Muuza viatu
JF-Expert Member
- May 14, 2020
- 3,840
- 7,920
Bila shaka NATO na Russia wote madikteta ingawaje wanatofautiana namna wanavyoendesha udikteta wao.Baada ya vita ya pili ya dunia mataifa yenye nguvu yaliapa kutoingia vitani kupigana bila sababu ndo maana ya kuanzishwa umoja wa mataifa.
Urusi kwa wakati huu inatawaliwa na mbabe ambaye hajali taifa lolote kama alivyokuwa Hitler.
Hao wanaoitwa mabeberu ndo wametuwezesha nchi maskini kifikia tulipo. Huwezi kutegemea kutembeza kikombe bila masharti.
Putin Jeuri yake kubwa ni Gas anayoisambazia nchi jirani na ikumbukwe kuwa bomba la gas linapitia Ukraine hivyo basi wale ni mateka wa kiuchumi wa Putin. Ugermani nao wanategemea gas hiyo hiyo ya Putin.
Namtaja Putin sababu kipindi cha Stalin tuliona nchi zote alizozikomboa baada ya Vita ya pili, alizihodhi zote na ndicho chanzo cha Genocide iliyotokea Serbia na Ugoslavia.
Dictator yeyote anachotaka ni kulazimisha kuchuka kwa nguvu. Haya majimbo mawili aliyoyachukua, yalishajitenga na kama tunakumbuka ndege iliyodunguliwa kwenye anga la jimbo lililojitenga, hakuna mtu aliruhusiwa kwenda kutambua maiti au kutafuta chanzo mpaka Putin alipowaruhusu wale waliojitenga kuruhusu wakaguzi na waokoaji kuingia.
Kama mtoa mada anamsifia Putin ajikumbushe hii big donor tulikokuwa tumeishafikia.
Time would have been the right thing to mention. Nyerere angekuwa dikteta kama wengi wanavyofikiria, angeamua kuchukua sehemu ya Uganda kuwa chini ya TZ kama Stalin na Putin walivyofanya.
NATO waliivamia nchi huru za Iraq,syria na afghaaanistan kwa sabab za mchongo na kuondoa utawala uliopo madarakan tena kwa upande wa Iraq viongoz waandamiz wa NATO walikir hadharan kuwa sabab za kuivamia Iraq zilikua za mchongo.
NATO kwa kutumia midege yao huwa wanafanya mashambuliz ya anga ktk nchi huru tena bila ya ridhaa nchi husika na kuua watu kiholela kwa kisingizio cha ugaid na kuishia kuua raia wasio na hatia.