Pendekezo: Dkt. Hassan Abassi afukuzwe kazi kwa kiburi cha kukataa amri halali ya Rais wa Nchi

Pendekezo: Dkt. Hassan Abassi afukuzwe kazi kwa kiburi cha kukataa amri halali ya Rais wa Nchi

Hakuna ambaye hajamsikia Rais Samia Suluhu leo alipoagiza vyombo vya habari vilivyofungiwa kwa chuki vifunguliwe , huyu Hassan Abbass ni nani katika nchi hii hadi amlishe maneno Mh Rais kwamba Kilichoagizwa kufunguliwa ni Televisheni za mitandaoni , liko wapi andiko alilopewa na Mh Rais kuhusu hilo ?

Je amedhamiria kumpinga Mh Rais kwa faida ya nani ? kuna haja gani ya kuendelea kuwa na kiongozi mwenye kiburi kiasi hiki ?

Bila shaka huyu ameshindwa kwenda na kasi ya mama , ameamua kupandisha mabega yake juu kujimwabafai , napendekeza afukuzwe kazi haraka na ikiwezekana akamatwe na kushitakiwa .

View attachment 1745371
Tetesi zinasema PhD yake ni ya kuunga unga.
Alaf kupindisha maagizo ya Mkuu wako kazi ni dalili ya dharau.
Simuombei mabaya ila akiendelea hivi hafiki mbali ataliwa kichwa hakuna mamlaka inapenda kudharauliwa na aliyeko chini.
Dr. Abbas kuwa na nidhamu kwa Rais vinginevyo utaingia kwenye mfungo ukiwa na majonzi
 
Nikifanya Ziara Ujue Bango Moja Ujue DC/DED Anaondoka Sijasema Mkawazuie Wananchi Kuandika Mabango. 😂😁
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Honorable Madame Samia Suluhu Hassan
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Huyu Hassan Abbas Hilo Ni Bango Kajibebea Mwenyewe Subirini Aondoke. 😣😏😂😁😀😆😅😄😄
 
Sasa huyu Dr Abbas hiyo ya online tv pekee kaitolea wapi Rais aliitoa hiyo statement mwanzo tu baadaye akageneralize kuwa vyombo vyote vya habari au kipindi anasema hivi Dr alikuwa washroom? Mbona anataka kumshika ushungi Rais mapema hivi

Dr taratibu bana usitake kumfuata yule wa TPA uwe kigogo wa pili kufurushwa Rais amesema vyombo vya habari kila mtu amesikia kama kuna vyombo ulikuwa una bifu navyo hayo ni yako tekeleza agizo tu hata kama hupendi kinyume na hapo uende tu ukafundishe chuo
IMG-20210406-WA0003.jpg
 
Kwani vyombo vya Habari ni Tv pekee? mbona huyu bwana mdogo anataka kujibishana na Mh Rais? Ni nini kinampa kiburi haswa?


Anyway time will tell, naona kabisa taratibu masalia ya Jiwe yakiondolewa taratibu kwenye mfumo?
 
Hivi ni kiburi cha kukataa au akili ndogo hajamuelewa Rais?

Kuna nafasi moja lazima ataiachia, zaidi hiyo ya msemaji wa serikali, labda majukumu mawili yamemlemea ndio sababu akili haichaji vizuri.
Jamaaa ana akili ndogokaangalie imatokeo yake yakidato ha sita ndo mtamjua
 
Hili dude silpendi Hivi hii Corona imekula rushwa? Nashauri iondoke na hili dude.

Jifunze kubariki ili nawe ubarikiwe. Usiwe mtu wa kuombea watu mabaya.

Naamini kabla mwaka huu haujaisha, COVID- 19 atakua ndani ya familia yako kabla ya kukutembelea wewe mwenyewe mapema mwaka ujao.
 
Dr Abbas anaipunguza speech ya rais katika tafsiri anayoitaka yeye. Rais kasema vyombo vya habari yeye anasema online TV tu.
Huu ni ukaidi
Mama asimcheleweshe huyu kifutu,emepandisha mabega ayafyekelewe mbali. Amezingua azinguliwe tu hakuna jinsi nyingine. Mama ajue kuwa huyu bumunda anamjaribu akimuacha na wengine watafanya hivyo hivyo.
 
Ngoja tuone.

PhD inaposhindwa kutafsiri maana ya vyombo vya habari.

PhD inasema gazeti siyo chombo cha habari.

PhD inambishia Rais ambaye ni taasisi.

PhD inachanganya itikadi na maswala ya kiserikali.

Ngoja tuone.

Ukinizingua Nakuzingua!
Ww jamaa kitu ulifanya ktk uongozi wa mwendazake ulikuwa upo neutral katika hoja zako,nahisi ww humu jf ndio mataga uliekuwa unajitambua,hongera kwa hilo[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Dr bila shaka kaondoka na tafsiri ya ile statement ya pili ambapo ilikuwa kama mfano wakati mama akitamka neno viji-tv vya mkononi.
 
Back
Top Bottom