Pesa inayofaa kuacha kwa matumizi ya familia yenye watoto wawili wasiozidi miaka 5

Pesa inayofaa kuacha kwa matumizi ya familia yenye watoto wawili wasiozidi miaka 5

Huyu atakuwa last born,hataki kujua majukumu yake ngoja jf wafanyie na kumpangia majukumu....

Na huyo mwanamke siku jamaa akija kuchacha....bomu litakalolipuka apo hatari

Laki 8 unaacha nyumbani...!!!? Afu unakuja kulialia kwa watu wanao Acha laki 2 adi laki 1 kwa mwezi...!!
Mkuu bahati nzuri mimi ni First born,huwezi amini nmepata baadhi ya madini ya kuanza nayo kwenye kufanya maamuz yngu
 
Hutaweza kutatua tatizo lako mpaka pale utakapotaka kujua matumizi sahihi ya hizo hela,
Mkuu, umetaja ENEO, pia kujua matumizi ya fedha! Ni sahihi sana!

Tsh 800,000 kwa mwezi, watoto wawili, mama pengine na beki 3, inatosha sana kwa masuala ya maakuli!

Masuala ya sijui Bima, Ada, Bill za umeme, maji na ving'amuzi zisiwe sehemu hiyo ya 800k.

Zaidi, kama huyo mkeo naye ni mtafuta kipato, yaani masaa pengine 9 ya siku anaiacha familia mikononi mwa beki 3 na walimu, basi 800k inatosha sana tu; palipobakiwa atajazia yeye.
- Bima na Ada, mtakaa mezani kuona namna nzuri ya ku-cover

Vyovyote wasemavyo, usiruhusu kipato cha mwanamke kipotelee kusikojulikana, mpe majukumu ya kifamilia, angalau nusu ya kipato chake chote kitumike kwenye familia.
 
Mkuu, umetaja ENEO, pia kujua matumizi ya fedha! Ni sahihi sana!

Tsh 800,000 kwa mwezi, watoto wawili, mama pengine na beki 3, inatosha sana kwa masuala ya maakuli!

Masuala ya sijui Bima, Ada, Bill za umeme, maji na ving'amuzi zisiwe sehemu hiyo ya 800k.

Zaidi, kama huyo mkeo naye ni mtafuta kipato, yaani masaa pengine 9 ya siku anaiacha familia mikononi mwa beki 3 na walimu, basi 800k inatosha sana tu; palipobakiwa atajazia yeye.
- Bima na Ada, mtakaa mezani kuona namna nzuri ya ku-cover

Vyovyote wasemavyo, usiruhusu kipato cha mwanamke kipotelee kusikojulikana, mpe majukumu ya kifamilia, angalau nusu ya kipato chake chote kitumike kwenye familia.

Huyo muhusika ameshasema ni muajiriwa; hivi mnafaham mishahara ya Wafanyakazi waliowengi au mnaongelea wale wachache. Takriban 70% ya wafanyakazi wana take home ya approximately 900,000shs kurudi chini.
Sasa sijui kama yupo kwenye 30% ya wenye mishahara yenye nafuu au yupo kwenye 70%
 
Nilikuwa na mwanamke nilizaa nae watoto wawili

Nilijaribu kumfungulia biashara akaiua

Nilikuwa nauliza kwa wenzangu wenye uzoefu ikiwa kama mwanaume nalipa vitu vifuatavyo:

Kodi, bima za afya za watoto na mama yao, maji, umeme, ving'amuzi, ada ya mtoto aliyeanza kusoma, mavazi na mengineyo

Je ni kiasi gani kinafaa kumwachia mwanamke ya kuweza kuwalisha ile standard kabisa kwa maisha yetu haya ya kitanzania kwa mwezi
laki 4 na elfu 50 kwa wastani kila siku atakuwa anatumia shilingi elfu 15 zitamtosha kabisa.
 
Nimekuwa nikifanya hivyo kumpa bila kumkadiria but ninayompatia unakuta haifiki hata mwezi anasema imeisha na kwavile mimi nafanyia shughuli zangu nje ya Dar,kurudi kwangu huwa ni weekend tu
Nunua nahitaji yote muhimu Kama unga, mchele, sukari, mafuta, gesi na mengineyo, lipa bili za maji, umeme na Kodi ya nyumba. Machine pesa zikiwemo za dharula Kama itatokea ugonjwa akimatumia vibaya juu yake
 
Huyo muhusika ameshasema ni muajiriwa;
Pia kuna sehemu kasema anaacha 800k

Takriban 70% ya wafanyakazi wana take home ya approximate 900,000shs kurudi chini.
Hii nilikuwa sijui, sasa mbona maisha yao ni mazuri sana kulinganisha na 900k kwa mwezi!
  • Ndo wamiliki wa hizi SUV mjini hapa
  • Shopping ni kwenye malls tu
  • Huku mitandaoni, wajuaji wa maisha bora ndo wao.

Net pay ya 900k ni kubwa ila sio kwa life wanaloishi hawa watwana huku mtaani!

Au umemaanisha 9,000,000 kwa mwezi?

Kwanza nasikia siku hizi, mtumishi wa umma anayeanza kazi na degree moja, mshahara unaanzia tsh 3,100,000.
- Hiyo 70% ya kupata 900k inakuaje?
 
Nashukuru mkuu kwa ushauri wako,mimi ni mwajiriwa so kipato cha mwezi ni constant
basi mshahara wako gawa by %ge,

-15% iwe ya mahitaji yao ya bills hizo sjui umeme, maji, decoder nk.
-20%ndio ya food nk

so kwenye mshahara wako toa 35% ya mshahara ndio utumie kwa mahitaji muhimu ya watoto wako nyumbani, then 65% fanyia matumizi yako, usisahau saving tu za emergency.
 
Hapo hauna mwanamke shekhe cha kufanya ww kila siki asubui mtumie 10,000 kwenye cm ,

Kila asubui mtumie hivyo atoe 9,000 atumie
 
Shida pesa ninayomkabidhi anamaliza kabla ya mwezi kuisha so inabidi nitume nyingine ndo maana nimeuliza kwa ndugu zangu wa JF,kama ninaweza kupata mwongozo kidogo
kwa sababu anahisi unayo zaidi, hivo anakukomoa,.pia si unatujua sisi wanawake, ye umemuacha dar we upo dom, lazima aoneshe matashtiti kwa mashoga zake na majirani kua nina bwana wa maana yuko dom, ananipa kila nachotaka, ana mihela, nakula vizuri nk

mjini matashtiti muhimu ili watu wasitudharau kua,hatuna mabwana wa maana.

kijana wangu, za kuambiwa changanya na zako, mshaambiwa muishi na wanawake kwa akili.
 
Kwa maelezo Yako ni WA,I kabisa mkeo hawezi kujisimamia kwenye suala la pesa,,, sasa fanya hivi,, nunua Michele wa kutosha wa mwezi, unga, nyama, samaki, nyanya, viazi....then kama uko vizuri kiuchumi mwachie 100k au 150k ya emergency....
 
Mkuu mambo hayo mengine kuhusu mambo ya jikon sihusiki nayo,ndo mana niwe mkwel kwa mwezi namwingiziaga laki 8 bank,nikijua kwa maisha yetu ya kitanzania itamtosha but mwezi unakuta hauishi anadai hela imeisha,ndo maana nimeuliza wadau ili niambulie mawili matatu ili nipate pa kuanzia
Wewe ndo mwenye tatizo siyo yeye,baba ni kiongozi.Hapo umeshindwa kuonesha kuwa wewe ni kiongozi.Familia yangu ina watu 16-20 lkn natumia 170000 kwa wiki.
Hapo vitu muhimu kama mafuta ya kula, mchele,sabuni na gesi nakuwa nimevinunua.
Muongoze mke wako matumizi,badilisha utaratibu anza kumpa kwa kila wiki 150000.
 
Jenga tabia ya kumuwekea balance kwenye bank account yake au mpesa etc.then hakikisha ndani ya huo mwezi umefanya shopping kubwa ya mahitajiya ndani.

Halafu ukimuachia hata 20 au 15.itamtosha akifeli ata draw kwenye ile akiba unayo muwekea.

Kama shida ni kubwa utapata simu toka kwake.pia jenga tabia ya kutuma au kurudi na kitoweo.hiii hupunguza jam sku inayo fuata.
 
Mkuu bahati nzuri mimi ni First born,huwezi amini nmepata baadhi ya madini ya kuanza nayo kwenye kufanya maamuz yngu
Sasa mkuu budget ya familia inakushindaje kupanga....!!.au mna share income mkeo,au mkeo ndo mwenye sauti ndani....bado nawaza sipati jibu
 
Nimekaa nikatafakari, naona kuna shida mahari furani,mleta mada hajaweka wazi. Nachohisi mahusiano si mazuri. Pia naona kama alivyosema mdau,kuna siku bomu litalipuka. Nadhani ukituweka wazi, mambo yatakuwa mengine,na ushauli utakuwa mwingine kabisa.
 
Mkuu mambo hayo mengine kuhusu mambo ya jikon sihusiki nayo,ndo mana niwe mkwel kwa mwezi namwingiziaga laki 8 bank,nikijua kwa maisha yetu ya kitanzania itamtosha but mwezi unakuta hauishi anadai hela imeisha,ndo maana nimeuliza wadau ili niambulie mawili matatu ili nipate pa kuanzia
Laki 8 kuna kajamaa lazima kana hongwa shituka mapema.
 
Mkuu, umetaja ENEO, pia kujua matumizi ya fedha! Ni sahihi sana!

Tsh 800,000 kwa mwezi, watoto wawili, mama pengine na beki 3, inatosha sana kwa masuala ya maakuli!

Masuala ya sijui Bima, Ada, Bill za umeme, maji na ving'amuzi zisiwe sehemu hiyo ya 800k.

Zaidi, kama huyo mkeo naye ni mtafuta kipato, yaani masaa pengine 9 ya siku anaiacha familia mikononi mwa beki 3 na walimu, basi 800k inatosha sana tu; palipobakiwa atajazia yeye.
- Bima na Ada, mtakaa mezani kuona namna nzuri ya ku-cover

Vyovyote wasemavyo, usiruhusu kipato cha mwanamke kipotelee kusikojulikana, mpe majukumu ya kifamilia, angalau nusu ya kipato chake chote kitumike kwenye familia.
Mkuu hyo laki 8 ni kwa ajili ya chakula na vitu vidogo vidogo.hizo bili nyingine nazilipa mimi
 
Huyo muhusika ameshasema ni muajiriwa; hivi mnafaham mishahara ya Wafanyakazi waliowengi au mnaongelea wale wachache. Takriban 70% ya wafanyakazi wana take home ya approximately 900,000shs kurudi chini.
Sasa sijui kama yupo kwenye 30% ya wenye mishahara yenye nafuu au yupo kwenye 70%
Mkuu kwa ayo makisio yako au takwimu zako nitakuwa kwenye hyo 30%.hoja iliyopo mkuu ni hayo matumizi ya wife kutokutosha mpka kudai nyongeza nyingne
 
Back
Top Bottom