Rais Putin asaini waraka wa kuamuru majeshi ya Russia kuingia Ukraine kulinda amani ktk majimbo-yenye-uasi ya Luhansk na Donetsk
Rais Vladimir Vladimirovich Putin Putin wa Russia amesaini tamko rasmi/ decree kuamrisha majeshi ya Russia kuingia nchi Ukraine katika majimbo Luhansk na Donetsk, ambayo Russia inadai ni majimbo asili kwa karne nyingi ingawa yapo nchini Ukraine lakini yanayoiunga mkono Russia, hati hiyo aliyosaini rais Vladimir Putin ni ili kulinda amani toka tishio la majeshi ya Ukraine ambayo bado ni tiifu kwa utawala wa rais wa Ukraine ktk mji mkuu wa Ukraine Kiev / Kyiv .
Rais Putin ametoa tamko hili mubashara ktk televisheni na kusema hatua hiyo ni muhimu ili kulinda majimbo hayo mawili yaliyoamua kujitenga toka Ukraine.
Rais Vladimir Putin ameyatambua majimbo hayo ya Ukraine kuwa ni Jamhuri ya Luhansk na Jamhuri Donetsk ikimaanisha siyo tena majimbo ya Ukraine na hivyo kupeleka msaada wa majeshi ya Russia kutekeleza majukumu aliyoyaita kulinda amani.
Ikulu ya White House Marekani imetangaza kuiwekea vikwazo Jamhuri ya Luhansk na Jamhuri Donetsk ya nchini Ukraine huko Umoja wa Ulaya UE nayo imeitisha kikao cha dharura kufuatia hali hiyo mpya huku nchi zingine za Ulaya zikitoa matamko ya kulaani ubeberu wa Russia dhidi ya Ukraine.
Toka mji wake mkuu wa Kyiv, Ukraine imetaka Umoja wa Mataifa / UN kuitisha kikao cha dharura kufuatia hali hiyo.
Source: Russia MoD
Kwa wiki kadhaa majeshi ya Russia yalionekana kujikusanya karibu ya mipaka ya Ukraine pande za nchi za Russia yenyewe, Belarus, Crimea na bahari ya Black Sea kwa kile Russia ilichosema ni mazoezi ya kawaida ya utayari ya majeshi yake. Lakini majeshi ya utambuzi / intelligence ya nchi za umoja wa majeshi ya Ulaya Magharibi na Marekani wa NATO yalitia shaka hicho kilichoitwa mazoezi ya utayari ya Russia kwa wingi wa majeshi, vifaa vya kivita vya ulinzi wa anga, manowari za kivita, ndege za kijeshi, askari wa miguu, logistics, propaganda kupitia media mbalimbali za habari na mpangilio wa formation ilionesha wazi ni mpangilio wa kuweza kufanya uvamizi wa spidi kubwa na kuwapiga butwaa nchi marafiki za Ukraine.
Source : PBS Newshour
Ikumbukwe nchi ya Russia pia inaikalia asilimia 20% ya nchi ya Georgia toka mwaka 2008 na pia iligema eneo la Ukraine la Crimea mwaka 2014 katika bahari ya Black Sea toka Ukraine kupitia pia kuvamia maeneo ya nchi hizo kijeshi kwa sababu hizo hizo za kulinda amani na kuleta amani. Nchi za magharibi hazikuchukua hatua zozote za kijeshi zaidi ya kulaani hatua hizo za miaka iliyopita ktk nchi za Georgia na Ukraine.
Putin orders Russian troops into Ukraine separatist regions | DW News
Russian President Vladimir Putin has signed a decree to send what he is describing as "peacekeeping troops" into the separatist regions of Luhansk and Donetsk. The decision comes after Putin recognized both regions as independent states and described Ukraine as ancient Russian territory. The move could mark a significant escalation amid fears Russia could soon launch a full-scale invasion of Ukraine.
Source : DW News
Mbona kelele nyingi hayo majimbo yanajulikana ni ngome ya Russia mbona hawakuchukua na Kiev yenyewe?