Rais Samia aingilie kati tatizo la wazee kuwaoa mabinti wadogo; aagize sheria ya ndoa kurekebishwa

Rais Samia aingilie kati tatizo la wazee kuwaoa mabinti wadogo; aagize sheria ya ndoa kurekebishwa

Jambo wakuu!

Sitaki kuwachosha, naingia kwenye mada moja kwa moja. Kumekuwa na wimbi baya la wazee kuwaoa mabinti wadogo ambao ni sawa na watoto au wajukuu zao na kibaya zaidi, baadhi ya wazee hao waliwahi kulitumikia taifa kwa nyadhifa kubwa. Tofauti na matarajio ya wengi kuwa wazee hawa walipaswa kuonyesha mfano bora kwa watanzania, badala yake wamegeuka kuwa kero kwa kugeuza uharibifu wa mabinti kuwa jambo la umaarufu. Halafu wamekuwa siku zote wakitamba kabla na baada ya kufanya vitendo hivyo wakidhani kuwa wanafanya jambo zuri. Inasikitisha sana.

Baadhi ya viongozi wakubwa wa kitaifa ambao wamejitumbukiza kwenye mchezo huu mchafu wa kuwaoa mabinti wadogo ni Profesa Kapuya, Pius Ngwandu, Abrahamu Mengi na sasa mzee Augustine Lyatonga Mrema ametangaza kufunga ndoa hivi karibuni na binti mbichi kabisa anayelingana na wajukuu zake. Namuomba Mh mama Samia uingilie kati jambo hili kwa kuagiza Wizara ya Sheria kuifanyia mabadiliko sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ili kuwasnusuru mabinti wasiolewe na wazee vikongwe. Sheria iweke tofauti ya umri wa watu wanaofaa kuoana; ikiwa tofauti ya umri itakuwa kubwa (kwa mfano miaka kuanzia 20 na kuandelea) basi ndoa hiyo ichukuliwe kuwa ni batili na mhusika (mume) atakayekuwa ametenda kosa hilo achukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kupigwa faini, kufungwa jela au vyote kwa pamoja. Watanzania wanapaswa kuiga mfano bora wa Pius Msekwa na John Malecela waliowaoa watu wazima wanaolingana nao kiumri.

Mama Samia umefanya jambo jema kuwaruhusu mabinti waliozaa kurejea shule kutimiza ndoto zao za kielimu. Hapa umeupiga mwingi mama yangu mpendwa. Adhma yako ya kutoa elimu kwa mabinti haiwezi kutimia ikiwa mabinti hao unaowapigania kurudi shule kupata elimu watakwapuliwa na wazee wenye uchu wa ngono. Nakuomba pia ushughulikie tatizo hili la mabinti wadogo kuolewa na baba au babu zao ili kuwakoa mabinti wanaoingia kwenye mtego huu wa fisi wapenda ngono.

Watu wanaweza kuchukulia jambo hili kuwa dogo lakini ukiliangalia kwa jicho la latu, hili ni tatizo kubwa sana linaweza kuathiri maadili ya kitaifa na ukosefu wa uzalendo na utii wa sheria. Ikiwa wazee wataendelea na tabia yao hii ya kuwaoa mabinti wadogo kuna uwezekano vijana wadogo wakiume nao wakaanza kuwaoa wanawake watu wazima ili kulipiza kisasi. Ndio. Ipo siku vijana watakosa mabinti wa kuwaoa na kuwageukia vikongwe. Endapo nchi itafikia hatua hii, maadili ya kitaifa yatamomonyoka kwa kiasi kikubwa. Kuliko kusubiri ukuta uanguke tujenge mpya, nakuomba mama Samia uingilie kati suala hili kabla hali haijwa mbaya sana.

Nawasilisha.​
Mama Samia hatoweza fanya lolote kwa sababu tatizo hili linaendekezwa sana na waze wa Kiislam. Mtu ana mshipa eti anakwenda kuoa katoto ili kawe kanachezea mshipa wake usiku.
 
Siku wakitaka kuoa watamuoa nani wakati wazee watakuwa wameishaoa wote? Acha roho mbaya mkuu.
𝐍𝐚𝐨𝐧𝐚 𝐰𝐚𝐭𝐮 𝐰𝐞𝐧𝐠𝐢 𝐰𝐞𝐦𝐞𝐤𝐮𝐬𝐡𝐚𝐦𝐛𝐮𝐥𝐢𝐚 𝐤𝐰𝐚 𝐤�𝐮𝐰𝐚 𝐮𝐦𝐞𝐢𝐭𝐚𝐣𝐚 𝐝𝐡𝐚𝐦𝐛𝐢 𝐲𝐚 𝐬𝐨𝐝𝐨𝐦𝐚 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐲𝐨 𝐤𝐢𝐥𝐚 𝐦𝐭𝐮 𝐚𝐧𝐚𝐢𝐚𝐛𝐮𝐝𝐮, 𝐌𝐮𝐧𝐠𝐮 𝐚𝐭𝐮𝐬𝐚𝐦𝐞𝐡𝐞 𝐭𝐮 𝐦𝐚𝐚𝐧𝐚 𝐬𝐢 𝐬𝐚𝐰𝐚 𝐦𝐭𝐨𝐭𝐨 𝐤𝐮𝐮𝐨𝐧𝐚 𝐮𝐜𝐡𝐢 𝐰𝐚 𝐛𝐚𝐛𝐚 𝐲𝐚𝐤𝐞 𝐧𝐚 𝐭𝐞𝐧𝐚 𝐧𝐢 𝐥𝐚𝐚𝐧𝐚 𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐡𝐚𝐰𝐚𝐣𝐮𝐢 𝐭𝐮,
 
Binafsi naona ni vyema Wazee kuoa mabinti wadogo. Hawa mabinti ndo wanajua kuwatunza Wazee. Wanafahamu ni muda gani mzee anywe chai, chakula cha mchana na cha jioni. Wanafahamu fika kumfulia mzee nguo zake na hata kumchagulia nguo ya kuvaa siku husika. Wanasimamia usafi wa Wazee hasa pale nyumbani na mengine mengi.
 
Mkuu nimesema kwamba wengi wa vigoli hawa hurubuniwa na wazee pamoja na wazazi wao kwa sababu ya ufukara; wengi hawaolewi kwa kupenda bali kwa mashinikizo y wazaz/walezi wao. You get me right?
Hakuna kushinikizwa ikiwa wamefikia umri wa kuolewa, ina maana wanatambua wanachokifanya.........
 
Mkuu hapa hatuongelei imani ya mtu bali tunaongelea sheria ya ndoa ya Tanzania ya mwaka 1971. Tunaomba irekebishwe ili kuwazuia wazee wasiwaoe mabinti wanaolingana na watoto/wajukuu zao. Umenipata?
Mkuu, utawanyima watu haki zao wakati hawavunji sheria yoyote (kama binti ni above 18)
 
Raisi akimaliza hilo aingilie kati pia suala la single mother kuolewa na kijana ambae hajawahi kuwa na mtoto, sio haki kabisa kabla hata mechi kuanza ubao wa matokeo kusoma 1 - 0 huo ni uonevu na pia ni unyanyasaji mkubwa wa kijinsia.
 
Unaelewa maana ya two consenting adult
hao mabinti hawashikiwi shoka wala panga!?
Unafahamu maana ya kuheshimu kila kauli itokayo kwa mzazi? Na ikiwa utamkaidi mzazi anaweza kukufuramia au kukulaani.
 
Jambo wakuu!

Sitaki kuwachosha, naingia kwenye mada moja kwa moja. Kumekuwa na wimbi baya la wazee kuwaoa mabinti wadogo ambao ni sawa na watoto au wajukuu zao na kibaya zaidi, baadhi ya wazee hao waliwahi kulitumikia taifa kwa nyadhifa kubwa.

Tofauti na matarajio ya wengi kuwa wazee hawa walipaswa kuonyesha mfano bora kwa watanzania, badala yake wamegeuka kuwa kero kwa kugeuza uharibifu wa mabinti kuwa jambo la umaarufu. Halafu wamekuwa siku zote wakitamba kabla na baada ya kufanya vitendo hivyo wakidhani kuwa wanafanya jambo zuri. Inasikitisha sana.

Baadhi ya viongozi wakubwa wa kitaifa ambao wamejitumbukiza kwenye mchezo huu mchafu wa kuwaoa mabinti wadogo ni Profesa Kapuya, Pius Ngwandu, Abrahamu Mengi na sasa mzee Augustine Lyatonga Mrema ametangaza kufunga ndoa hivi karibuni na binti mbichi kabisa anayelingana na wajukuu zake. Namuomba Mh mama Samia uingilie kati jambo hili kwa kuagiza Wizara ya Sheria kuifanyia mabadiliko sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ili kuwasnusuru mabinti wasiolewe na wazee vikongwe.

Sheria iweke tofauti ya umri wa watu wanaofaa kuoana; ikiwa tofauti ya umri itakuwa kubwa (kwa mfano miaka kuanzia 20 na kuandelea) basi ndoa hiyo ichukuliwe kuwa ni batili na mhusika (mume) atakayekuwa ametenda kosa hilo achukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kupigwa faini, kufungwa jela au vyote kwa pamoja. Watanzania wanapaswa kuiga mfano bora wa Pius Msekwa na John Malecela waliowaoa watu wazima wanaolingana nao kiumri.

Mama Samia umefanya jambo jema kuwaruhusu mabinti waliozaa kurejea shule kutimiza ndoto zao za kielimu. Hapa umeupiga mwingi mama yangu mpendwa. Adhma yako ya kutoa elimu kwa mabinti haiwezi kutimia ikiwa mabinti hao unaowapigania kurudi shule kupata elimu watakwapuliwa na wazee wenye uchu wa ngono.

Nakuomba pia ushughulikie tatizo hili la mabinti wadogo kuolewa na baba au babu zao ili kuwakoa mabinti wanaoingia kwenye mtego huu wa fisi wapenda ngono.

Watu wanaweza kuchukulia jambo hili kuwa dogo lakini ukiliangalia kwa jicho la latu, hili ni tatizo kubwa sana linaweza kuathiri maadili ya kitaifa na ukosefu wa uzalendo na utii wa sheria. Ikiwa wazee wataendelea na tabia yao hii ya kuwaoa mabinti wadogo kuna uwezekano vijana wadogo wakiume nao wakaanza kuwaoa wanawake watu wazima ili kulipiza kisasi. Ndio.

Ipo siku vijana watakosa mabinti wa kuwaoa na kuwageukia vikongwe. Endapo nchi itafikia hatua hii, maadili ya kitaifa yatamomonyoka kwa kiasi kikubwa. Kuliko kusubiri ukuta uanguke tujenge mpya, nakuomba mama Samia uingilie kati suala hili kabla hali haijwa mbaya sana.

Nawasilisha.​
kuna mzee mmoja alinambia

"Umeona wapi gari bovu likasukumwa na gari bovu lenzake"

ukiutafakari vizuri huo msemo utajua kwanini wanafanya hivo
 
Hivi unajua muasisi wa Imani yake alioa binti wa umri gani?!!!

Huu uzi ulianzisha jana jioni, hadi muda huu Una views zaidi ya 1,200 na posts zaidi ya 90, lkn bado hakuna like hata moja!
Maana'ake wadau hawaafikiani na maoni yako!
Huu uzi ni mujarabu kwa kuwa hakuna dislike hata moja kuonyesha kuwa watu hawajanielewa.
 
kuna mzee mmoja alinambia

"Umeona wapi gari bovu likasukumwa na gari bovu lenzake"

ukiutafakari vizuri huo msemo utajua kwanini wanafanya hivo
Mkuu huwezi kutumia misemo ya mtaani kuhalalisha uhalifu/uovu.
 
𝐍𝐚𝐨𝐧𝐚 𝐰𝐚𝐭𝐮 𝐰𝐞𝐧𝐠𝐢 𝐰𝐞𝐦𝐞𝐤𝐮𝐬𝐡𝐚𝐦𝐛𝐮𝐥𝐢𝐚 𝐤𝐰𝐚 𝐤�𝐮𝐰𝐚 𝐮𝐦𝐞𝐢𝐭𝐚𝐣𝐚 𝐝𝐡𝐚𝐦𝐛𝐢 𝐲𝐚 𝐬𝐨𝐝𝐨𝐦𝐚 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐲𝐨 𝐤𝐢𝐥𝐚 𝐦𝐭𝐮 𝐚𝐧𝐚𝐢𝐚𝐛𝐮𝐝𝐮, 𝐌𝐮𝐧𝐠𝐮 𝐚𝐭𝐮𝐬𝐚𝐦𝐞𝐡𝐞 𝐭𝐮 𝐦𝐚𝐚𝐧𝐚 𝐬𝐢 𝐬𝐚𝐰𝐚 𝐦𝐭𝐨𝐭𝐨 𝐤𝐮𝐮𝐨𝐧𝐚 𝐮𝐜𝐡𝐢 𝐰𝐚 𝐛𝐚𝐛𝐚 𝐲𝐚𝐤𝐞 𝐧𝐚 𝐭𝐞𝐧𝐚 𝐧𝐢 𝐥𝐚𝐚𝐧𝐚 𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐡𝐚𝐰𝐚𝐣𝐮𝐢 𝐭𝐮,
Watu wengi hawajui laana iliyojificha kwenye kuona uchi wa mzazi wako. Na hii laana ndiyo inatutafuna watanzania hadi leo. Sijui tunakwama wapi. 😳 😳 😳
 
Back
Top Bottom