Peter Madeleka: Kutishia watu kuwapeleka Magereza ili wateseke ni Ushamba na ulimbukeni. Kuuza bandari za Watanganyika ni ufisadi

Peter Madeleka: Kutishia watu kuwapeleka Magereza ili wateseke ni Ushamba na ulimbukeni. Kuuza bandari za Watanganyika ni ufisadi

I don't know why but huyu jamaa huwa nahisi bado ni mtu wa system.... Nashangaa wapinzani wanaji attach naye sana, he might be the mole in the opposition. Maana aliminywa maslahi yake akiwa kwenye mfumo akakosana nao so simply akirudishiwa maslahi yake anaweza kuplay double agent.

We should be very careful na Hawa moles wa CCM.
Siamini usemacho bila proof,

Na hata kama usemacho ni Kweli,

Jambazi aliyekubali kuacha ujambazi na kuchagua kuwa police, huzuia uhalifu na mianya yake vizuri kuliko police wa kawaida.
 
Kwa mujibu wa RIPOTI ya CAG ya mwaka 2020/2021, ni kwamba, MAGEREZA yote Tanzania, YAKIJAA, yanauwezo wa KUBEBA watu 35,000 tu. Uwanja wa MKAPA-DSM, UKIJAA, unaweza KUBEBA watu 60,000. Tanzania ina watu 60 MILIONI. Kwa hiyo, KUTISHIA watu MAGEREZA, ni USHAMBA na ULIMBUKENI.

View attachment 2748697

Lema apewe heshima ya kuwa mtabiri wa taifa kisiasa​

 

Attachments

  • 5475778-7cbee36af811d0f80109e6743290bd35.mp4
    5.1 MB
Siamini usemacho bila proof,
Proof ya Nini, mbona watu walisema patrobas ni double agent mapema kabisa ila baadae ikawa dhahihiri. Ni muhimu sana chama kujiweka mbali na Hawa moles kutoka TISS hata huyo Mwabukusi wafanye naye kazi ila akiwa huko huko NCCR sio tena aingizwe CHADEMA.

Nimeona hata kina Mwamakula sijui Askofu Maxmillian yaani watu sketchy sketchy wanakaribishwa Hadi jikoni. Lazima chama ki separate mambo ya jamii na harakati za chama. Ni ajabu sana Lissu anaenda ngorongoro alafu anasindikizwa na watu ambao sio wanachama!!

This should stop otherwise tutakuja malizwa kizembe.
 
Wakili huyu kwanini anaandamwa sana na serikali hii? Ana siri gani anazozijua wakihofu kuendelea kuzilipua hadharani hadi wakeshe wakifikiria namna ya kumrejesha gerezani? Kwanini wananchi wasiamini serikali hii imejaa uonevu kwa kutumia kichaka cha demokrasia ambayo ni garasha tupu?

Serikali acheni kumtesa wakili huyu kutokana na madhaifu yenu na watu wenu
Alikuwa jeshi la uhamiaji ,kabla yakuamua aachane na kazi malipo kiduchu

Kama
Ndg yake mwabukusi aliyeacha KAZI serikali ndani ya masaa 24 kwahiyali yake
 
Proof ya Nini, mbona watu walisema patrobas ni double agent mapema kabisa ila baadae ikawa dhahihiri. Ni muhimu sana chama kujiweka mbali na Hawa moles kutoka TISS hata huyo Mwabukusi wafanye naye kazi ila akiwa huko huko NCCR sio tena aingizwe CHADEMA.

Nimeona hata kina Mwamakula sijui Askofu Maxmillian yaani watu sketchy sketchy wanakaribishwa Hadi jikoni. Lazima chama ki separate mambo ya jamii na harakati za chama. Ni ajabu sana Lissu anaenda ngorongoro alafu anasindikizwa na watu ambao sio wanachama!!

This should stop otherwise tutakuja malizwa kizembe.
Askofu Maxmillian... Loh, nimemzooooom!!

Umesema Kweli, Umakini uongezeke, bt mengine ni ya kumwachia Mungu, maana ndani ya chama pia wapo wa kutosha.
 
Aib
Kwa mujibu wa RIPOTI ya CAG ya mwaka 2020/2021, ni kwamba, MAGEREZA yote Tanzania, YAKIJAA, yanauwezo wa KUBEBA watu 35,000 tu. Uwanja wa MKAPA-DSM, UKIJAA, unaweza KUBEBA watu 60,000. Tanzania ina watu 60 MILIONI. Kwa hiyo, KUTISHIA watu MAGEREZA, ni USHAMBA na ULIMBUKENI.

View attachment 2748697
Aibu kabisa kubambikia wananchi kesi ili kuficha ufisadi unanavanywa na walioaminiwa maofisini.
 
Kwa mujibu wa RIPOTI ya CAG ya mwaka 2020/2021, ni kwamba, MAGEREZA yote Tanzania, YAKIJAA, yanauwezo wa KUBEBA watu 35,000 tu. Uwanja wa MKAPA-DSM, UKIJAA, unaweza KUBEBA watu 60,000. Tanzania ina watu 60 MILIONI. Kwa hiyo, KUTISHIA watu MAGEREZA, ni USHAMBA na ULIMBUKENI.

View attachment 2748697
Madeleka ni fisadi fulani tu ambaye alikuwa Polisi na mke wake alikuwa ofisa Ujamiaji Arusha.

Madeleka alipoacha Upolisi akawa wakili. Na wateja wake wakubwa walikuwa wahamiaji haramu ambao mkewe alikuwa anawakamata halafu anaacha "mwanya" wa kutokea kwenye ushahidi.

Hivyo Madeleka akiwa wakili wao, na mkewe akiwa prosecutor wa Immigration, walikuwa wanapiga hela ndefu kutoka kwa wahamiaji haramu.

CG Makakala akalitambua hilo ndipo akamuachisha kazi mkewe kutokana na hujuma hizo. Kilichofuata ni mashtaka yaliyomtupa ndani hadi akakubali plea bargain.

Chuki yake kwa system na kwa Makakala ilianzia hapo. Siyo msafi hata kidogo
 
Proof ya Nini, mbona watu walisema patrobas ni double agent mapema kabisa ila baadae ikawa dhahihiri. Ni muhimu sana chama kujiweka mbali na Hawa moles kutoka TISS hata huyo Mwabukusi wafanye naye kazi ila akiwa huko huko NCCR sio tena aingizwe CHADEMA.

Nimeona hata kina Mwamakula sijui Askofu Maxmillian yaani watu sketchy sketchy wanakaribishwa Hadi jikoni. Lazima chama ki separate mambo ya jamii na harakati za chama. Ni ajabu sana Lissu anaenda ngorongoro alafu anasindikizwa na watu ambao sio wanachama!!

This should stop otherwise tutakuja malizwa kizembe.
Sijui kwanini unaishi maisha ya hofu sana, unachoandika hapa ni kama vile huiamini intelijensia ya Chadema, kitu ambacho binafsi sioni maana yake.

Haya mambo ya siasa siku zote hayapo static, kama hamtaunganishwa kwa sera zenu, lazima kuna mambo yatakayojitokeza yatakayowaunganisha, na pale mnapokuwa na common interest, kujitenga na wenzio ni ujinga tu.

Ni ujinga kwa sababu unapojitenga na wenzio ndio unapeleka ujumbe kwa jamii jinsi ulivyo selfish, na unapigilia misumari zile tuhuma za kusema Chadema hawapendi kujiunga na wengine wakati wa chaguzi, unaonesha vile usiyefaa kupewa nchi uiongoze kwasababu utawatenga wengine utakaowaona hauna maslahi nao, wakati hutakiwi kufanya hivyo.

Sioni ubaya wowote Chadema wanaoufanya mpaka sasa, kila hatua yao naiamini, na sio uaminifu wa mashaka, ni uaminifu wa uhakika kwasababu walishanionesha wako vizuri kuikwepa mitego ya CCM toka wakati ule wa usaliti wa Zitto Kabwe na wenzie, chama makini hakitakiwi kuwatenga watu, kinatakiwa kuishi nao kwa akili.
 
Wakili huyu kwanini anaandamwa sana na serikali hii? Ana siri gani anazozijua wakihofu kuendelea kuzilipua hadharani hadi wakeshe wakifikiria namna ya kumrejesha gerezani? Kwanini wananchi wasiamini serikali hii imejaa uonevu kwa kutumia kichaka cha demokrasia ambayo ni garasha tupu?

Serikali acheni kumtesa wakili huyu kutokana na madhaifu yenu na watu wenu
Nadhani wanashindwa kuzijibu hoja zake ndio upelekea huo msuguano
 
Kwa mujibu wa RIPOTI ya CAG ya mwaka 2020/2021, ni kwamba, MAGEREZA yote Tanzania, YAKIJAA, yanauwezo wa KUBEBA watu 35,000 tu. Uwanja wa MKAPA-DSM, UKIJAA, unaweza KUBEBA watu 60,000. Tanzania ina watu 60 MILIONI. Kwa hiyo, KUTISHIA watu MAGEREZA, ni USHAMBA na ULIMBUKENI.

View attachment 2748697
🤣🤣Come back ya verse moja light........
 
huyu si ndie alikimbia mahakamani baada ya kuachiwa
Vyombo vya habari siku hizi vimekuwa vya hovyo sana, vinaandika umbea wa kumfurahisha mtawala tu, ndio maana nimefuta app zote za news kwenye simu yangu, anzia Mwananchi, Ayo wote...

Bora nibaki na Al Jazeera, BBC, na Sky.
 
Hakuna anayeweza kuuza bandari ni uelewa wetu kuwa mdogo na kuwasikiliza sana wanaharakati wenye kupotosha jamii wakiwa na malengo maalum.

Bandari inakodishwa, hii ya Dar inakwenda kuwa na wapangaji wawili DPW na mwingine wa magati namba nane mpaka namba kumi na moja.

Ile ya Tanga inakwenda kuwa na mwendeshaji mmoja, ile ya Bagamoyo inakwenda kuwa na mwendeshaji mwingine.

Haya ni masuala ya kiuchumi yenye kuhitaji mtu kuyatazama kiuchumi, mtu tu layman mwenye uelewa mdogo wa masuala nyeti hawezi kuelewa nini haswa kinachotafutwa.

Tunatoka katika mfumo wa mmiliki wa bandari kuendelea kumiliki yeye kama yeye tunaingia katika mfumo wa Land lord Port ambao mwendeshaji mkuu TPA anakuwa na wapangaji wengine ili kuongeza ufanisi na kurahisisha mzigo mwingi sana uliopo ndani ya Tanzania na nchi zinazotuzunguka kuweza kuyafikia mataifa ya nje haraka.

Kuna tani zaidi ya milioni 30 za mizigo mbalimbali inayotakiwa itoke huko bara na kwenda nje ya nchi, huo ni mzigo mwingi sana na kwa aina ya uendeshaji wa kizamani wa bandari tulionao hakuna nafasi ya kitaifa kuweza kuinuka kiuchumi.

Haya ni masuala ya kiuchumi yenye kutaka ufafanuzi wa kina wa kiuchumi, huu sio wakati wa kufikiria kizamani halafu matokeo ya ufikiriaji huo yawe na mashiko kwenye maisha ya kisasa.
Huo ushindani wa wazi wa namna ya kuwapata waendeshaji hizo gati wenye tija ya kiuchumi na viwango vya ubora vya mikataba yenyewe hata kama unakodisha ndiyo matatizo yanakoanzia. Huo uchumi wa wapi unaousema?
 
Hakuna anayeweza kuuza bandari ni uelewa wetu kuwa mdogo na kuwasikiliza sana wanaharakati wenye kupotosha jamii wakiwa na malengo maalum.

Bandari inakodishwa, hii ya Dar inakwenda kuwa na wapangaji wawili DPW na mwingine wa magati namba nane mpaka namba kumi na moja.

Ile ya Tanga inakwenda kuwa na mwendeshaji mmoja, ile ya Bagamoyo inakwenda kuwa na mwendeshaji mwingine.

Haya ni masuala ya kiuchumi yenye kuhitaji mtu kuyatazama kiuchumi, mtu tu layman mwenye uelewa mdogo wa masuala nyeti hawezi kuelewa nini haswa kinachotafutwa.

Tunatoka katika mfumo wa mmiliki wa bandari kuendelea kumiliki yeye kama yeye tunaingia katika mfumo wa Land lord Port ambao mwendeshaji mkuu TPA anakuwa na wapangaji wengine ili kuongeza ufanisi na kurahisisha mzigo mwingi sana uliopo ndani ya Tanzania na nchi zinazotuzunguka kuweza kuyafikia mataifa ya nje haraka.

Kuna tani zaidi ya milioni 30 za mizigo mbalimbali inayotakiwa itoke huko bara na kwenda nje ya nchi, huo ni mzigo mwingi sana na kwa aina ya uendeshaji wa kizamani wa bandari tulionao hakuna nafasi ya kitaifa kuweza kuinuka kiuchumi.

Haya ni masuala ya kiuchumi yenye kutaka ufafanuzi wa kina wa kiuchumi, huu sio wakati wa kufikiria kizamani halafu matokeo ya ufikiriaji huo yawe na mashiko kwenye maisha ya kisasa.
Nani alikuambia sisi hatuwezi? Au kwa kuwa sisi ni wezi!, Kwa nini tusikodishe menejimenti wakati tunajenga uwezo wa kuendesha wenyewe? Kwa utaratibu huo unadhani lini tutakuwa na uwezo wa kuendesha wenyewe? Tusiwe wajinga hao tunaodhani wanaweza Kuna mahali walianzia hapo ndio tunapataka. Zamani tuliambiwa hatuwezi kujenga Barbara ya Rami Leo tunaweza baada ya mkapa kuthubitu,tuliambiwa hatuwezi kujenga BWAWA la Nyerere Magufuli akathubutu tunaelekea kuweza kwa mifano hiyo hakuna tusichoweza.
 
Wakili huyu kwanini anaandamwa sana na serikali hii? Ana siri gani anazozijua wakihofu kuendelea kuzilipua hadharani hadi wakeshe wakifikiria namna ya kumrejesha gerezani? Kwanini wananchi wasiamini serikali hii imejaa uonevu kwa kutumia kichaka cha demokrasia ambayo ni garasha tupu?

Serikali acheni kumtesa wakili huyu kutokana na madhaifu yenu na watu wenu

Naona mama ameamua kuwa kama Magufuli.
Ni mwendo wa kuwashughulikia wote wanaokosoa utendaji wa Serikali yake.

Ameamua kuvaa rasmi viatu vya mwendazake
 
Huo ushindani wa wazi wa namna ya kuwapata waendeshaji hizo gati wenye tija ya kiuchumi na viwango vya ubora vya mikataba yenyewe hata kama unakodisha ndiyo matatizo yanakoanzia. Huo uchumi wa wapi unaousema?
Njia ya manunuzi iliyompata DP World ni single source procurement method, ilitumika baada ya TPA kugundua kuwa mwarabu ndio mwenye mzigo kule Rwanda na DRC hivyo hapakuwa na sababu ya kumshindanisha na washindani wengine.

Ni kampuni yenye faida tayari kwa mamlaka ya bandari kwa maana ya kuwa na teknolojia za kisasa za ushushaji na upakiaji wa mizigo, unapomshindanisha unaweza kumpata mwekezaji mwenye mipango tofauti na DP World na ukaikosa tenda kubwa ya mizigo yake anayotarajia kuipitisha kwenye SGR yetu iliyojengwa kwa matrilioni ya pesa.

Hayo magati mengine na bandari nyingine zinatangazwa tenda kwa mtindo tofauti kwa sababu mazingira ya kibiashara na kiuendeshaji yatakuwa tofauti na yale yaliyompa DP World nafasi ya moja kwa moja ya kuendesha sehemu ya bandari yetu.
 
Nani alikuambia sisi hatuwezi? Au kwa kuwa sisi ni wezi!, Kwa nini tusikodishe menejimenti wakati tunajenga uwezo wa kuendesha wenyewe? Kwa utaratibu huo unadhani lini tutakuwa na uwezo wa kuendesha wenyewe? Tusiwe wajinga hao tunaodhani wanaweza Kuna mahali walianzia hapo ndio tunapataka. Zamani tuliambiwa hatuwezi kujenga Barbara ya Rami Leo tunaweza baada ya mkapa kuthubitu,tuliambiwa hatuwezi kujenga BWAWA la Nyerere Magufuli akathubutu tunaelekea kuweza kwa mifano hiyo hakuna tusichoweza.
Dunia ya kisasa haikusubiri wewe mpaka uweze kujiendesha mwenyewe. Sababu za mheshimiwa Rais kuamua kuja na mfumo wa kisasa wa Landlord Port ni kuweza kuendana na ushindani wa bandari wa kidunia.

Sisi hao hao tunaolilia kujiendesha ndio hao hao ambao CAG kila kukicha anatoa report chafu anapofanya ukaguzi!.

Kumbuka kuwa mojawapo ya masharti ya kimkataba aliyowekewa DP World ni kuhakikisha anatoa elimu ya masuala ya usafirishaji wa majini kwa vijana wetu. Ni kuhakikisha anaendeleza uwezo wa vyuo vya bandari.

Mawazo ya kijamaa mara nyingi yanakosa mashiko kwenye dunia halisi, ni njozi zenye kudanganya watu kupitia akili za 'sisi tunaweza'.

Si ajabu mwanazuoni mmoja wa Marekani aliwahi kusema Ujamaa huishiwa nguvu pale watoa pesa wanaposhindwa kuendelea kuhudumia uchumi wa nchi.
 
Back
Top Bottom