Mia ya noti
JF-Expert Member
- Dec 30, 2018
- 866
- 1,234
Lakini si hii hii ccm iko madarakani kwa miaka sitini? Walishindwa nini kuundoa huo umasikini mpk leo iwe issue ya dharura?Uko sahihi hyo katiba ni nani anaitaka kabla umaskini haujaondolewa wanasiasa wanakuja na agenda zisizogusa Raia Moja kwa moja.
Na hawa waliopo wanakataa katiba mpya ili kulinda madaraka yao? AuProf Yuko sahihi katiba haiwezi kumaliza umaskini simply kwa kuwa tu na katiba, wanasiasa wanaililia kisa madaraka Yao.
Narudia tena, takwa la katiba sio takwa la wananchi walio wengiMatakwa ya watu yanawezaje kuheshimiwa ikiwa takwa la katiba mpya hamliheshimu? Hivi nyinyi mataga mbona huwa akili zenu mnapenda kushikiwa?
acha uongo professor katiba mpya ndio kila kitu.Msomi nguli wa Tanzania Prof Issa Shivji amelichambua dai la katiba mpya na kusema halina tija wala si mwarobaini wa matatizo yanayowakumba watanzania kwa sasa.
Prof Shivji amesema wanasiasa wanapenda madaraka na siyo siasa safi na kuwatumikia wananchi, ametolea mfano kwa vita ya madaraka inayoendelea nchini Kenya na Afrika Kusini licha ya kubadili katiba mara kwa mara.View attachment 1838690
Huku kenya tuna katiba mpya,kwa ujumla maisha ni mazuri sana,,kila mtu huku ana maisha ya kati,,usafiri mzuri,nyumba za kisasa na hospital za kupigana na magonjwa,,ndo maana viongozi wa nje wakipata corona huletwa Nsirobi,,katiba imetukomboa sanaAtuambie basi huo mwarobaini
Ova
Hapana. Mimi siyo CHADEMA. Ila wewe hukuelewa. Maana yake ni kuwa Katiba Mpya pekee haitoshi, lakini ni ya lazima. Not sufficient but necessary.chadema wataelewa tu sasa maana kila mtu waliyemtegemea atawageuka wanaonekana hawana subira
KILA KITAFUTWACHO KINA FAIDA. ANAYEKIPATA AWE NA SIFA NA IWE NI HALALI NA HAKI. KILA CHAMA CHA SIASA LENGO NI MADARAKA HATA CCM. SASA KWA KUWA WOTE HUTAKA NA WANAHAKI SAWA. APATAYE KWA KUWASHINDA WENGINE IWE NI KWA UHALALI NA HAKI INAYOONEKANA. WASHINDWAWO WAMSHIKE MKONO NA KUMPONGEZA ALIYESHINDA. HAPO NDIPO TUNAPOTAKA WOTE. NA NJIA NI KUPATA KATIBA MPYA AU KUREKEBISHA KATIBA ILIYOPOumeonyeshwa africa ya kusini wana katiba bora lakini haijamaliza walichokuwa wanakifikiria hapa kilichopo siyo katiba mpya ni uchu wa madaraka tu
Alafu ukishapata tume huru....Katiba Mpya itatupa Tume HURU ya Uchaguzi japokuwa sio Mwarobaini wa matatizo yetu ila itayapunguza kwa kiasi kikibwa.
Hata kama katiba mpya si mwarobaini, ukweli kwamba bado inahitajika uko palepale.Katiba siyo lazima iwe mwarobaini ambao inasemekana unatibu magonjwa arobaini.
Katiba hata ikiwa panadol inatosha kabisa kutuondolea headache!
Professa amechemsha. Wasomi wetu hovyo sana. Wao ndiyo chanzo cha matatizo tuliyonayo kama Taifa. Hawana msaada zaidi ya maji gambol na Matumbo yao tuu.
Ni kipimo gani kitakachotumika kujua kama mbunge ana-perform au laa?? Ni nani atakuwa mpimaji wa hiyo performance?1. Kwa upande wangu, Katiba Mpya (hasa ile iliyopendekezwa na tume ya Warioba) ni msingi wa kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya Watanzania kwa sababu imeweka misingi mizuri na thabiti ya uongozi wa nchi na uwajibikaji wa viongozi wengine wa umma kwa wananchi. mfano, mbunge asipoweza ku'perform' wananchi wana haki na nguvu ya kumwondoa na kumchagua mwingine anaye'perform'.
2. Kama Katiba Mpya ni nzuri, hata sera, sheria na kanuni zitakazotungwa zitakuwa nzuri pia.
3. Ukisema Katiba Mpya siyo mwarobaini wa matatizo yetu, ina maana hata hayo mambo mengine ambayo Prof Shivji anadhani ndiyo mwarobaini nayo hayatakuwa mwarobaini.
4. Hii ina maana kwamba Katiba Mpya nzuri inaweka utaratibu mzuri au ni mahali pazuri pa kuanzia na haina maana kwamba tukishakuwa na hiyo Katiba Mpya basi mambo mengine yasifanyike.
5. Nilimsikia akitolea mfano nchi kama Afrika Kusini na Kenya (na pia Uganda) kwamba ndizo zenye Katiba nzuri sana Afrika, lakini mbona zina matatizo as if hakuna nchi duniani zenye Katiba nzuri ambazo mambo yao yanaenda vizuri. Ni kama kusema kwa vile mama akijifungua anapata maumivu, basi kujifungua siyo kuzuri. Au kwa vile ndege huwa zinapata ajali, basi usafiri wa ndege siyo salama au kwa vilevile kuna wanandoa wanaoachana basi kuoa siyo kuzuri au hakufai. Kwa nini Prof hakutolea mfano nchi zenye Katiba nzuri na zinafanya vizuri? Ni kama Katiba Mpya (yaani tukiwa na Katiba nzuri bora kuliko tuliyonayo) mambo yatazorota zaidi kuliko ilivyo sasa. Mimi naona kama ni starting point inayotupa direction ya kuboresha pia maeneo mengine kwa sababu tayari tunakuwa na msingi mzuri wa kuanzia ujenzi wa taifa letu.
Watawala wapya ili waje wafanye nini?? Nchi inataka maendeleo haina shida na watawala. Kama shida ni watawala basi wapo wengi sanaTume huru itatuletea watawala wapya......
Wanasiasa wote mnatetea masilahi yenuNa hawa waliopo wanakataa katiba mpya ili kulinda madaraka yao? Au
Umaskini Africa ni janga we lack visionary leader with good strategy ya kutuvisha as a result nchi zote tuliokuwa nazo maskini in 1960 Sasa zimekuwa developmental state, nchi ka china, Malaysia wamepita hatua kubwa tu. Swala ni kuamuaLakini si hii hii ccm iko madarakani kwa miaka sitini? Walishindwa nini kuundoa huo umasikini mpk leo iwe issue ya dharura?
Labda kweli kama raia wa kenya anaweza kupewa uongozi tz unataka kitokee kitugani hapoMsomi nguli wa Tanzania Prof Issa Shivji amelichambua dai la katiba mpya na kusema halina tija wala si mwarobaini wa matatizo yanayowakumba watanzania kwa sasa.
Prof Shivji amesema wanasiasa wanapenda madaraka na siyo siasa safi na kuwatumikia wananchi, ametolea mfano kwa vita ya madaraka inayoendelea nchini Kenya na Afrika Kusini licha ya kubadili katiba mara kwa mara.View attachment 1838690
Hali za watu ziwe vizuri kisha ndio wanasiasa wapewe sinia la nyamaπππ sasa nyie wapeni ulaji halafu ndio mtaelewa kazi! Watapiga hela hadi wafie Madarakani
Sindio maana mivutano haiishi watu wanagombea collection plates wametuweka wananchi kama bonds! πππ..nilidhani wanasiasa wameshapewa sinia la nyama kwa katiba hii mbovu tuliyonayo.
..unadhani walioko madarakani sasa hivi hawapigi pesa? unadhani wana mipango ya kuondoka madarakani hivi karibuni?