Rais Magufuli: Nitaheshimu ukomo wa miaka 10 ya Urais kulingana na Katiba ya Tanzania

Rais Magufuli: Nitaheshimu ukomo wa miaka 10 ya Urais kulingana na Katiba ya Tanzania

Toka Uhuru tulikuwa na uongozi wa Nyerere, watu hawakuhoji juu ya miaka yake ya kukaa madarakani.

Inawezekana hatukuwa tunajua Nini maana ya uongozi bora kwakuwa hatukuwa na jerea.

Ilipokuja awamu ya Mwinyi watu wakaanza kuulinganisha na uongozi wa Nyerere,wakaanza kutoa kasoro.
Hali hiyo imeendelea mpk awamu hii.
Watu kaanza kuyaona hata makosa ya Nyerere kwa kulinganisha na awamu zilizofuata.

Tofauti ya awamu hii na zingine ni moja tu,WATU
KUHOJI SUALA LA KUMUONGEZEA MAGUFULI MIAKA YA KUTAWALA.
Jambo hili mpaka awamu ya Kikwete halikuwepo.
Hii inaonesha awamu hii haikubaliki kabisa na watanzani85%
Ila inakubalika na wachache wanaomzunguka mkuu, Kama kina Butiku, makamba Yusuf na ccm wachache wanaomega mkate pamoja na mkuu.

Hivyo ccm, msiwalazimishe watanzani kubadiri Katiba yao kwa kubadiri ukomo kwaajili ya magufuli.

Ccm mtambue kuwa watanzania wanazidi kuelimika, wanazidi kupata ujasiri, ipo siku mtatusababishia vurugu na umwagaji wa damu.

Watanzani watadai haki yao ya kikatiba Kama kwa mkoloni wa ndani.

Sasa tumetambua kuwa kumbe mbunge wa chemba mlimtuma kuchokoza mada ili kupima upepo.
ACHENI JAMBO HILI HARAKA
Hawalazamishi wala hawana uwezo wa kulazimisha. Ongea na Diwani wako, na Mbunge wako, waambie kuwa hutaki aongezwe muda. Hayo ni maoni yako, wewe mpiga kura mmoja, Diwani naye atakusanya mwoni ya wapiga kura wote.

Na mbunge hivyo hivyo, watakwambia maoni ya walio wengi. Ukiona wengi wanataka aongezwe, nenda kwa tundulissu, ema kule aliko EU, au kupitia kwa Mnyika Ufipa Street Kinondoni.

Watakupongeza, watakupokea kwa mikono miwili. Sasa tuvumiliane hadi 2025 Uchaguzi Mkuu wapambanishe Ilani. Mkishinda, mmeshinda, hatoongezwa. Lakini mkishindwa tafuta shoka uanze kukata tamaa ukisubiri 2030,
 
Mkuu wetu wa nchi hii nchi unayoiongoza ina wananchi takribani mil 60. Kati ya hao ni 5% ni wanasiasa. Lakini wengi wao amaboa ni 95% ni wakulima na wafanyakazi.

Wewe unayo mamlaka ya kupata maoni ya nini 95% ya raia wa Tanzania wanatoa maoni juu ya uongozi wako.

Ukweli usiopingika wafanyabiashara wengi hawataki uongezewe muda hata sekunde moja. Maana tangu umeingia madarakani umekuwa mwiba kwao. Biashara zimefungwa sababu ya kutaka walipe kodi hata kama mazingira ya kibiashara sio rafiki. Kila sekta ya kibiashara imeganda.

Wakulima wapo kimya wanaugulia moyoni. Maana tangu uingie madarakani hali yao kuuza mazao imekuwa mbaya.Mazao ya nafaka mengi yamekosa soko hasa la nje ambalo ndio chanzo kikubwa cha mapato yao.

Wafanyakazi wa umma ndio wanakilio kikubwa. Wao wanaomba Mungu ustaafu hata kabla hujamaliza muda wako. Maana hujaongeza mshahara kwa miaka mitano tangu uingie madarakani. Hali ya maisha ni ngumu kwao maana maisha ni ghali.

Je kwa mazingira kama haya nani ambae ni mwananchi wa kawaida atataka uongezewe muda wa kutawala?

Hao wanasiasa wanaokupaka mafuta kwa mgongo wa chupa ambao ni 5% ya watanzania? Wewe ni mkuu wa nchi. Fanya utafiti juu ya hili. Wananchi wa kawaida wanaomba Mungu miaka minne iishe haraka aje rais mwingine mwenye huruma ili maisha yaendelee. Usidanganywe na akina Jah pipo wa Njombe.
Kwani katiba inasemaje jamani? Nahao wanao shadadia kuongeza Muda hawajuwi wana vunja katiba na wanaweza kushitakiwa? Last kwani hawaja msikia akisema hataki kuongeza hata siku moja?
 
Tanzania hii ni kubwa, ina watu wa kila aina...kwa kuwa hiyo kura unayoisemea itahusisha wananchi wote na siyo kikundi kidogo cha watu,unaweza shangaa anaibuka na uungwaji mkono wa 100 kwa 100..usikute hata wewe ukamuunga mkono
 
Tanzania hii ni kubwa,ina watu wa kila aina...kwa kuwa hiyo kura unayoisemea itahusisha wananchi wote na siyo kikundi kidogo cha watu,unaweza shangaa anaibuka na uungwaji mkono wa 100 kwa 100..usikute hata wewe ukamuunga mkono
Hata kwa mtutu wa bunduki,siwezi kuunga mkono wazo hili.
 
Screenshot_20210127-021703.png
 
Magufuli katu hataongezewa hata siku moja, yeye mwenyewe analitambua hilo na ameshalikubali.

Kwasasa atajaribu kufanya yote anayoyatamani ndani ya muda uliobaki.

Na karata ya mwisho ni kujaribu kumwachia nchi mrithi anayeamini ataendeleza pale alipoishia.
 
Kwani Magufuli huwa anategemea kura halali?Zitachakachuliwa kama kawaida kwa manufaa ya matumbo ya wachache!
Kabisa, nimeshangaa hata salary slip anapendekeza njia ya kura! Linapokuja suala la njia ya kura, ni wazi Magufuli atapata 100% na hakuna kura hata moja itaharibika, maana huwa hategemei kura, bali huagiza kuwa anataka kura kiasi gani.
 
Maghufuli ameona miradi yake ya kukurupuka haitaisha na mda unayoyoma , na ameliingizia hasara Taifa, anataka ajiongezee mda , Ila kama Mungu angekuwa anasikia huyu jamaa hatakiwi kabisa kujiongezea mda , miaka yake 10 ya mateso imetosha aiseee..... Mungu si utusikie Tu hili ombi jamani , huyu mtu arudi Tu kwao......Hili Taifa linahtaji huruma za Mwenyezi Mungu kuliko wakat wwte
 
Toka Uhuru tulikuwa na uongozi wa Nyerere, watu hawakuhoji juu ya miaka yake ya kukaa madarakani.

Inawezekana hatukuwa tunajua Nini maana ya uongozi bora kwakuwa hatukuwa na jerea.

Ilipokuja awamu ya Mwinyi watu wakaanza kuulinganisha na uongozi wa Nyerere,wakaanza kutoa kasoro.
Hali hiyo imeendelea mpk awamu hii.
Watu kaanza kuyaona hata makosa ya Nyerere kwa kulinganisha na awamu zilizofuata.

Tofauti ya awamu hii na zingine ni moja tu,WATU
KUHOJI SUALA LA KUMUONGEZEA MAGUFULI MIAKA YA KUTAWALA.
Jambo hili mpaka awamu ya Kikwete halikuwepo.
Hii inaonesha awamu hii haikubaliki kabisa na watanzani85%
Ila inakubalika na wachache wanaomzunguka mkuu, Kama kina Butiku, makamba Yusuf na ccm wachache wanaomega mkate pamoja na mkuu.

Hivyo ccm, msiwalazimishe watanzani kubadiri Katiba yao kwa kubadiri ukomo kwaajili ya magufuli.

Ccm mtambue kuwa watanzania wanazidi kuelimika, wanazidi kupata ujasiri, ipo siku mtatusababishia vurugu na umwagaji wa damu.

Watanzani watadai haki yao ya kikatiba Kama kwa mkoloni wa ndani.

Sasa tumetambua kuwa kumbe mbunge wa chemba mlimtuma kuchokoza mada ili kupima upepo.
ACHENI JAMBO HILI HARAKA
Hapo mtoe butiku na makamba
 
View attachment 1696487

Rais Magufuli akiwa Korogwe Tanga amesema hayuko tayari kuendelea kuongoza baada ya miaka 10 iliyowekwa kikatiba. Ameyasema haya baada ya Mbunge wa Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani (Prof. Maji Marefu) kusema Rais anastahili kuongezwa muda ilia afanye mambo mengi zaidi.

Hii kauli imemaliza wasiwasi wa watu wote waliokuwa na speculation kuwa Rais anaweza kuongeza muda wa kukaa madarakani.
Hata m7 alisema hivyo
 
anasema uwongo ndio wanasemaga ivyo ivyo anataka aonekane alilazimishwa ila yeye hakupenda waongo sana hawa msidanganyike na maneno yake
 
HABARI: Rais John Magufuli amesema hawezi kukaa kwenye urais miaka 20 kama alivyoombwa na Mbunge, Steven Ngonyani kwa kuwa ni kinyume na katiba.

Mh Rais anahutubia muda huu hapa Korogwe Stand,Tanga.

mbona magufuli na ccm wanavunja sana katiba ? anasemaje atalinda kitu anayoivunja ??
 
Ukweli ni kwamba, hizi kelele za baadhi ya watu kutaka Magufuli aongezewe muda, ni kelele tu za watu wachache ambao ama wanafaidika na huu utawala, au wanatumika na huu utawala kuendesha hiyo kampeni na si vinginevyo.

Ni imani yangu, watanzania wengi wanatamani muda wake uishe aondoke apishe wengine kuanzia wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima, wafugaji, watu walioko katika sekta ya madini, vijana wanaotafuta ajira, n.k kiasi kwamba hata kura ya maoni ikipigwa leo hii kuhusu swala hili la kumuongezea Magufuli muda wa kukaa madarakani, hawezi pata uungwaji mkono hata wa asilimia 30 ya kura zote zitazopigwa.

Hata baadhi ya aliowapa vyeo nao wanaweza kupiga kura ya kukataa jambo hilo kwani hata wao hawana uhakika wa nafasi zao huku wako ambao na wao wanatamani hiyo- nafasi ya uraisi.

Siamini kabisa kama watu wanafurahia namna Magufuli anavyoendesha hii nchi wakiwemo wana-CCM wenyewe kwani ni wazi kauli za Magufuli na vitendo vyake haviwapendezi wengi na mfano mzuri ni kauli ya hivi karibuni kuhusu madakatri walioacha kazi serikalini na ile ya kuhusu kutoa chakula cha msaada wakati wa njaa kwa wananchi kauli hizi zikiwa ni muendelezo wa kauli zake zenye ukakasi tangu aingie madarakani mwaka 2015.

Ukiacha maswala kama ya kutoongeza wafanyakazi mishahara, wafanyabiashara kubambikiziwa kodi kubwa, mazao ya wakulima kukosa soko,kuminya uhuru wa maoni, kukandamiz demokrasia,vitendo vya utekaji, n.k ,jambo lingine linalommaliza vibaya kisiasa ni ili la kuutangazia umma kuwa hakuna Covid na kuonekana ni kosa kusema mtu fulani kafa kwa corona katika nchi hii wakati mitaani hali inaonekana kuwa ni tofauti.

Jambo lingine linalomuweka pabaya kisiasa ni tuhuma za kutumia fedha za umna kuendeleza sehemu anayotoka (Chato), jambo linaloonekana kuwakera watanzania wengi na hivyo kujiuliza iwapo ataongezewa muda hiyo Chato itakuwaje ukilinganisha na maeneo mengine ya nchi na maswali mengine mengi.

Kwa kifupi, kulingana na mtazamo wangu na ambao naamini ni mtazamo wa watu wengi pia, Magufuli amefeli sana katika swala zima la uongozi na alichoweza ni kuendeleza tu sekta ya ujenzi na miundombinu mambo ambayo hayawezi kumfanya aonekane anastahili kuongezewa muda kwani mahitaji ya watanzania ni zaidi ya miundombinu.

Hivyo, kutokana na sababu hizo na zingine ambazo sikuzitaja(amabazo unaweza kuzitaja), Magufuli hawezi pata uungwaji mkono hata wa asilimia 30 litapokuja swala la kura ya maoni juu ya kumuongezea au kutumuongezea muda wa kukaa madarakani.
Magufuli hawezi kupata hata 5% kama kuna uchaguzi wa huru na haki.... say uchaguzi usimamiwe na EU kila ngazi, hatoboi
 
Maghufuli ameona miradi yake ya kukurupuka haitaisha na mda unayoyoma , na ameliingizia hasara Taifa, anataka ajiongezee mda , Ila kama Mungu angekuwa anasikia huyu jamaa hatakiwi kabisa kujiongezea mda , miaka yake 10 ya mateso imetosha aiseee..... Mungu si utusikie Tu hili ombi jamani , huyu mtu arudi Tu kwao......Hili Taifa linahtaji huruma za Mwenyezi Mungu kuliko wakat wwte

Na hata wapambe wake wanajiuliza wataficha wapi nyuso zao pindi hasara aliyoingiza nchi hii itakapoanza kuwekwa wazi. Hivyo wanataka aendelee kukaa madarakani ili ukweli usifahamike.
 
Hayo maneno atakuja kuyajutia tu siku za usoni wakati tamaa ya kuendelea kutawala itakapo endelea kumuwakia moyoni mwake.
 
Back
Top Bottom