Rais Samia aagiza kushushwa tozo kwenye bidhaa za mafuta

Rais Samia aagiza kushushwa tozo kwenye bidhaa za mafuta

Tanzania mafuta yakipanda leo Duniani, bei inapanda siku hiyohiyo ila mafuta yakishuka bei huko Duniani Tanzania tutaambiwa kuna shehena ya zamani ilinunuliwa kwa bei ya zamani.

Unajiuliza mbona kwenye kupanda hatuambiwi kuna shehena ya zamani tusubiri iishe?

Magenge ya wauza mafuta wameweka pale mawakala wao huko ewura, tunaokamuliwa ni sisi choka mbaya.
Na mbaya zaidi viongozi ndio wafanya biashara hiyo
 
Chief Hangaya unatengeneza matatizo halafu unajifanya kuyatatua. Hizo zilikuwa siasa chafu za Magufuli achana nazo.
Acha ujinga wewe kuna tozo 23 lakini tozo 1 tuu ndio Rais aliiweka.

Sasa tozo zimerekebishwa lakini sijaridhishwa na huo mchakato kwa sababu haujashusha bei bali umeongeza bei kwa sh.12 zaidi.

Japo mh.Rais kasema kama kuna mambo yanahitaji marekebisho ya sheria basi wapeleke mswaada wa sheria Bunge lijalo kufuta kabisa baadhi ya tozo ambaO ziliwekwa kwa sheria ya Bunge.
 
Hujaelewa kuna tozo karibia 10 za ajabu ajabu kwenye kila lita moja ya mafuta inayoingia nchini,kitu ambacho kinasababisha mafuta hayo hayo kutoka bandarini kwetu Dar yakifika Zambia wao bado bei kwa lita ni chini ya 1800. Kuna tozo sijui EWURA, Bandarini, TRA, wakala wa vipimo, TBS na zingine kibao!! Hapa ilitakiwa zingine siyo kupunguza bali zifutwe kabisa na tungenunua petrol kwa 1500 kabisa hapa.
Ziko 23 na Rais kawaambia wapeleke mswaada Bungeni wafute hayo matozo mewngi ya kijinga.
 
A great move if seriously and positively implemented.
Similar initiatives should be taken towards investments and moves aiming at reducing and curbing the Costs of Electricity.
Hiyo move itakuwa na tija endapo agizo la Rais la kupeleka mswada Bungeni kufuta matozo yaliyopo kisheria ila kwa sasa tozo ambazo zilipachikwa tuu zimeishia kuongeza bei kwa sh.12 kwa Lita badala ya sh.145 .
 
Hiyo move itakuwa na tija endapo agizo la Rais la kupeleka mswada Bungeni kufuta matozo yaliyopo kisheria ila kwa sasa tozo ambazo zilipachikwa tuu zimeishia kuongeza bei kwa sh.12 kwa Lita badala ya sh.145 .
.... if seriously (all inclusive) implemented.......
 
Hivi kwa nini tunang'ang'ana na mafuta wakati tuna gesi ya kufa mtu? au yote kapewa mchina.......maana bongolala ni kichwa cha mwendawazimu.
 
Unafiki tu. July tu wameongeza viwango vya kodi kwenye mafuta.....wafute na hizo pia!
 
.... if seriously (all inclusive) implemented.......
Unfortunately nimefanya kupitia tozo zote kumbe zilianzishwa na sheria ya Bunge..Hiyo sheria iligawanya tozo zinazoweza kurekebishwa na waziri inapobidi na tozo ambazo hazibadilishwi zinabaki kama zilivyo..

Matokeo yake ndio haya sasa wamerekebisha viwango lakini hawawezi kuzifuta,way fowadi ni lazima zirudishwe Bungeni zikafutwe .

Nikajiuliza kwani Katiba yetu haimpi Rais executive orders ya kufuta hizo sheria kama tulivyoona kwa Trump hadi kusubiria mchakato wa Bunge?

Tusubirie unafuu pindi Bunge likikaa na kufuta tozo ambazo serikali itataka zifutwe..

Ushauri wafute matozo yote ya kijinga lakini wafanye adjustment kwenye tozo inayoenda Tarura,sh.100 haitoshi angalau iwe 150 ..
 
Unafiki tu. July tu wameongeza viwango vya kodi kwenye mafuta.....wafute na hizo pia!
Hizo haziwezi kufutwa maana hakuna tozo imefutwa bali viwango vya kutoza ndio vimerekebishwa..

Tozo zilipitishwa na Bunge lazima zirudi Bungeni.
 
Mama kaamua kupambana na mafia kwenye mafuta. Kagusa sekta yenyewe ambayo ni nyeti.

Namtakia kila lenye kheri na nguvu za Mungu ziwe juu yake. Nahisi kama anajitengenezea mazingira mabaya ya usalama wa uhai wake.
 
Hujaelewa kuna tozo karibia 10 za ajabu ajabu kwenye kila lita moja ya mafuta inayoingia nchini,kitu ambacho kinasababisha mafuta hayo hayo kutoka bandarini kwetu Dar yakifika Zambia wao bado bei kwa lita ni chini ya 1800. Kuna tozo sijui EWURA, Bandarini, TRA, wakala wa vipimo, TBS na zingine kibao!! Hapa ilitakiwa zingine siyo kupunguza bali zifutwe kabisa na tungenunua petrol kwa 1500 kabisa hapa.
Kwani hizo tozo ziliwekwa na ACT wazalendo au CCM?![emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom