Pesa inayofaa kuacha kwa matumizi ya familia yenye watoto wawili wasiozidi miaka 5

Pesa inayofaa kuacha kwa matumizi ya familia yenye watoto wawili wasiozidi miaka 5

Mkuu majibu yako yaonyesha wewe ni mbangaizaji mwenzetu, kwa hiyo mpe 300,000 hadi 500,000 ila uridhike na chochote atakachopika manake bajeti yako ni ndogo na familia ni kubwa ili iwatoshe kumaliza mwezi
Kweli mkuu tunabangaiza hivyo ili maisha yasonge nashukur kwa mawazo yako mkuu
 
Hivi,kuna kitu wanaume wengi hawajui. Mwanamke akiamua kukukomoa,utakufa kabla ya siku zako. Je,hakuna wengine wasiopata hata laki 3 na wanaishi? Kama una uhakika biashara aliua mwenyewe, basi jiandae. Ila mi ningekupa tu ushauri. Mtafutie kitu kinachouzika nyumbani hapo hapo,akapate hela ya mboga. Mahitaji mengine ya kukaa mda mrefu,nunua mwenyewe. Si yeye amefeli? Af kwa atakachokuwa anapata,utajua kipi kinaendelea. Wapo wengine hawana uchungu na jasho unalotumia kupata hiyo pesa. Na ukiuliza imefanya kazi gani,hawana majibu. Hapo ikishindikana we lea watoto wako. Japo pia kwa upande mwingine kuna sehemu mnakosea. Unazaa na mtu,watoto wawili,unamuacha unaenda kuoa kwingine. Unategemea nini? Kama si mkeo,lazima nae awe na akili ya kutafuta kianzio cha maisha. Hapo anakusanya mtaji,ili ukizingua ajue anaanzia wapi. Kwa upande mwingine namuelewa. Mi kama naona siwezi kuishi na wewe,hata kugegedana lazima niwe makini. Maswala ya mimba usikopenda,ujue utateseka mpaka unakata upepo. Labda kama watoto huwakubali.
 
Then usiulize, tafuta mwenye matumizi mazuri, Man up Dogo, wanawake ni washenzy sana we never negotiate; we just lead them the way we see it fit!
Mkuu sometimes busara inabidi itumike huwezi kumwacha mwanamke eti kisa ana matumizi mabaya,utaacha wangapi.kila mtu ana mapungufu yake
 
Hivi,kuna kitu wanaume wengi hawajui. Mwanamke akiamua kukukomoa,utakufa kabla ya siku zako. Je,hakuna wengine wasiopata hata laki 3 na wanaishi? Kama una uhakika biashara aliua mwenyewe, basi jiandae. Ila mi ningekupa tu ushauri. Mtafutie kitu kinachouzika nyumbani hapo hapo,akapate hela ya mboga. Mahitaji mengine ya kukaa mda mrefu,nunua mwenyewe. Si yeye amefeli? Af kwa atakachokuwa anapata,utajua kipi kinaendelea. Wapo wengine hawana uchungu na jasho unalotumia kupata hiyo pesa. Na ukiuliza imefanya kazi gani,hawana majibu. Hapo ikishindikana we lea watoto wako. Japo pia kwa upande mwingine kuna sehemu mnakosea. Unazaa na mtu,watoto wawili,unamuacha unaenda kuoa kwingine. Unategemea nini? Kama si mkeo,lazima nae awe na akili ya kutafuta kianzio cha maisha. Hapo anakusanya mtaji,ili ukizingua ajue anaanzia wapi. Kwa upande mwingine namuelewa. Mi kama naona siwezi kuishi na wewe,hata kugegedana lazima niwe makini. Maswala ya mimba usikopenda,ujue utateseka mpaka unakata upepo. Labda kama watoto huwakubali.
Nashukur mkuu kwa ushauri wako nimeupokea
 
Twenzetu ,kitu kimoja hujaweka wazi. Umezaa nae na kila mmoja anaishi kivyake, au badae mlirudiana! Maana mada inaanza kwamba ulikuwa na mwanamke ulozaa nae.
MKuu sijamuacha,ila kazi ndo imenitenganisha na familia,mimi nafanya kazi Dom,familia inaishi Dar
 
Mkuu hapo umekosea mawazo yako ni muhimu katika kusaidia kuchukua maamuzi
Unataka tukupangie badget wakati hujatupa muongozo;

Hatujui huwa mnapendelea kula nini?

Kama mboga saba je?

Kama mnaenda supermarket au sokoni?

Kama kila week mnafanya shoppings za mavazi?

Hatujui matumizi yenu ya umeme, maji?

Matumizi ya data, Huenda mkeo anashinda TIKTOK?

Kiufupi kaa na mkeo chini muangalie matumizi ya msingi zaidi myatengee bajeti, Yale yasiyo ya msingi mjitahidi kuyapunguza au muachane nayo.

Kila mtu ana level yake ya Matumizi wakishua atakwambia Milioni kadhaa, Wa hali ya chini atakwambia Laki kadhaa, Hilo liko ndani ya uwezo wako mwenyewe.
 
unampaje mzazi mwezako Hela za watoto ,fanya hivi mwezi ujao usitoe hela nunua vyakula mkabidhi nafaka
Mkuu kwani vibaya kumwachia wife pesa ya chakula na mengine madogo madogo,shida ni aina ya matumizi anayoyafanya
 
Nilikuwa na mwanamke nilizaa nae watoto wawili

Nilijaribu kumfungulia biashara akaiua

Nilikuwa nauliza kwa wenzangu wenye uzoefu ikiwa kama mwanaume nalipa vitu vifuatavyo:

Kodi, bima za afya za watoto na mama yao, maji, umeme, ving'amuzi, ada ya mtoto aliyeanza kusoma, mavazi na mengineyo

Je ni kiasi gani kinafaa kumwachia mwanamke ya kuweza kuwalisha ile standard kabisa kwa maisha yetu haya ya kitanzania kwa mwezi
Hili nalo ni la ku google kweli?
 
Sasa shida ni nn km umekuachia na anapanga vizuri?
Shida pesa ninayomkabidhi anamaliza kabla ya mwezi kuisha so inabidi nitume nyingine ndo maana nimeuliza kwa ndugu zangu wa JF,kama ninaweza kupata mwongozo kidogo
 
Akifanya hivi miezi mitatu tu atapata kujua wastani wa matumizi ya familia yake kwa mwezi
vyepesi tu ,ajiulize yafuatayo

Nyama robo watoto wake wanakula Milo mingapi(kwa wiki wanatakiwa kula marangapi
MBOGA majani kwa wiki wale marangapi

mchele kwa wiki wanakula kiasi Gani
ugali ,ataxame unga
Danga lake asilipigie hesabu , na tatizo lenu mnayaita madanga mitandaoni ,ndani ya Kuta eti wife
 
Unataka tukupangie badget wakati hujatupa muongozo;

Hatujui huwa mnapendelea kula nini?

Kama mboga saba je?

Kama mnaenda supermarket au sokoni?

Kama kila week mnafanya shoppings za mavazi?

Hatujui matumizi yenu ya umeme, maji?

Matumizi ya data, Huenda mkeo anashinda TIKTOK?

Kiufupi kaa na mkeo chini muangalie matumizi ya msingi zaidi myatengee bajeti, Yale yasiyo ya msingi mjitahidi kuyapunguza au muachane nayo.

Kila mtu ana level yake ya Matumizi wakishua atakwambia Milioni kadhaa, Wa hali ya chini atakwambia Laki kadhaa, Hilo liko ndani ya uwezo wako mwenyewe.
Mkuu nimeshasema awali bills nyingine zote naclear kama umeme,mqji mk
 
Mada kama hizi nazipenda kwani kwa uchangiaji tu, unaweza kujua WIFE MATERIAL tulio nao huku jukwaani.
Mungu awabariki!
 
Kama huhusiki na kutaka kujua jinsi ya matumizi ya hiyo hela basi sina cha kukusaidia,na inawezekana usipate msaada wowote humu,

Kingine,maisha yanatofautiana kutokana na eneo analoishi muhusika,hapa hata hujasema hiyo familia inaishi wapi,

Hutaweza kutatua tatizo lako mpaka pale utakapotaka kujua matumizi sahihi ya hizo hela,
Huwezi kupanga bajeti bila kujua matumizi yanaenda kutumika kwenye nini na nini.
Huyu atakuwa last born,hataki kujua majukumu yake ngoja jf wafanyie na kumpangia majukumu....

Na huyo mwanamke siku jamaa akija kuchacha....bomu litakalolipuka apo hatari

Laki 8 unaacha nyumbani...!!!? Afu unakuja kulialia kwa watu wanao Acha laki 2 adi laki 1 kwa mwezi...!!
 
Back
Top Bottom