Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Mleta mada anao ujumbe uliojificha, nimeutambua ndio maana maoni yangu yapo hivyo kama ulivyoyasoma.
 

Asante kwa maoni yenye kuongozwa na ubinadamu 🙏🏿.
 
Kilema[emoji3582]
Mlemavu[emoji3581]
 

Nyerere aliongoza shughuli nyingi tu za waislam.

Mkapa akahakikisha wanakuwa na chuo pale Morogoro.

Magufuli akichangisha sadaka maalum tayari inakuwa nongwa!.
 
Nimesoma hadi mwisho sijaruka kipengele chochote, japo sikujua kinachoendelea lakini umeelezea vizuri nikapata mwanga,

Binafsi nakazia kwa msumari yote uliyoyaandika, Dini isichanganywe na Siasa.
Rais angeitisha harambee msikitini kisha angalia rafiki zake waislam na wasio waislam nakutumia platform ya waislam(jukwaa la waislam) hapo angekuwa sahihi
 
Sasa John, imagine wakiristo waombwe kanisani kujenga nyumba ya ibada ya "wapagani", huoni kuwa hilo nalo pia ni kuwakwaza wakiristo?
Yesu alitutaka tumuahidi kwamba arudipo mara ya pili aikute amani duniani, ujenzi wa nyumba za ibada ni sehemu ya kuitengeneza amani!
 
Msikiti upi hapa nchini ulijengwa kwa michango ya wakiristo ukiachilia mbali huu ambao Magufuli anataka kiki za kisiasa?
Yani mingi sana mimi binafsi nimechangia, kuna msikiti Muhimbili, Kijitonyama Masjid Kuba, Mwananyamala kwa mama Zakaria, Mwenge kijijini huo nilichangia pesa ya harambee.

Bukoba mjini hamgembe huu sijui kama ulijengwa tayari, maana eneo walilotaka kujenga lilikuwa na migogoro.

Kuna ki msikiti Bunju B kule Mbatia aliuza viwanja nilichangia.

Hahaha ukiwa unaswali hiyo misikiti kumbuka nami niliichangia.
 

Waislamu wao wenyewe hawajashindwa kujenga msikiti huko Ikulu ya Chamwino.
Haihitajiki harambee za kanisani kujenga msikiti wa waislamu!. Yeye atoe tu eneo kisha awaachie waislamu wenyewe wafanye mchakato wa ujenzi, wskitaka kumshirikisha watamshirikisha

Mbona wakati anajenga kanisa hilo hakuomba harambee za waislamu?

Au anataka baadae, Waislamu wasimangwe kuwa hata huo msikiti wenu ndani ya Ikulu yetu ya dodoma ulijengwa kwa sadaka za Wakiristo?
 

Harambee ya kuchangia ujenzi wa msikiti mliifanyia kanisa gani na ilisimamiwa na padri au baba askofu gani?
 
Amabao hatuna mungu wala uchawi tutaishi vibaya sana hii nchi
 
Wenye dini yao wala hawana tatizo na hilo suala la michango. Nchi yetu sote hii na wala sio mara ya kwanza kuchangiana ujenzi wa makanisa na misikiti. Tatizo kila jambo linachanganywa na siasa.

Ni juzi tu Joketi Mwogelo Mkuu wa Wilaya Kisarawe amechagua ujenzi wa Msikiti na Waislamu wenyewe wamechagua kuwa mlezi wa kamati ya ujenzi.
 
Harambee ya kuchangia ujenzi wa msikiti mliifanyia kanisa gani na ilisimamiwa na padri au baba askogu gani?
Hahaha wewe unatafuta vita sasa, mwisho utaomba na cheque number ya mchango wangu.

Nimekwambia mimi nimechangia hiyo misikiti niliyokutajia.

Punguza jazba sito dai pesa yangu, nilitoa mchango kujenga nyumba ya ibada.

Nakumbuka msikiti wa mwenge kijijini tulichangia hadi zulia, waislamu wakampiga sheikh wa ule msikiti kwamba kala pesa iliyotoka uarabuni, tafrani lile hadi FFU walikuja kutuliza ghasia.

Hahaha huwa naguswa tu nachangia mkuu, usije susa kuswali bure.
 
majuzi TAG, sasa RC, bado bakwata na KKKT yote ni kuomba kura.
Lissu akienda utasikia kelele zitakavyopigwa na ccm na waliowaalika watasakamwa kwelikweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…