Prof. Janabi: Kujifungua Mtoto 'Bonge' si nzuri Kiafya

Proffesa kanena vyema,Ila hapo kwenye sababu za matatizo ya Figo ndipo kapuyanga! kushindwa kumweleza ukweli tu Bwana Joseph Haule na wengineo,wengi wanaosumbuliwa na matatizo yanayofanana na hayo kuwa unywaji wa pombe uliopitiliza ndio Sababu! proffesa vp Tena?
calling a spade,spade not a big spoon
 
Mkitukanwa mnalalamika. Sasa hapo umejibu nini? Nakuuliza tena, yapi madhara ya kunywa maji mengi?
Figo haziwezi chuja maji endapo utakunywa mengi sana, zitazidiwa. Ukinywa maji mengi kiasi figo huchuja madini yabaki mwilini na maji ya ziada pamoja na takamwili zitoke nje kama mkojo.
Ukinywa maji mengi figo zitazidiwa utatoa maji nje yakiwa na madini kama Sodium yanayohitajika kwenye damu. Mwili utazidiwa maji utatapika, kupata kizunguzungu, ubongo kushindwa kufanya kazi vizuri mfano ukasahau kitu, kujishikiza uvivu, kuzirai au na kupelekea hadi kufariki.
 
Mtoto akitoka mdogo nayo inakuwa nafuu kwa mama kusukuma, sasa akiwa bonge si ndio maumivu makubwa ikiwemo kuchanika msamba? Wamama wale vyakula bora wakati wakiwa wajawazito
Haya mambo wazee walishayaona hata kabla ya ujio wa wakoloni.

Ndipo tulisikia masharti ya kuwatia hofu ili wasile vyakula fulani fulani maana hakukuwa na data za kisayansi za kuwasaidia waache uroho kipindi cha ujauzito.

Ndio maana kukawa na miiko ya ulaji. Mfano mjamzito alikatazwa kulanvyakula vya protini kama samaki, mayai, nyama, kipindi cha ujauzito ila walimkazania sana ulaji wa vyakula vya wanga, matunda na mboga za majani.

Waliwapa shuhuda za kutisha kama watoto kufia tumboni, au kuzaliwa hawana nywele/viparang'oto, watoto kuwa wafupi, etc.

Sayansi ilikuwapo Africa tena muda mrefu sana ila ni vile tulichagua kuipuuza.
 
Hahaaaa, wacha weeeee. Kwahiyo kunywa maji yanaweza sababisha umauti?
 
Kwanza ajiangalie yeye mwenyewe afya gani ile, ashukuru ana kazi nzuri na anafanya kazi kwenye sekta ya afya tofauti na hapo iko afya nzuri
 
BIG BABY
 
ndiyo!
ndio maana japokuwa kila mmoja atakufa Ila tukitembea barabarani hatupiti katikati.
Unadhani watu hawapiti katikati sababu ya kifo? Sababu si kifo bali ni hakuna maslahi wala utamu wowote kupita katikakati ya barabara.

kifo huogopwa na wengi pale tu kisababishi cha hicho kifo kinapokosa maslahi au utamu.


Kama huamini Tangaza dau la malipo kwa kila anayepita katikati ya barabara uone kama hutapata wahusika wengi au ondoa utamu kwenye uke uone kama ukimwi utakuwa ni tatizo tena, Ondoa utamu kwenye junk food uone kama presha, kisukari itakuwa ni tatizo tena.

Suala si kifo, suala ni kisababishi cha kifo kina maslahi au utamu? Kama hakina kitaogopwa.
 
Nimewahi kumuuliza mnywa maji mmoja, kwanini anakunywa maji lita karibu 5 kwa siku anayapeleka wapi?


Akanijibu kuwa mwanadamu anatakiwa kunywa hizo lita 5 kwa siku.

Nikamwambia sidhani kama ni kweli (japo mimi si mtabibu) sababu wanadamu tuna miili tofauti, haiwezekani mimi wa kg 70 ninywe maji sawa na mtu mwenye kg 100 au kg 45.

Naamini labda hawa watamsaidia ndugu yangu yule. Maana naona anavyouchosha mwili wake bila yeye kujua.
 
Mie nikiwa mjamzito nakula kama kiwavi jeshi tena chips ni kila siku na hua naongezeka uzito wa kutosha lakini watoto wangu hamna aliyevuka 3.3kg. Sijui chakula kinapoteleaga wapi kama anavyosema profesa maana kula hua nakula kweli kweli tena carbs
 
Mie nikiwa mjamzito nakula kama kiwavi jeshi tena chips ni kila siku na hua naongezeka uzito wa kutosha lakini watoto wangu hamna aliyevuka 3.3kg. Sijui chakula kinapoteleaga wapi kama anavyosema profesa maana kula hua nakula kweli kweli tena carbs
Ukila na watoto wanakula sasa usiulize chakula kinaenda wapi maana unakua haupo peke yako Mama mjamzito unakua umebeba kiumbe kingine,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…