Rais Samia aagiza Vyombo vya Uchunguzi kumpa taarifa ya kina ya Kifo cha Ali Mohamed Kibao

Rais Samia aagiza Vyombo vya Uchunguzi kumpa taarifa ya kina ya Kifo cha Ali Mohamed Kibao


Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Bwana Mohamed Ali Kibao. Natoa pole kwa viongozi wa chama hicho, familia ya Mzee Kibao, ndugu, jamaa na marafiki.

Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana Haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii.

Pia Soma:
Bila kuja na plan mbadala ya njia ya ukamataji wa kihalali na uwazi ni bure
 
Ninaamini kauli hii ya Rais Samia ni ya dhati. Ukweli ni kwamba ndugu yetu Ally ametekwa na kuuawa na kile kinachojiita kikosi kazi/task force. Ndani yake wamo polisi, TISS na JWTZ. Sasa vyombo alivyoviagiza Rais vifanye uchunguzi, ni chombo gani nje ya hawa wahusika wakuu?

Hiki kikosi cha kiharamia kisipovunjwa na kupotezwa, kadiri kinavyozidi kunogewa na damu za watu, kuna siku kinaweza kuwageukia hata wao wenyewe au wapendwa wao.

Hawa wauaji, Rais Samia amewalea mwenyewe. Watu wanatekwa na kuuawa, yeye anasema kuwa eti ni drama!! Halafu akaongeza kwa kusema kuwa eti anawapongeza nchi imekuwa shwari. Baada ya hizo pongezi, wakaongeza uovu.
ni muhimu sana,
ikiwa yupo raia anazo taarifa sahihi na za kuaminika za uhalifu wa tukio hili na mengineyo kushirikiana na vyombo vya uchunguzi kubainisha na kudhitisha ukweli wa mambo kwenye matukio haya ili hatua husika zichukuliwe dhidi ya wahusika na haki itendeke kwa waathirika...🐒
 
Na wewe umemwamini kwamba polisi watafanya uchunguzi wa haki?
Ukute alieratibu utekaji ndie anae manage hiyo twitter account.

Kauli yeyote inayotolewa ni kufunika kombe mwanaharamu apite. Hii yote ni well orchestrated mission yenye kila baraka ya wateuzi na wateuliwa.

Mungu awape machungu ya kuondokewa na wakwao kama wanavyoondoshea wenzao.
 

Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Bwana Mohamed Ali Kibao. Natoa pole kwa viongozi wa chama hicho, familia ya Mzee Kibao, ndugu, jamaa na marafiki.

Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana Haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii.

Pia Soma:
Mama kasema....

Tuungane naye katika kuyaendea hayo.....

#Nchi Kwanza[emoji7]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
“Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya mauaji ya kiongozi wa CHADEMA, Bwana Mohamed Ali Kibao. Natoa pole kwa viongozi wa chama hicho, familia ya Mzee Kibao, ndugu, jamaa na marafiki.

Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii.” – Rais Samia Suluhu


View: https://x.com/swahilitimes/status/1832806858639233511?t=Q7dxv-guM5xKq_icgxWsGg&s=19
 
Ingekuwa Nchi zinazojitambua hadi Sasa IGP alitakiwa awe amejiuzulu au ameongea na umma kuujulisha hatua Gani amechukua.rais kafanya la maana lakini uchunguzi unafanywa na haohao watekaji na watatoa majibu ambaye wao hayatawahusisha.Hapo inatakiwa iundwe tume ambayo haihusishi vyombo vya ulinzi kama vile wanasheria,asasi za kiraia za haki kama TLHR,madaktari n.k
 
Kwa hili Mama Samia achutame aone aibu, haiingii akilini kwamba yeye kama amri jeshi mkuu akose taarifa ya kikosi kazi kinachopoteza wananchi wake kwa unyama wa hali ya juu kama huu uliompata mzee Ali.

Nilitegemea kuona akitengua wakuu wa vyombo vya ulinzi hasa IGP na DG maana hao wanafahamu fika kile kinachoendelea katika utekaji huu haramu.

Na kama kweli hajui kuwa kuna watu wanatekwa na kupotezwa huwenda akawa anafichwa mengi sana na wakuu wake wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Inasikitisha sana
 

Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Bwana Mohamed Ali Kibao. Natoa pole kwa viongozi wa chama hicho, familia ya Mzee Kibao, ndugu, jamaa na marafiki.

Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana Haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii.

Pia Soma:
Drama Queen by Sueco
 
Back
Top Bottom