Prof Shivji: Katiba mpya siyo mwarobaini wa matatizo ya watanzania

Prof Shivji: Katiba mpya siyo mwarobaini wa matatizo ya watanzania

Hawa Chadema agenda yao imegundulika.

Mama anahangaika na namna ya kuwaletea Watanzania maendeleo sio huu upuuzi.
Kikubwa maswala ya uchumi na kuondoa umaskini basi hayo ndo ya msingi kwa mtanzania sio blah blah katiba
 
Uko sahihi hyo katiba ni nani anaitaka kabla umaskini haujaondolewa wanasiasa wanakuja na agenda zisizogusa Raia Moja kwa moja.
Hali za watu ziwe vizuri kisha ndio wanasiasa wapewe sinia la nyama😂😂😂 sasa nyie wapeni ulaji halafu ndio mtaelewa kazi! Watapiga hela hadi wafie Madarakani
 
Hatuna Haja ya katiba mpya kwa sasa hao wansotaka katiba na demokrasia mwenyekiti wao ana miaka 30 madarakani sasa kama yeye kashindwa kuheshimu demokrasia na katiba ya kwenye chama chake je ataweza kuheshimu katiba ya Tanzania?
TUSIDANGANYIKE.
 
Yeye kama nani wa kuwasemea watanzania na neno lake likawa sheria,anazeek vibaya
 
Professor Shivji ni mwanazuoni Mbobezi anaye heshimika kipindi chote, na huwa hana tabia ya kulopoka, ni msema kweli siyo mnafiki.
naungana mkono na Professor shivji ni kweli kabisa Katiba mpya sio mwarobaini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Finally, someone has spoken the reality.

Ni kweli kuwa na katiba bora ni jambo la muhimu lakini maendeleo na mabadiliko ya kweli yanahitaji zaidi ya katiba.

Kama wanasiasa wataacha unafiki na kuamua kulitumikia taifa na si matumbo yao, kuwatumikia wananchi na si maslahi ya familia zao, marafiki zao na washirika wao basi hatutaona uroho na ulafi wa madaraka, hatutaona sheria za ajabu ajabu zikitungwa, hatutaona watu wakiwa busy kutafuta loop holes ili kupiga dili. Maana kama mtu anaweza kushawishi watu wakabadili katiba ya chama ili iendane na matakwa yake au malengo yake ni kujidanganya kudhani mtu huyo huyo akipewa dhamana ya kuongoza Taifa hata kama kuna katiba nzuri vipi hatajaribu kubadilisha baadha ya maeneo ili kuhakikisha maslahi yao yanalindwa hili tunalishuhudia kenya sasa.
 
Msomi nguli wa Tanzania Prof Issa Shivji amelichambua dai la katiba mpya na kusema halina tija wala si mwarobaini wa matatizo yanayowakumba watanzania kwa sasa.
Prof Shivji amesema wanasiasa wanapenda madaraka na siyo siasa safi na kuwatumikia wananchi, ametolea mfano kwa vita ya madaraka inayoendelea nchini Kenya na Afrika Kusini licha ya kubadili katiba mara kwa mara.View attachment 1838690
Huyu mzee sasa kachoka hana jipya tena ni kigeugeu kwa ajili ya njaa zake, akae nyumbani kulea wajukuu
 
Angalau tuanzie kwa katiba mpya.....tume huru mengine yatakuja....
 
Katiba Mpya itatupa Tume HURU ya Uchaguzi japokuwa sio Mwarobaini wa matatizo yetu ila itayapunguza kwa kiasi kikibwa.
TUNAWEZA kupata TUME HURU bila kusumbuka na mchakato mrefu wa Katiba Mpya
 
Katiba yetu ya sasa siyo mbaya kama tunavyoaminishwa, ina mapungufu kadhaa ambayo tume ya Nyalali iliyabainisha wakati tunaingia mfumo wa vyama vingi.

Pamoja na tume ya Warioba kusifiwa ilifanya kosa moja kubwa, haikuipa kinga katiba yetu hapo namaanisha bado haikuondoa kinga ya rais kushitakiwa ikiwa amevunja katiba.

Kinachotakiwa wananchi waelimishwe kuhusu katiba ili ukifika wakati wa kufanya mabadiriko tujikite kwenye ajenda muhimu badala ya kujikita kwenye ajenda za kisiasa pekee.

Katiba ni zaidi ya siasa ni dira ambayo itatuongoza na sio kung'ang'ania siasa pekee.
 
TUNAWEZA kupata TUME HURU bila kusumbuka na mchakato mrefu wa Katiba Mpya
556.jpg

Tunaweza kupewa kweli?
 
Finally, someone has spoken the reality.

Ni kweli kuwa na katiba bora ni jambo la muhimu lakini maendeleo na mabadiliko ya kweli yanahitaji zaidi ya katiba.

Kama wanasiasa wataacha unafiki na kuamua kulitumikia taifa na si matumbo yao, kuwatumikia wananchi na si maslahi ya familia zao, marafiki zao na washirika wao basi hatutaona uroho na ulafi wa madaraka, hatutaona sheria za ajabu ajabu zikitungwa, hatutaona watu wakiwa busy kutafuta loop holes ili kupiga dili. Maana kama mtu anaweza kushawishi watu wakabadili katiba ya chama ili iendane na matakwa yake au malengo yake ni kujidanganya kudhani mtu huyo huyo akipewa dhamana ya kuongoza Taifa hata kama kuna katiba nzuri vipi hatajaribu kubadilisha baadha ya maeneo ili kuhakikisha maslahi yao yanalindwa hili tunalishuhudia kenya sasa.
Umenena
 
Tume huru ni nini na inatatuaje matatizo ya watanzania?

Muhimu watawala waheshimu matakwa ya watu.
Kwa ninavyojua katiba mpya italazizimisha tume huru ambayo italazimisha watawala waheshimu watakwa ya watu.

Lakini prof. Shivji anasema katiba si muarobaini wa matatizo ya watanzania. Ilibidi tusome andiko la muandishi ndo tungeweza kuchambua vizuri. Lazima prof atakuwa ameelezea alternative source ya muarobaini wa matatizo ya watanzania. Au muandishi kanjanja wa jamvi la habari anataka tu kutoa watu kwenye reli. Unaweza kusoma na heading na habari yenyewe ni tofauti kabisa.
 
Msomi nguli wa Tanzania Prof Issa Shivji amelichambua dai la katiba mpya na kusema halina tija wala si mwarobaini wa matatizo yanayowakumba watanzania kwa sasa.
Prof Shivji amesema wanasiasa wanapenda madaraka na siyo siasa safi na kuwatumikia wananchi, ametolea mfano kwa vita ya madaraka inayoendelea nchini Kenya na Afrika Kusini licha ya kubadili katiba mara kwa mara.View attachment 1838690
Chanzo ni Jamvi la Habari!!!???
Nitajadili hiyo kauli pale nitakapoona video au kumsikia Prof. Shivji akitamka hayo.
 
Wapumbavu Sana ,Iq zero , imagine mpumbavu kama huyo eti anakuambia katiba ina umuhimu gani katika kutafuta changamoto za kiuchumi na uongozi , jitu kama hilo unadhani lina akili ?
Hao ni misukule tu mkuu. Hawana akili, yani akili zao wameshikiwa kwahiyo hata ku tafakari masuala basic kama haya hawana uwezo. Yani ni ni lightweights watupu, vichwa empty kabisa.
 
Hawa Chadema agenda yao imegundulika.

Mama anahangaika na namna ya kuwaletea Watanzania maendeleo sio huu upuuzi.
Kuwaletea watanzania maendeleo kutoka wapi?
Miaka sitini ya uhuru bado asilimia hamsin ya watz wanaishi chini ya dola mbili.
Ccm isiwe na aibu kusema imeshindwa kuongoza taifa.
 
Back
Top Bottom