Rafiki yangu alimrusha mtu mwaka 2017/2018: Anamtafuta amwombe msamaha na kumlipa akikubali

Rafiki yangu alimrusha mtu mwaka 2017/2018: Anamtafuta amwombe msamaha na kumlipa akikubali

Kuna day moja nipo safarini natoka chuga nazama naenda singida kidogo naona Ela imeingia kwa ndamba ya mtu binafsi baada ya apo sms ya matumizi ikafata sindo nikamsanua kuwa umerong number alihisi kuchanganyikiwa sema nilimwambia asipige simu kuomba irudishwe nitamrudishia mwenyewe tu
Nice
 
Kuna kipindi wakati natafuta kazi nilikuwa choka mbaya..siku nikaitwa kwenye interview..sikuwa hata na jero.

Aisee naona 50K inaingia kwenye simu. Mara mhusika ananipigia kuwa kakosea. Nikamuambia nitamrudishia nikaitoa nikaenda fanya usaili.

Baada ya wiki tatu nikawa nimeajiriwa. Nikalipwa pesa ya kuhamishwa. Nikailipa ile pesa. Jamaa hakuamini. Nikamuambia ile pesa alikosea kwa kusudio la Mungu.
 
Sadaka yako ilikua ya kweli.

Sadaka zinapaswa ziwe zinatolewa kwa watu wenye uhitaji kama huyo, na sio sehwmu zisizo sahihi ambapo kuwafikia walengwa huwa ni tatizo.
Aseee sadaka ya kweli Mungu anakupa zaidi na zaidi,iliwahi nitokea mara mbili

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Kuna jamaa niliwahi kumtumia hela ya Michango ya msiba kimakosa,jamaa baada ya kuzungumza akaniambia anaishi Manzese Dar es salaam na akasema atanirejeshea.

Kuepusha lawama msibani wasidhani pesa nimetumia ikabidi nikope niitume halafu mimi nibaki kupambania deni,yule jamaa hela hakuirudisha na nikawa nampigia simu ananiambia nisimsumbue,aiseee ile haikuwa kubwa sana lakini nilisema lazima nimshikishe jamaa adabu.

Unajua kuna watu huwa hawajali pesa wanayopoteza,tatizo huwa linakuja kwa wapokea pesa,huwa wanakera na kuudhi sana hata kama hujafikiria kufanya jambo baya inakubidi ufanye jambo ili heshima iwepo.

Yule jamaa mwanzo nilimwambia asiponirudishia hiyo hela kwenye akaunti yangu atajuta kuzaliwa akadhani utani,safari hii sikutaka kutumia nguvu za Kikurya,nilipanga nitumie nguvu za wenye uwezo mbadala.

Kufupisha,Jamaa alikuwa ananitafuta baada ya kumkarabati analia nikamwambia sina muda yeye aendelee kula matanuzi!.

Aiseee baada ya kubembelezwa sana ndugu zake na hii ni baada ya miezi 7 ndipo tukaonana pale Rombo Green View wakanirudishia hela yangu nikachafua zangu,ingawa walidai wanilipe fidia mimi nikakataa nikawaambia sihitaji dhuruma nahitaji pesa nilikosea kutuma!.

Jamaa hata kaa anisahau hadi anaingia kaburini na hiyo pia itakuwa imempa funzo!.


MIMI SEHEMU YA NGUVU HUWA NATUMIA NGUVU ILA SEHEMU YA WAJUBA HUWA NAWAACHA WAJUBA WAFANYE KAZI YAO!.
Ulimkarabati kama kisauti alivyomkarabati Analyse 😂😂
 
Mungu anisamehe sana inawezakana ndo mana ridhiki zangu haziji

Watu walishawahi kosea kwangu =
150,000
95,000
80,000
Hizi 50,000 na zaidi ya mara 4

Sikuwahi kurudisha hata mia nliishia kuwablock

daah kuna mtu nakumbuka nilkosea kutuma hela kwakwe sh 52,000 ilikuwa namtumia mchepuko, nikapiga huduma kwa wateja kwasababu ile no ilikuwa Mtandao tofaut na mm.

niliambiwa nisubili masaa 72, ilikuwa jmos basi nikampigia yule jamaa nikamwambia nikosea kutuma hela kwakwe aniludishie walau 30,000 tuh, jamaa kweli akarudisha 30,000 nikamshukuru.

Nimekaa j3 sina mpango wowote naona messag ya muhamala unaiangia kwenye simu yangu hela imerudishwa, walah sikulemba nikaihamisha ile hela jamaa alipiga mara 3 sikupokea ila hakupiga tena
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Rafiki yangu alitumiwa pesa kimakosa kwenye no. yake ya mpesa inayoishia na 8650. Baada ya kutumiwa hiyo hela huyo rafiki yangu aliitoa yote. Alipigiwa na aliyekosea mwamala akamrudishia elf 50 Kwa ahadi ya kulipa kilichobaki ila aliposhindwa aliacha kutumia hiyo no yake inayoishia na 8650. Kama unaijua story hii jamaa anakutafuta aombe msamaha na kukulipa ukikubaliana maana anasema jambo hili linamtesa sana.

N.b. Jamaa alikua anamtumia pesa wife wake. Ataje kiasi na mkoa aliotoka maana ni vitu anavikumbuka. Asanteni.
Mm nilitumiwa pesa tar.7/07/2023 nikajua ataomba muamala urudishwe Kumbe hakurudisha , Jana nikakumbuka nikampigia Simu kapokea nikamielekeza akasema Kweli nilikosea ila mm mwenye hapa nilipo nipo taaban ninaumwa kwahiyo nilishindwa hata kuirudisha hiyo pesa.Kwa nilivyokuwa naongea nae nikweli anaonekana yupo hoi,basi nimemrudishia ameshukuru kweli.

Niwaombe mtu akituma pesa kimakosa irejeshe

Sent from my Infinix X6511E using JamiiForums mobile app
 
Mm nilitumiwa pesa tar.7/07/2023 nikajua ataomba muamala urudishwe Kumbe hakurudisha , Jana nikakumbuka nikampigia Simu kapokea nikamielekeza akasema Kweli nilikosea ila mm mwenye hapa nilipo nipo taaban ninaumwa kwahiyo nilishindwa hata kuirudisha hiyo pesa.Kwa nilivyokuwa naongea nae nikweli anaonekana yupo hoi,basi nimemrudishia ameshukuru kweli.

Niwaombe mtu akituma pesa kimakosa irejeshe

Sent from my Infinix X6511E using JamiiForums mobile app
07/07/2023??????
 
Back
Top Bottom