Mnachihanguuu
JF-Expert Member
- Feb 10, 2023
- 4,385
- 6,443
Hapana mimi sio mwalimu ila ndivyo nilivyo ukikosea tu kunitumia kuanzia buku hata ufanye nini sikurudishii humu ndani musijifanye watakatifu wengi wenu mumewakopa tala na hamukulipa hadi leo je hiyo nayo sio dhulma? Hivi mimi na viongozi wa serikali wanaofisadi pesa ya umma tuna tofauti gani? Mimi na mzinifu tuna tofauti gani? Mimi na anaecheza kamari tuna tofauti gani? Mimi na ninyi munaokesha bar tunatofauti gani? Acheni unafikiWaalimu jamani shida snaaaa...yani kakodi boda kwendaa kutoa helaa isiyokuwa yakeee
Hapo ndo maana huwa nasema kuwa Namba zetu zapaswa kuwa kama TINmwezi wa 4 mwaka huu nilituma 650,000 kimakosa-nimekuja kukumbuka dakika 5 zimekwisha jamaa amisha toa hela.dah niliumia sana
aiseee pole sanaamwezi wa 4 mwaka huu nilituma 650,000 kimakosa-nimekuja kukumbuka dakika 5 zimekwisha jamaa amisha toa hela.dah niliumia sana
Pole mkuu,chakufanya hiiyo hela uliyoplan kumpatia nunua zawadi ya mtoto kama tayari amepata mtoto kama bado nunua hata kitenge mpelekee.Mimi kuna mtu nilimuahidi kumchangia Harusi halafu sikumchangia... kiukweli roho iliniuma Sana kila ninapo kutana nae...
Kama ningejua ningemchangia tu...
Imeniumiza kuliko hela ambayo ningemchangia
Karma is realKama kichwa cha habari kinavyojieleza. Rafiki yangu alitumiwa pesa kimakosa kwenye no. yake ya mpesa inayoishia na 8650. Baada ya kutumiwa hiyo hela huyo rafiki yangu aliitoa yote.
Alipigiwa na aliyekosea mwamala akamrudishia elf 50 Kwa ahadi ya kulipa kilichobaki ila aliposhindwa aliacha kutumia hiyo no yake inayoishia na 8650.
Kama unaijua story hii jamaa anakutafuta aombe msamaha na kukulipa ukikubaliana maana anasema jambo hili linamtesa sana.
NB: Jamaa alikua anamtumia pesa wife wake. Ataje kiasi na mkoa aliotoka maana ni vitu anavikumbuka. Asanteni.
Wamevunja uaminifuMimi pia naapa kwa jina la mwenyezi Mungu ipo siku kuna watu 3 watanitafuta kuniomba msamaha kwa mambo walionifanyia.
Wewe bwege niniILAA KUNA WATU MNA ROHOO ZA WANYAMAA..HAMSTAHILI KUISHI!
So sad mkuu inaumizaHaya mambo ya hela za mtandao mimi huwa nayaheshimu sana,hujui hiyo hela aliyetuma huko alikokusudia kutuma ilikuwa ikafanye kazi gani?je mgonjwa yupo mahututi?msiba au ada?
Mwaka 2003 kipindi hiko hakuna pesa za kwenye simu jamaa yangu mama yake alikuwa na historia ya maradhi ya mara kwa mara na ya ghafla so yeye ndiyo mkubwa akawa yupo town anatafuta maisha ndugu zake wapo Arusha,alikuwa mlinzi muajiriwa wa wanaokumbuka kampuni ya GOHA SECURITY hawa walikuwa Magomeni Mapipa,siku moja ikapigwa simu nipo nae ilikuwa jioni ya 16:00 mama ameumwa tena na inatakiwa haraka hela kwa ajili ya dawa na huduma nyinginezo.
Jamaa alikuwa na akiba yake Tsh 50,000/= so ikabidi anunue voucher za Voda kisha nduguze kule kijijini wa-make deal na muuza vocha na mpigisha simu wa kijiji vocha itumwe kwake awe anaiuza kwa kurusha then akate itakayomtosha baki wapewe wakamuhudumie mama yao,jamaa akakosea namba moja mtu yupo Kigoma aloo ilikuwa balaa.
To cut a long story jamaa alikataa kurudisha hela (zile vocha) huku ndugu wa jamaa wanapiga simu mama anakufa hospital wamekataa kumuhudumia ikabidi apige tena simu Kigoma kwa jamaa huku analia kama mtoto akimuomba arudishe japo kidogo maana hela ilikuwa ni kwa ajili ya matibabu ndiyo kidogo jamaa akawa na huruma akarudisha japo sikumbuki kama alirudisha hata 40K,hii ilituumiza hata sisi tuliokua nae kwa ile hali jamaa alikuwa anapitia na toka siku ile nilijifunza mengi sana hasa kuheshimu hisia za watu nisiowaona.
So kwa yeyote atakaesoma hapa ajue anaweza akawa sababu za kifo cha mtu tujifunze kutokula visivyotuhusu.(nimekazia sana kwenye suala la kifo kwa sababu ndiyo sehemu pekee isiyokuwa na option ya subira)
Hii kitu sijui source ni niniUaminifu ni kitu muhimu sana kwenye maisha, wazungu wanaita "honesty"tatizo Ngozi nyeusi wengi wamekosa kitu hicho kutokana na malezi.
Huwezi jua mazingira ya mtumaji .Unaweza tuma hela ukiwa safarini au stendi unaendelea na safar Sasa wakala utampataje?Mbona kama Chai, yaani Wakala akosee afu aanze sumbuka kukupigia?
Wakala akikosea anawahi kuwapigia wenye mtandao hela inazuiwa.
Kama wakala katuma wewe hiyo namba iliyokosewa utaipataje?Huwezi jua mazingira ya mtumaji .Unaweza tuma hela ukiwa safarini au stendi unaendelea na safar Sasa wakala utampataje?
Kwamba wewe una mkeMwambie abaki nayo, si alijifanya mjanja kula hela yangu πππ