Polisi: Tumewakamata watuhumiwa waliokula njama ya kutaka kumteka Tarimo - Kiluvya

Polisi: Tumewakamata watuhumiwa waliokula njama ya kutaka kumteka Tarimo - Kiluvya

Hahababaa 2qtqnzania banaa.....tunachezewa sana akili z4tu wengi ni ..........wote wale wanajulikana na majina yao na vitengo vyao....wanahamisha magoli...hahaha khaaaa acha nicheke
 
Siku 23 tangu video za jaribio la kutaka kumteka Deogratius Tarimo, mkazi wa Kiluvya jijini Dar es Salaam zisambae, hatimaye Jeshi la Polisi limesema linawashikilia watuhumiwa wanane wa tukio hilo.

Taarifa ya kushikiliwa kwa watu hao imetolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Jumanne Muliro leo Jumanne, Desemba 4, 2024.

"Tarehe 11 Novemba, 2024 eneo la Kiluvya, Ubungo Dar es Salaam lilitokea tukio la kutekwa kwa Deogratius Tarimo, mfanyabiashara na mkazi wa Kibaha mkoani Pwani.

"Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imefanikiwa kukamata kundi la watu wanane wanaotuhumiwa kula njama kwa pamoja na baadaye kufanya tukio la kumteka Deogratius Tarimo. Watuhumiwa wamekamatwa kwa nyakati tofauti Dar es salaam, Songea Ruvuma na eneo la Mbingu Mlimba, Morogoro,"imeeleza taarifa hiyo.

Pia imeongeza kuwa: "lilipatikana gari aina ya Toyota Raum ambayo ilitumiwa wakati wa tukio hilo, huku ikitumia namba isiyo halisi T 237 EGE na baada ufuatiliaji namba halisi ya gari hiyo ni T237 ECF."

Taarifa hiyo imewataja watuhumiwa hao kuwa ni Bato Bahati Tweve (32), Bondia, mkazi wa Kimara Bunyokwa na Songwe Mbozi, Yusuph Abdallah (32), mkazi wa Mbingu Mlimba, Morogoro, Fredrick Juma (31), mkazi wa Kibamba na Nelson Elimusa (24) maarufu msela, dereva teksi, mkazi wa Mbezi Luguluni.

Wengine ni Benk Daniel Mwakalebela (40) maarufu tall, mkazi wa Mbezi -Makabe na Kyela Ipinda, Rusungo Mbeya, Thomas Ephraim Mwakagile (45) maarufu Baba Mage, mkazi wa Bunyokwa na Kyela Ngonga Ndiali- Mbeya, Anitha Alfred Temba (27), mkazi wa Mbezi Mwisho na Isack Mwaifani, maarufu boxer, mkazi wa Kimara Tembo Salanga na Bujonde Isanga Kyela, Mbeya.
 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linaendelea na operasheni maalum kali ya kuzuia vitendo vya kihalifu maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam. Kwa ujumla hali ya usalama Dar es Salaam inaendelea vizuri.

Tarehe 11 Novemba, 2024 eneo la Kiluvya Ubungo Dar es Salaam lilitokea tukio la kutekwa kwa Bw. Deogratius Tarimo, mfanyabiashara na mkazi wa Kibaha Mkoa wa Pwani. Kufuatia tukio hilo na mengine ya nyuma Polisi Dar es salaam imekuwa ikiendelea kuchunguza na kufuatilia taarifa mbalimbali pia kukusanya ushahidi wa kisheria kuhusiana na matukio hayo ili kuyazuia.

Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam imefanikiwa kukamata kundi la wahalifu wanane wanaotuhumiwa kula njama kwa pamoja na baadae kufanya tukio la kumteka Deogratius Tarimo. Wat uhumiwa hao wamekamatwa kwa nyakati tofauti Dar es salaam, Songea Ruvuma na eneo la Mbingu Mlimba Morogoro. Pia lilipatikana gari aina ya Toyota Raum ambayo ilitumiwa wakati wa tukio hilo huku ikitumia namba isiyo halisi T 237 EGE na baada ufuatiliaji namba halisi ya gari hiyo ni T237 ECF.

Watuhumiwa hao ni :-

1. Bato Bahati Tweve, Bondia, Miaka 32, Mkazi wa Kimara Bunyokwa na Songwe Mbozi

II. Yusuph Abdallah, Miaka 32, Mkazi wa Mbingu - Mlimba Morogoro

III. Fredrick Juma, Miaka 31, Mkazi wa Kibamba

IV. Nelson Elimusa msela, Dereva Tax, Miaka 24, Mkazi wa Mbezi Luguluni

V. Benk Daniel Mwakalebela@tall, Miaka 40, Mkazi wa Mbezi Makabe na Kyela Ipinda

Rusungo Mbeya

VI. Thomas Ephraim Mwakagile @ baba mage Bunyokwa na Kyela Ngonga Ndiali Mbeya Miaka 45, Mkazi wa Kinyerezi

VII. Anitha Alfred Temba, Miaka 27, Mkazi wa Mbezi Mwisho.

VIII. Isack Mwaifani, @ boxer, Mkazi wa Kimara Tembo Salanga na Bujonde Isanga Kyela Mbeya

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linaendelea na kazi ya kuzuia vitendo vya kihalifu lakini pia kuwakamata na kutokuwa na huruma kwa watuhumiwa wote wanaojihusisha na matukio ya kihalifu ikiwa ni pamoja na kuwashughulikia kwa mujibu wa sheria kwa kuwapeleka kwenye mamlaka zingine za haki.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutoa taarifa za kweli ili Jeshi lichukuwe hatua za kisheria kwa watu wanaopanga kufanya matukio ya kihalifu ili washughulikiwe mapema kabla ya matukio.

Imetolewa na;
Muliro J. Muliro -SACP
Kamanda Kanda Maalum ya Polisi
Dar es Salaam
www.polisi.go.tz
www.twitter.com/tanpol

Kutoka hapa sijui picha linaepekea wapi, naahindwa kulitabiri
 
Taarifa ya kushikiliwa kwa watu hao imetolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Jumanne Muliro leo Jumanne, Desemba 4, 2024.

"Tarehe 11 Novemba, 2024 eneo la Kiluvya, Ubungo Dar es Salaam lilitokea tukio la kutekwa kwa Deogratius Tarimo, mfanyabiashara na mkazi wa Kibaha mkoani Pwani.
Huwa wana kawaida ya kuwapiga picha na kuwaweka hadharani basi tunaomba hata hao wapigwe picha na kuwekwa hadharani ili raia wawatambue kama watu hatari iwapo wataonekana mtaani
 
Polisi imesema imewakamata Watu 8 kufuatia tukio la kutaka kumteka Mh Tarimo Bonge wa Kiluvya

Source: Ayo TV
 
Back
Top Bottom