Rafiki yangu alimrusha mtu mwaka 2017/2018: Anamtafuta amwombe msamaha na kumlipa akikubali

Rafiki yangu alimrusha mtu mwaka 2017/2018: Anamtafuta amwombe msamaha na kumlipa akikubali

Haya mambo ya hela za mtandao mimi huwa nayaheshimu sana, hujui aliyetuma huko alikokusudia kutuma ilikuwa ikafanye kazi gani?je mgonjwa yupo mahututi?msiba au ada?

Mwaka 2003 kipindi hiko hakuna pesa za kwenye simu jamaa yangu mama yake alikuwa na historia ya maradhi ya mara kwa mara na ya ghafla so yeye ndiyo mkubwa akawa yupo town anatafuta ndugu zake wapo Arusha,alikuwa mlinzi muajiriwa wa wanaokumbuka kampuni ya GOHA SECURITY hawa walikuwa Magomeni Mapipa,siku moja ikapigwa simu nipo nae ilikuwa jioni ya 16:00 mama ameumwa tena na inatakiwa haraka hela kwa ajili ya dawa na huduma nyinginezo.

Jamaa alikuwa na akiba yake Tsh 50,000/= so ikabidi anunue voucher za Voda kisha nduguze kule kijijini wa-make deal na muuza vocha na mpigisha simu wa kijiji vocha itumwe kwake awe anaiuza kwa kurusha then akate itakayomtosha baki wapewe wakamuhudumie mama yao,jamaa akakosea namba moja mtu yupo Kigoma aloo ilikuwa balaa.

To cut a long story jamaa alikataa kurudisha hela huku ndugu wa jamaa wanapiga mama anakufa hospital wamekataa kumuhudumia ikabidi apige tena simu Kigoma kwa jamaa huku analia kama mtoto akimuomba arudishe japo kidogo maana hela ilikuwa ni kwa ajili ya matibabu ndiyo kidogo jamaa akawa na huruma akarudisha japo sikumbuki kama alirudisha hata 40K,hii ilituumiza hata sisi kwa ile hali jamaa alikuwa anapitia.

So kwa yeyote atakaesoma hapa ajue anaweza akawa sababu za kifo cha mtu tujifunze kutokula visivyotuhusu.(nimekazia sana kwenye suala la kifo kwa sababu ndiyo sehemu pekee isiyokuwa na option ya subira)
Mimi nakumbuka wakati nipo chuo 2010s nilituma pesa kimakosa, ile pesa nilikuwa namtumia mwenye uhitaji tena kwa haraka.

Nilikosea namba, aliyepokea pesa alikuwa Mbeya aisee nilivurugwa sio poa. Wazo likanijia nimpigie nikiri yule jamaa ni miongoni mwa watu waungwana alirudisha ile pesa instantily.

Kuna watu wana utu nakumbuka sikujielezea sana jamaa akasema nakurudishia kaka.. jamaa uliyenirudishia ile pesa popote ulipo una maua yako na Mungu azidi kukubariki [emoji120]
 
Kuna siku saa kumi na moja asubh nasikia simu inaita nkapokea nko na usngz namba ngen inaniulza mshaanza safar nkamjbu apana nkakata cm nkaendelea kulala kumbe aliendelea kupga akatuma na hela 350000 ma msg za kutosha kua tupitie jeneza tuje nalo, naamka sa mbil ndio naona msg na miscal za kutosha kupga ipe simu haipatikan nikaanza kuumiza kichwa huu msba wa wap nije na jeneza wap inafka sa sita simu inapgwa tena jamaa anaongea kilugha kwa ukali hatar nkamwambia mm skuelew unasema nn ndio akaanza kuongea kiswahil kua wanasubr jeneza mazish ni saa nane mchana nkamwambia itakua mmekosea namba mm nko mkoa flan jamaa akanza kuomba nimrudishie iko kias kwa haraka kabisa nkasema sawa nakutumia nkaMrushia kias chao japo ilkua imekatwa mpawa 18000 nkaenda kuiongezea kwa wakala.. usile kisicho kua cha haki yako wazee
 
2020 nilikosea kumtumia mtu 206,000. Ilikuwa ni malipo ya hela ya Chakula ya vibarua kwenye site yangu.

Nilikuwa busy kidogo, ilipofika tu jamaa niliyempigiaa simu akapiga. Nikamuandikia ujumbe kuwa tayari nimeshatuma. Niliamini ni fundi anauliza. Jamaa, akaniandikia pokea mara moja.

Akapiga lakini niligundua si sauti ya fundi. Akaniambia kuna fedha nimemtumia ila anaomba asirudishe. Nilipanick kidogo, jamaa akanielezea story ya magumu anayopitia. Anaomba sana nimuachie kiasi kile cha hela. Akaniambia kama sitaridhia atarudisha kiasi hicho punde baada ya kukata simu.

Lakini kwa magumu yale, niliridhia kumuachia kiasi hicho cha pesa. Ukweli ni kuwa niliokoa maisha ya mwanae. Na maombi yake yalijibiwa kupitia mimi. Nilifanya alternative nyingine kuwesesha kule site.

Jioni nilipata dili zuri mno. Nikajua tu ni Mungu ananilipa kwa Sadaka yangu ya asubuhi.
Mungu mkubwa,miujiza hii,but Mungu ndiye anaejua.[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Kuna siku saa kumi na moja asubh nasikia simu inaita nkapokea nko na usngz namba ngen inaniulza mshaanza safar nkamjbu apana nkakata cm nkaendelea kulala kumbe aliendelea kupga akatuma na hela 350000 ma msg za kutosha kua tupitie jeneza tuje nalo, naamka sa mbil ndio naona msg na miscal za kutosha kupga ipe simu haipatikan nikaanza kuumiza kichwa huu msba wa wap nije na jeneza wap inafka sa sita simu inapgwa tena jamaa anaongea kilugha kwa ukali hatar nkamwambia mm skuelew unasema nn ndio akaanza kuongea kiswahil kua wanasubr jeneza mazish ni saa nane mchana nkamwambia itakua mmekosea namba mm nko mkoa flan jamaa akanza kuomba nimrudishie iko kias kwa haraka kabisa nkasema sawa nakutumia nkaMrushia kias chao japo ilkua imekatwa mpawa 18000 nkaenda kuiongezea kwa wakala.. usile kisicho kua cha haki yako wazee
Nazani bila kusema jeneza au msiba isingeludi hiyo Hela [emoji1]
 
iliwahi kunitokea hiyo mwaka 2011 meseji imeingia kucheki laki 7 imeingia na ukifikiria sikuwa na kitu mfukoni aisee nilikodi bodaboda kwenda kijiji cha jirani kuitoa pesa njiani akawa ananipigia nikamwambia nipo barabarani nikifika nakurudishia hela yako ondoa shaka nilipofika kwa wakala nikaichomoa yote
 
Mungu anisamehe sana inawezakana ndo mana ridhiki zangu haziji

Watu walishawahi kosea kwangu =
150,000
95,000
80,000
Hizi 50,000 na zaidi ya mara 4

Sikuwahi kurudisha hata mia nliishia kuwablock

daah kuna mtu nakumbuka nilkosea kutuma hela kwakwe sh 52,000 ilikuwa namtumia mchepuko, nikapiga huduma kwa wateja kwasababu ile no ilikuwa Mtandao tofaut na mm.

niliambiwa nisubili masaa 72, ilikuwa jmos basi nikampigia yule jamaa nikamwambia nikosea kutuma hela kwakwe aniludishie walau 30,000 tuh, jamaa kweli akarudisha 30,000 nikamshukuru.

Nimekaa j3 sina mpango wowote naona messag ya muhamala unaiangia kwenye simu yangu hela imerudishwa, walah sikulemba nikaihamisha ile hela jamaa alipiga mara 3 sikupokea ila hakupiga tena
Mungu anakupima imani yako,

Wewe hauna huruma,


Omba msamaha,jutia
 
iliwahi kunitokea hiyo mwaka 2011 meseji imeingia kucheki laki 7 imeingia na ukifikiria sikuwa na kitu mfukoni aisee nilikodi bodaboda kwenda kijiji cha jirani kuitoa pesa njiani akawa ananipigia nikamwambia nipo barabarani nikifika nakurudishia hela yako ondoa shaka nilipofika kwa wakala nikaichomoa yote
Mtaua watu kwa presha.
 
Back
Top Bottom