Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Ila bana, tuache utani, hizo sime kwa karne hii waachane nazo tu,
Kesho kutwa mm nikiwa natembe na AK47 mtaniruhusu kwa kuwa sipigi nayo mtu?
Kama ni utamaduni wenu fanya tu
 
Yeriko Nyerere give us a break
Fimbo na sime za kina Ole Ngurumwa zinahatarisha Muungano?🤧
Hivyo Wamarekan/Watanzania wasizuiwe kutembea na AR-15 machine guns barabarani
Maasai sio watu exceptional zaidi ya WaTz wengine
Sheria ikigusa masai watu wanalalamika balaa,
Wanapinga masai kuhamishwa ila watu kibao hii nchi wamehamishwa na watu wapo kimya,
 
Zanzibar mibaguzi sana,, nimefurahi Kwa kichapo walichopewa wajukuu chotara wa mwarabu
 
Utamaduni wa hovyo tu
 
Serikali ya mapinduzi inapotoshwa kwa hili la wamasai. Kuna chuki kubwa za kidini dhidi ya jamii Za watanganyika
Ila kwa ajili ya siasa watakanusha , wafute tangazo lao kimyakimya dhidi ya wamasai.
Mangi.. SI Kila kitu chuki ya dini nyingine ni taratibu na Sheria zinazolinda usalama wa raia
 
Utamaduni wa Wamasai kutembea na Visu na virungu ni wanapokuwa Kwao ambako kiasili ni Mbugani so wanapigana na Wanyama na wadudu wengine hatari

Sasa kwenye nchi iliyostaarabika kama Zanzibar unatembeaje na Rungu na Sime mitaani kwa wala urojo?

Wamasai waache uporipori🐼
 
Kweli watu wanabadilika! Huyu si ndiyo 'YERICKO NYERERE' aliyekuwa anaonekana kama 'Great thinker' kwa makala zake mbalimmbali zenye akili hapa JF? Mimi nadhani kuna mtu atakuwa anatumia ID yake.
Sikutarajia makala ya namna hii yaandikwe na mtu kama YERICKO NYERERE mtu ambaye wakati fukani alionekana kama 'Great thinker hapa JF! Yaani wamasai kukatazwa kutembea na fimbo na masime baada ya kufanya 'tukio la kihalifu' iwe sababu ya kuhatarisha muungano? Hivi nyinyi watu mnauelewa muungano vizuri lakini?

Kama hamuelewi waulizeni Wazanzibari, 'walipambana kwa jasho na damu' na wameshindwa!

Wamasai lazima wafuate sheria ili waendelee na shughuli zao za kimaisha, mimi naamini, hata ukiona mmasai yupo Zanzibar, ujuwe huku Tanganyika alisha kosa hiyo fursa na hata akirudi wewe huna kazi ya kumpatia

Jengine ni kwamba hata nyinyi mnaoshabikia 'upuuzi' na kujifanya kuwa na huruma na wamasai ni waongo tu, sisi tunaoishi na wamasai kwa karibu huku tunayaona mateso yao!
 
Watanganyika tuna upole uliochanganya mpaka kufikia kilele cha ukilaza.

mfano:kwa ilo tukio la masai na polisi wa Zanzibar raia wa tz wangekua ndio raia wa South,Nigeria n,k wazanzibari wangechezea kichapo huku bara mpaka huo muungano ungejuta.
 
Huo upumbavu ni wewe unao sio wao dunia yote kuna jamii flan flan utazikuta hazibadiliki na kutaka kulazimisha unakuwa wewe ndio mjinga. Kenya watu wapokot Turkana na Maasai ni the same uganda wapo Namibia wapo Botswana wapo marekan wapo Scotland wapo Australia wapo nk. Hiz jamii kwanza ndizo wa
Ila bana, tuache utani, hizo sime kwa karne hii waachane nazo tu,
Kesho kutwa mm nikiwa natembe na AK47 mtaniruhusu kwa kuwa sipigi nayo mtu?
Karne gan aisee. Hiv ukimuona mwarabu kavaa kanzu unamuona ni mjinga flan sio. Au ukienda Yemen wanavyovyaa yale majambia unahc vichaa sio.
 
Ngoja nikuache akili zako ni za kijinga, hao pokot kwa kufanywa special saivi wanamiliki siraha za moto hadi wanapambana na Jeshi.

Endeleeni kuwaza kijingajinga majibu ya huu upumbavu mtayaona
 
Unajaribu kuwafokea wazenji,we kama Nani kwamfano.
Ile ni Serikali kamiri.
Tena usirudie ujinga wako huo.
Ukitaka kumjua kama wewe sio mmoja wao,nenda na hela zako ukanunue eneo tuone kama utauziwa.

Msiwapangie Cha kufanya.

Nyie kama hamna Serikali kaeni kimya.
Mzanzibari ana haki bara,kumpata au kufanya chochote,Sasa nnajizima DATA kuwa nyie sio Watanganyika😄.
By the way,CCM mbele Kwa mbele.
 
Jamani sime,rungu na fimbo sio silaha. Sime kwa ajili ya kukata nyama,fimbo na rungu ni kwa ajili ya ulinzi(self defence)
 
Wale wanavaa majoho
 
Wewe Yeriko Nyerere, hata ukiwa Rais na ukanda serikali lazima utaipinga tu serikali yako uliyoiunda. Kama Lisu, hata akiunda serikali ataipinga tu serikali.
Fimbo za nini mjini? Kule tarime wakurya walikuwa wanatembea na sime, rungu na mapanga yakawa yanahatarisha amani. Serikali ikaona hapana. Ikakataza. Leo hii Tarime wakurya wamezoea hawatembei na silaha hizo.
Hao wamasai wasiambiwe kitu kisa wamasai. Wanyamganywe tu maana hakuna sheria inaruhusu watu kutembea na silaha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…