balimar
JF-Expert Member
- Sep 18, 2015
- 7,743
- 13,657
Aiseh yaan bora nikae kimyaHii nchi nzuri sana.
Unaiba halafu unalipwa.
Hongereni kwa kulipa wezi.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Aiseh yaan bora nikae kimyaHii nchi nzuri sana.
Unaiba halafu unalipwa.
Hongereni kwa kulipa wezi.
Tena na ribaWalipweeeeeee
Ni sahihi sababu walitumika kujenga Taifa.Akili zao zilitumika na sio vyeti vyaoNi Mei Mosi ambpo Samia ametoa maagizo haya kuwa walioondolewa kwa vyeti feki enzi za Magufuli walipwe stahiki zao kama mafao ya kustaafu
Je ni sahihi kuwalipa hasa ikizingatiwa walitenda uhalifu kuingia kazini?
Mbona mwenyewe na makonda walitumia vyeti feki kupata ajira serikaliniKwa Haki vipi na cheti FEKI?
Kwani michango yao kwenye mifuko ya jamii ipo wapiHizo pesa zipo au ni mashairi ya jukwaani tu
Adhabu ipi? Wakifunguliwa mashtaka pia mtakuja kusema wanaonewa? Adhabu ipi inawafaa?Nafahamu mazingira yaliyopelekea hivi vyeti feki kuwa vingi namna hii maana wengine tumekuwa tukishuhidia utendaji wao na kuziona kazi zao kwa miaka mingi.
Hawa watu wengi walifoji vyeti waliajiriwa kihalali kabisa ila baada ya kufanya kazi muda mrefu na serikali kutaka wajiendeleze walikubali ila kurudi shule wakakuta si sawa na uzoefu walio nao huku makazini, kama unavyojua elimu yetu ni kukariri formular, magazijuto n.k wakashindwa na wakashawishika kutumia shortcut. HILI LILIKUWA KOSA na lilistahili adhabu ila si ya kiwango cha kuwanyima hata hizo 5% walizokatwa.
Wengine walifeli masomoni kabla ya ajira, wakanunua cheti(HILI LILIKUWA KOSA) halafu wakasoma kihalali mpaka degree na kuendelea, wakaajiriwa. Wanastahili adhabu lakini si ya kiwango cha kuwanyima hata hizo 5% walizokatwa.
Cheti Ni tatizo, Lakini dogo! Suala la msingi wamefanya kazi zinazostahili malipo na hatimaye mafao, ambayo kimsingi yamekatwa kwenye mapato yao?! Kwani Ni cheti, kiwe original Au fake, kilicho fanya kazi?Ni Mei Mosi ambpo Samia ametoa maagizo haya kuwa walioondolewa kwa vyeti feki enzi za Magufuli walipwe stahiki zao kama mafao ya kustaafu
Je ni sahihi kuwalipa hasa ikizingatiwa walitenda uhalifu kuingia kazini?
Kama ni feki kosa la nani wao au muajiriWalitumikia kwa haki wakati walighushi vyeti?
Mbona mafisadi hayafungwiMajizi yanalipwa!!
Kiboo ya ndesii!!!
Mmerithi uSadist kutoka kwa mungu wenu mfu wa chatoHii nchi nzuri sana.
Unaiba halafu unalipwa.
Hongereni kwa kulipa wezi.
Majizi yanalipwa!!
Kiboo ya ndesii!!!
Ni cheti kilichofanya kazi na kikatwa hayo mafao?Kwa Haki vipi na cheti FEKI?
Jiweke upande wao, vyaa viatu vyao..u will feel it.We utakuwa vyetu feki wewe! [emoji23]
Sio kwamba alikuwa na huruma, ni kwamba alihitaji kupunguza wafanyakazi bila gharama kubwa na akatumia makosa ya hao watumishi kutimiza takwa lake hilo.Mamá Samia hakupaswa kabisa sio tu kulitamka bali hata kulifikiria hili swala
Maana hawa wa vyeti feki wana hatia ya kuidanganya Serikali na kupatiwa mishahara isivyo halali
Jpm alikuwa na huruma ila kiutaratibu walitakiwa kufunguliwa mashtaka ya kufoji na kujipatia pesa isivyo halali
Hao unaowaita majizi wengine walikuhudumia wewe kima ww.Siwezi kuvaa viatu vya majizi ya kitaaluma.
Mimi nimesoma nimeenda shule bwana. Siwezi kuwa sambamba na majizi ya vyeti.
Tumeelewana? Au niongeze sauti ya redio?
Cheti ndo kinaendesha gari,fundisha darasani,safisha vidondaUtakuwaje na ujuzi bila shule? [emoji23]