Profesa Janabi: Aliyewaambia Watu wawe Wanakunywa Maji Lita 5 kwa Siku kawadanganya sana

Profesa Janabi: Aliyewaambia Watu wawe Wanakunywa Maji Lita 5 kwa Siku kawadanganya sana

Sidhani kama amefanya research yeye kama yeye ila nakubaliana na alichokisema kwani mesikia hizo habari kitambo toka kwa madocta nguli wa huko mbele kama Dr Hyman mark na Dr berg ambao naamini nae kafatilia na kujifunza toka ktk makala za watu kama hao...

Na nadhani siku sio nyingi atakuja na maswala ya intermediate fasting pia jambo ambalo litakuwa zuri pia
Una mashaka na uelewa na medical doctor professor?
 
Miili ya wanadamu hawawezi kulingana kiasi cha mahitaji hasa ya maji.

Kuna watu hawaruhusiwi kunywa zaidi ya nusu lita ya maji kuanzia maji yaliyopo kwenye mlo wao hadi anayoyanywa kama maji yasivuke nusu lita (wanateseka sana)

Kuna watu hata lita 5 ni kidogo kwao

Na kuna watu watakunywa kiasi chochote kinachohitajika bila kulazimisha.

Maji yapo kwenye matunda, mlo wa siku, vinywaji na maji yenyewe. Utajikuta tu unapata kiasi unachohitaji.

Ila glasi 8 au lita 5 kama lazima hii ni propaganda ya hali ya juu. Kwanza inachosha viungo vya ndani ya mwili kufanya kazi isiyo ya lazima.
 
"Unatakiwa kunywa Maji pale tu Mwili wako ukikuambia au ukijisikia kuwa una Kiu.

Na hata kama usiposikia Kiu na kutokunywa Maji bado Afya yako itakuwa imara.

Huwa nashangaa mno kuwaona na kuwasikia Watu wakisema kuwa Mwanadamu kwa Siku anatakiwa Kunywa Maji Lita 5 hii si sahihi na wengi wanaokunywa Maji ya Ujazo huo hujikuta wakiwa wameibua Magonjwa mengine Miilini mwao" amesema Profesa Mwenye Akili Nyingi Janabi muda mfupi tu uliopita alipokuwa Mubashara ( Live ) ITV na Radio One katika Kipindi nilichokisahau Jina ila Mtangazaji Miongozaji wake Julieth Robert kutokana na Urembo wake na Sauti yake tamu sijamsahau.

Haya sasa endeleeni tu Kufakamia Mimaji Lita 5 na Kubeba Michupa yenu hovyo barabarani kama Wendawazimu mkijidanganya kuwa mnaimarisha Afya zenu wakati akina GENTAMYCINE tunaokunywa Glasi Tatu ( 3 ) tu za Maji tunaendelea kuwa Werevu (Intelligents) na Afya zetu Kuimarika kila Uchao na Kuonekana bado ni Vijana wakati sasa tunaelekea Saa 12 Jioni.

Kazi Kwenu.
wazee,
mchongo pesa pia inalipa
 
Janabi nae fix tu.
Mpaka kusikia kiu maana yake ushauchelewesha mwili kuupa maji, si vyema kunywa maji eti baada ya kuhisi kiu.

Pili.
Maji mtu anakunywa kutokana na uzito wake.

Ni kweli lita 5 ni nyingi mnoo, lakini lita 2-3 inabidi tunywe kwa siku kwa mtu mzima.. hapo factor ya kazi(kuutumikisha mwili) tumeweka pembeni.
Word...
 
Nashukuru mkuu, japo maelezo ni mengi, jibu la swali langu hakuna.
Je wingi wa maji ni lita ngapi?
Chief Wingi wa Maji unategemeana kati ya mtu na mtu, Umri,Uzito, Wingi wa shughuli au kazi anazofanya ,Na sehemu Ya kimazingira anayoishi..

Mkuu unywaji wa mji mengi Husababisha Kitu kinachoitwa kitaalamu Water intoxication au Hyponatremia .....

Kwasababu unapokunywa maji zaidi ya mwili unachohitaji Unaenda kudilute Sodium na madini mwngine mwilini..
Sasa bahati mbaya kama wewe si mlaji wa vyakula vya kuongeza mineral (Balance diet) unaweza ukasababisha matatizo..
Alichosema GENTAMYCINE ni sahihi sana kwamba ni muhimu kusikiliza mwili wako nini unataka...Mwili kam ukitaka maji Utatoa signal na wewe utakunywa kwa ajili ya Hydration....
Kwa mfano una kilo 40,Una miaka 18 maji lita tano we ya nini?
 
Chief Wingi wa Maji unategemeana kati ya mtu na mtu, Umri,Uzito, Wingi wa shughuli au kazi anazofanya ,Na sehemu Ya kimazingira anayoishi..

Mkuu unywaji wa mji mengi Husababisha Kitu kinachoitwa kitaalamu Water intoxication au Hyponatremia .....

Kwasababu unapokunywa maji zaidi ya mwili unachohitaji Unaenda kudilute Sodium na madini mwngine mwilini..
Sasa bahati mbaya kama wewe si mlaji wa vyakula vya kuongeza mineral (Balance diet) unaweza ukasababisha matatizo..
Alichosema GENTAMYCINE ni sahihi sana kwamba ni muhimu kusikiliza mwili wako nini unataka...Mwili kam ukitaka maji Utatoa signal na wewe utakunywa kwa ajili ya Hydration....
Kwa mfano una kilo 40,Una miaka 18 maji lita tano we ya nini?
Ungesoma comment yangu ya kwaanza kabisa, hicho ulichoandika kimo mule.

Naunga mkono unywaji wa maji kutokana na kilo zako.. ila usinywe mpaka upate kiu kwa maisha yetu haya mbona mtihani saana.

Dr. Nipe hasara za mtu asiyekunywa maji..
 
Maji mengi yanaupotezea mwili madini muhimu wanasema it washes electrolytes... Vinginevyo unywe mineralsed water
Ni kweli, lakini kuna wataalam wanaoelekeza namna ya kunywa maji.
wanasema lita 1 ya maji unatakiwa uinywe ndani ya masaa 4, na usinywe kwa mkupuo, kunywa kiasi cha kizibo cha maji kwa wakati mmoja mara kwa mara ndani ya masaa 4. Kwa style hii maji mengi yanabaki mwilini na unaweza usiyatoe kabisa.
 
Kuna route km 5 za mwanadamu anatakiwa kuzifanya akikosa mojawapo lazima aumwe au magonjwa nyemelezi.
1.kula Chenye rutubisho nyingi,kuna hadi mama mtilie wanapigisha draft la msosi,nyama/samaki kidogo,mboga jani kidogo,maharage,dagaa kidogo.
2.mazeozi kuna watu hata kutembea umbali wa 30min mtu anaona mateso lkn anashinda hospital wkt magonjwa mengine angejitibu mwenyewe.
3.kupata muda wa kulala at least 6hrs iliubongo upumzike and reset. And mwili upumzike.
4.uwe na furaha aka stress release unaweza kwenda sehemu or do what make you happy baada ya mihangaiko migumu ya dunia. At least once per weekend.
5.change mazingira unapnga nyumba km ndio ya urithi hama hata mkoa ukapate new ideas or nenda katembee mimosa mingine like likizo vile
 
Janabi nae fix tu.
Mpaka kusikia kiu maana yake ushauchelewesha mwili kuupa maji, si vyema kunywa maji eti baada ya kuhisi kiu.

Pili.
Maji mtu anakunywa kutokana na uzito wake.

Ni kweli lita 5 ni nyingi mnoo, lakini lita 2-3 inabidi tunywe kwa siku kwa mtu mzima.. hapo factor ya kazi(kuutumikisha mwili) tumeweka pembeni.
Nakuunga mkono, unywaji wa maji uendane na uzito wako lakini pia tukumbuke tunatumia vinywaji vingine kama cola, soda au vileo ambavyo kwa namna au nyingine ni vyema tuzingatie unywaji wa maji ili tusiipe kazi sana figo katika kazi yake


Unakuta mtu anapiga liquid chupa hata nane kwa siku na zaidi! , Kweli na hapo unywe maji vikombe viwili??
 
Nakuunga mkono, unywaji wa maji uendane na uzito wako lakini pia tukumbuke tunatumia vinywaji vingine kama cola, soda au vileo ambavyo kwa namna au nyingine ni vyema tuzingatie unywaji wa maji ili tusiipe kazi sana figo katika kazi yake


Unakuta mtu anapiga liquid chupa hata nane kwa siku na zaidi! , Kweli na hapo unywe maji vikombe viwili??
Ni sahihi kabisa mkuu
 
Ni kweli, lakini kuna wataalam wanaoelekeza namna ya kunywa maji.
wanasema lita 1 ya maji unatakiwa uinywe ndani ya masaa 4, na usinywe kwa mkupuo, kunywa kiasi cha kizibo cha maji kwa wakati mmoja mara kwa mara ndani ya masaa 4. Kwa style hii maji mengi yanabaki mwilini na unaweza usiyatoe kabisa.
nashukuru nimefahamu. Ila kuna matumizi ya water therapy wale wa asubuhi.
 
Ungesoma comment yangu ya kwaanza kabisa, hicho ulichoandika kimo mule.

Naunga mkono unywaji wa maji kutokana na kilo zako.. ila usinywe mpaka upate kiu kwa maisha yetu haya mbona mtihani saana.

Dr. Nipe hasara za mtu asiyekunywa maji..
Nimekuelewa Sana uko sahihi na kingine kuhusu Tanzania Asilimia kubwa Sana Hatuna Mineral Water..
all we have is Purified water.
na ndo maana utakuwa Sijui Afya pure water ,Kili pure water e.tc..
Na ndo Maana pengine amegusa Kundi la watu wengi Tanzania wanaotumia Tap water,Purifying water na Distillied water..
Hasara za mtu asiyekunywa Maji cha kwanza kuliko vyote Ni Dehydration hivyo vingine vinavyofuatia ni complication ya Dehydration
 
Nimekuelewa Sana uko sahihi na kingine kuhusu Tanzania Asilimia kubwa Sana Hatuna Mineral Water..
all we have is Purified water.
na ndo maana utakuwa Sijui Afya pure water ,Kili pure water e.tc..
Na ndo Maana pengine amegusa Kundi la watu wengi Tanzania wanaotumia Tap water,Purifying water na Distillied water..
Hasara za mtu asiyekunywa Maji cha kwanza kuliko vyote Ni Dehydration hivyo vingine vinavyofuatia ni complication ya Dehydration
Hapo tumeelewana mkuu.
 
GENTAMYCINE tunaokunywa Glasi Tatu ( 3 ) tu za Maji tunaendelea kuwa Werevu (Intelligents) na Afya zetu Kuimarika kila Uchao na Kuonekana bado ni Vijana wakati sasa tunaelekea Saa 12 Jioni.
Mkuu hapa mbona umetushupalia sana! Japo hii elimu tumepata kweli, si unajua ujinga bado ni mwingi na shule zetu nyingi ni za kuingia darasani! 😄
 
Back
Top Bottom