Putin asaini waraka wa kuamuru Majeshi ya Urusi kuingia Ukraine kulinda amani majimboni

Putin asaini waraka wa kuamuru Majeshi ya Urusi kuingia Ukraine kulinda amani majimboni

Good job ukraine
Screenshot_2022-02-24-18-04-55-693_com.instagram.android.jpg
 
tulishazoea vita vya panzi furaha kwa kunguru hii sasa kinyume chake sijui.
vita vya kunguru shida kwa panzi.
 
Rais Putin asaini waraka wa kuamuru majeshi ya Russia kuingia Ukraine kulinda amani ktk majimbo-yenye-uasi ya Luhansk na Donetsk

Rais Vladimir Vladimirovich Putin wa Russia amesaini tamko rasmi/ decree kuamrisha majeshi ya Russia kuingia nchi Ukraine katika majimbo Luhansk na Donetsk, ambayo Russia inadai ni majimbo asili kwa karne nyingi ingawa yapo nchini Ukraine lakini yanayoiunga mkono Russia, hati hiyo aliyosaini rais Vladimir Putin ni ili kulinda amani toka tishio la majeshi ya Ukraine ambayo bado ni tiifu kwa utawala wa rais wa Ukraine ktk mji mkuu wa Ukraine Kiev / Kyiv .

Rais Putin ametoa tamko hili mubashara ktk televisheni na kusema hatua hiyo ni muhimu ili kulinda majimbo hayo mawili yaliyoamua kujitenga toka Ukraine.

Rais Vladimir Putin ameyatambua majimbo hayo ya Ukraine kuwa ni Jamhuri ya Luhansk na Jamhuri Donetsk ikimaanisha siyo tena majimbo ya Ukraine na hivyo kupeleka msaada wa majeshi ya Russia kutekeleza majukumu aliyoyaita kulinda amani.

Ikulu ya White House Marekani imetangaza kuiwekea vikwazo Jamhuri ya Luhansk na Jamhuri Donetsk ya nchini Ukraine huko Umoja wa Ulaya / EU nayo imeitisha kikao cha dharura kufuatia hali hiyo mpya huku nchi zingine za Ulaya zikitoa matamko ya kulaani ubeberu wa Russia dhidi ya Ukraine.

Toka mji wake mkuu wa Kyiv, Ukraine imetaka Umoja wa Mataifa / UN kuitisha kikao cha dharura kufuatia hali hiyo.

Source: Russia MoD

Kwa wiki kadhaa majeshi ya Russia yalionekana kujikusanya karibu ya mipaka ya Ukraine pande za nchi za Russia yenyewe, Belarus, Crimea na bahari ya Black Sea kwa kile Russia ilichosema ni mazoezi ya kawaida ya utayari ya majeshi yake. Lakini majeshi ya utambuzi / intelligence ya nchi za umoja wa majeshi ya Ulaya Magharibi na Marekani wa NATO yalitia shaka hicho kilichoitwa mazoezi ya utayari ya Russia kwa wingi wa majeshi, vifaa vya kivita vya ulinzi wa anga, manowari za kivita, ndege za kijeshi, askari wa miguu, logistics, propaganda kupitia media mbalimbali za habari na mpangilio wa formation ilionesha wazi ni mpangilio wa kuweza kufanya uvamizi wa spidi kubwa na kuwapiga butwaa nchi marafiki za Ukraine.


Source : PBS Newshour

Ikumbukwe nchi ya Russia pia inaikalia asilimia 20% ya nchi ya Georgia toka mwaka 2008 na pia iligema eneo la Ukraine la Crimea mwaka 2014 katika bahari ya Black Sea toka Ukraine kupitia pia kuvamia maeneo ya nchi hizo kijeshi kwa sababu hizo hizo za kulinda amani na kuleta amani. Nchi za magharibi hazikuchukua hatua zozote za kijeshi zaidi ya kulaani hatua hizo za miaka iliyopita ktk nchi za Georgia na Ukraine.

Putin orders Russian troops into Ukraine separatist regions | DW News


Russian President Vladimir Putin has signed a decree to send what he is describing as "peacekeeping troops" into the separatist regions of Luhansk and Donetsk. The decision comes after Putin recognized both regions as independent states and described Ukraine as ancient Russian territory. The move could mark a significant escalation amid fears Russia could soon launch a full-scale invasion of Ukraine.

Source : DW News


Updates:

24 February 2022
Kharkiv, Ukraine

Mji maarufu wa kimkakati wa viwanda vikubwa wa Kharkiv Ukraine kama matrekta maarufu XTZ-243 yenye nguvu n.k ulioanzishwa na utawala ya Stalin wa USSR 1930-31 umeamka huku wakisikia milio mikubwa ya milipuko. Jimbo la Mji huu wa kimkatati wa viwanda upo mpakani na Russia

War in Ukraine: Explosions in Kyiv, Kharkiv as Russia launches invasion • FRANCE 24 English



People in Kyiv awoke to the sound of explosions and air-raid sirens this morning as Russia launched a military offensive into Ukraine, with similar scenes in major cities across the country as Russian artillery struck airports and infrastructure.
Source : France24
Tulia ww
Screenshot_2022-02-24-18-04-55-693_com.instagram.android.jpg
 

Hatari sasa vita imeingia ktk majukwaa mbalimbali ya media, yaani ni propaganda kila upande wa mvamizi kwa kisingizio cha 'kulinda Amani' na aliyevamiwa nchini kwake wote wanatumia njia zote mbadala kushinda ktk uwanja wa vita na pia uwanja wa propaganda kupitia media zote ili kujenga mshikamano ktk raia pia jeshi, kuongeza morali na kutafuta watakaowaunga mkono kupitia huruma n.k
 
Kwa mara moja ni uongo,mara moja ipi ya kushambulia Kambi zote za jeshi kwenye Kila Nchi at once?

Hizi huwa ni porojo maana hata mashambulizi yanayofanywa sasa yanahisisha makombora ya masafa ya Kati na helicopter kwenda maeneo ya target physically.
Wewe labda you are uninformed Kwa taarifa yako Russia ana ballistic missiles ambazo zinaweza kuhit multiple targets kutoka bara moja na lingine pia anasilaha nyingi za nyuklia ambazo zinatosha kupiga marekani na ulaya Kwa mara moja.
 
Wewe labda you are uninformed Kwa taarifa yako Russia ana ballistic missiles ambazo zinaweza kuhit multiple targets kutoka bara moja na lingine pia anasilaha nyingi za nyuklia ambazo zinatosha kupiga marekani na ulaya Kwa mara moja.
Kwa hiyo zitahit kila Kambi kila Nchi at once 😄😄😄😄😄😄😄
 
Kwa hiyo zitahit kila Kambi kila Nchi at once [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Ndiyo kwakua kuna namna nyingi ya kurusha makombora vita vya nyuklia ikianza dunia yote inaweza kuharibiwa Kwa Muda mfupi.alafu urusi ndo anaongoza kwenye nuclear na ballistic missiles
 
[emoji599] Ukraine’s Zelensky: “Today I asked the 27 leaders of Europe whether Ukraine will be in NATO, I asked directly. Everyone is afraid, does not answer. And we are not afraid, we are not afraid of anything.”
 
Back
Top Bottom