Natumaini kwamba utachukua hatua stahiki.

Vile vile nimeona nafasi ya Mkurugenzi wa habari maelezo iko wazi.Nafikiri ni wakti sasa wa kumfikiria Mayala na kumpa nafasi hio atuoneshe uwezo wako

Nakutakia 2020 njema.
 
Kwani Roma kesharudi bongo🤔
....ok nimekumbuka tuliambiwa Hana elimu ya kutosha kuongea na wasomi....tuendelee na mjadala.
 
Ogopa sana watu wenye technology yao, maovu yanayotendeka yote wanayajua, hapa Makonda mwenyewe analijua hilo damu zisizo na hatia zitamuandama sana
 
Ukisoma vizuri ile barua Makonda ni chambo tu, Anaua kwa mkono wake au anatuma watu?

Hiyo haki ya kuishi anaamua muda atakao kukupoteza au?
Kwani Roma kesharudi bongo[emoji848]
....ok nimekumbuka tuliambiwa Hana elimu ya kutosha kuongea na wasomi....tuendelee na mjadala.
 
Mkuu huyu si anashinda madhabahuni akila na wachungaji, Wachungaji hawakuona hili kupitia upako wao
Ogopa sana watu wenye technology yao, maovu yanayotendeka yote wanayajua,hapa Makonda mwenyewe analijua hilo damu zisizo na hatia zitamuandama sana
 
Pia jiwe alimtuma asimamie shambulizi la lissu na lengo lilikuwa kumdhulumu haki ya kuishi, lkn mungu akasema hapana.
 
Roma alikoswa koswa kudhulumiwa haki ya kuishi na sehemu alipofichwa bashite alikuwa anafahamu, so huyu jamaa ni engineer wakudhulumu haki za maisha.
 
Mkuu huyu si anashinda madhabahuni akila na wachungaji, Wachungaji hawakuona hili kupitia upako wao
Hatuna wachungaji nchi hii,ni wa kuhesabu sana wengine wote ni wachumia tumbo tu,aibu wanayoipata sasa baada ya kumtetea na kumsafisha wanajua wenyewe
 
Marekani wametupatia jawabu...Bashite anahusika na matukio ya utekaji & mauaji.
Ni kiongozi wa wale "wasiojulika"

Na kwa vyovyote vile kwa ushahidi wa maneno hata vitendo... anatumwa na mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kuzuia madawa ya kulevya kwa nguvu zote ndio unakotafsiri kuwanyima watu haki ya kuishi? Yaani kwa busara zako unaona USA watakukatalia visa kwenda kwao kwa kuwa unaongooza vita dhidi ya madawa ya kulevya? Au kukataza ushoga ni kumnyima mtu haki ya kuishi?

Hivi watu mna uziwi wa kiasi gani?
Mwambie hivi kama Marekani wanachukizwa na vita ya madawa ya kulevya ajaribu yeye kwenda nayo ili aone vita ya madawa kule ikoje.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kumnyima Visa ya kuingia Marekani ndo watazuia juhudi zake na serikali kupiga vita madawa ya kulevya na genge la madawa ya kulevya paomoja na ushoga? Ataendelea tena kwa saana kwasababu amewashika pabaya! Moja ya mikakati ya USA ni kuungana na magenge ya uhalifu wa kimataifa kuzinyongonyeza nchi masikini ili wapore mali na utajiri wa nchi za kiafrica. Moja ya mbinu inayozitumia marekani ni pamoja na kusupport magenge ya madawa ya kulevya kuingizwa katika nchi masikini kuharibu vizazi ili kutengeneza mwanya wa kuzipora rasilimali zao!
Jaribu kutumia akili Mkuu, usitumie makalio. Huyo ameua akina Saa nane, Azory gwanda na wengineo wengi tu. Unataka tuseme mara ngapi hapa?
 
Back
Top Bottom