Rais Samia aiteka mijadala ya kisiasa mitaani, wananchi waupongeza uongozi wake

Rais Samia aiteka mijadala ya kisiasa mitaani, wananchi waupongeza uongozi wake

Endelea kumdanganya mwenzio.
IMG-20230104-WA0005.jpg
 
Nitakupigia nikupe mchongo uachane na kujitwisha zigo la madodoki.

BiTOZO atakufanya uonekane kituko as if hauna baba wala mama.
Mimi Ni mkulima ninayetumia Neema ya ya Taifa letu kubarikiwa kuwa na ardhi kubwa yenye rutuba na inayostawisha mazao ya aina mbalimbali
 
Huku kwetu mbolea ya Ruzuku IPO na inaendelea kupatikana kwa Bei elekezi na wakulima kila mmoja anakwenda kununua kwa wakati wake,na wale waliotaka kuleta janja janja wamekumbana na mkono wa serikali shupavu na madhubuti ya Rais samia
WanaJF hawajakuelewa kwa kuwa bandiko lako kuu ni KITENDAWILI
 
-Bidhaa bei juu.
-Kikokotoo cha TRA kuagiza mzigo hasara tupu kwa mfanyabiashara.
-Deni la taifa linapaa kwa kasi ya kimbunga
N.k
 
Kazi kubwa na za kipekee alizozifanya Rais wetu na ambazo zimeendelea kuonekana machoni pa watanzania zinajitangaza zenyewe na kuonekana kwa yeyote asiye jipa ukipofu
Najua hata wewe unajua ugumu unaoupata kwa kutoa hizi sifa.
Ni sawa na mwalimu kufundisha somo au mada ngumu anatumia nguvu nyingi, na anajua kabisa wanafunzi wake hawamuelewi.

Kwa vile ndio kazi yake, inambidi akomae tu.
Pambana ndg, maji ndio hayoo ushayavulia nguo sharti uoge! Ila hata wewe unajua ukweli kwa ground hali ni mbayaaa, hawampendi hata kidogo
 
Waambie wakubwa ukweli halisi huku kitaa:
  • Bei ya bidhaa/huduma ipo juu;
  • Biashara haziendi. Amina za watu kwenye vikoba zimeshikiliwa baada ya marejesho kugoma;
  • Watu wanakimbia nyumba kukwepa mikopo umiza hasa samani kuuzwa n.k.
N.B: Enyi wasifiaji wa kudumu wa JF msijiondoe ufahamu kwa haya maisha yasipokupiga wewe moja kwa moja yatakuoiga kupitia ukosefu wa ajira WA ndugu wa karibu. Jizime data, ila Ukirudi live utakula za USO.
 
Najua hata wewe unajua ugumu unaoupata kwa kutoa hizi sifa.
Ni sawa na mwalimu kufundisha somo au mada ngumu anatumia nguvu nyingi, na anajua kabisa wanafunzi wake hawamuelewi.

Kwa vile ndio kaxi yake, inambidi akimae tu.
Pambana ndg, maji ndio hayoo ushayavulia nguo sharti uoge! Ila hata wewe unajua ukweli kwa ground hali ni mbayaaa, hawampendi hata kidogo
Labda wewe ndio una chuki binafsi lakini mh Rais anakubalika na kupendwa Sana na watanzania, ukienda kwa wakulima Wanampongeza na kumshukuru Rais Samia kwa kuwapatia mbolea za Ruzuku, ukienda kwa wazazi wanamshukuru na kumpongeza mh Rais kwa kuwapunguzia mzigo wa mchango baada ya kukamilisha vyumba vya madarasa bila kuwasumbua kwa michango, ukienda kwa vijana wana matumaini ya kutimiza Ndoto zao za kielimu baada ya Elimu kuwa bure Hadi kidato Cha sita huku mikopo ya Elimu ya juu ikipatikana na kuwanufaisha wenye sifa, ukienda kwa wafanyabiashara Wana mpongeza mh Rais kwa kuwawekea mazingira mazuri ya kibiashara, ukienda kwa watumishi wa umma Wanampongeza mh Rais kwa kuwaboreshea mazingira ya kazi na maslahi yao, N.k
 
Waambie wakubwa ukweli halisi huku kitaa:
  • Bei ya bidhaa/huduma ipo juu;
  • Biashara haziendi. Amina za watu kwenye vikoba zimeshikiliwa baada ya marejesho kugoma;
  • Watu wanakimbia nyumba kukwepa mikopo umiza hasa samani kuuzwa n.k.
N.B: Enyi wasifiaji wa kudumu wa JF msijiondoe ufahamu kwa haya maisha yasipokupiga wewe moja kwa moja yatakuoiga kupitia ukosefu wa ajira WA ndugu wa karibu. Jizime data, ila Ukirudi live utakula za USO.
Vijana wameona namna mh Rais tangia alipoapishwa kuwa Rais namna alivyomwaga maelfu ya ajira mitaani katika secta zote,wameona na kunufaika na mikopo ya halmashauri, wanaendelea kunufaika na fursa za ajira kupitia secta binafsi ambayo kwa Sasa inaendelea kunawili na kuwa yenye Afya njema
 
Ndugu zangu watanzania,

Rais Samia Ameendelea Kuiteka mijadala ya kisiasa Mitaani,kila mahali Ni Rais Samia,Ni Rais Samia juu ya uchapa kazi wake ulio tukuka,Ni Rais Samia juu ya kuimarisha demokrasia,Ni Rais Samia juu ya kuendesha na kuongoza maridhiano,Ni Rais Samia juu ya kulituliza Taifa letu,Ni Rais samia juu ya kukuza uchumi wetu,Ni Rais samia juu ya kuimarisha mifumo ya haki na utawala Bora,Ni Rais Samia juu ya kuhubiri na kutenda haki,Ni Rais Samia juu ya Uzalendo wake kwa Taifa letu,Ni Rais Samia juu ya mapinduzi ya kilimo,Ni Rais Samia juu ya kuliheshimisha Taifa letu,Ni Rais Samia juu ya usikivu wake,Ni Rais Samia juu ya Ukarimu na Upendo wake,Ni Rais Samia juu ya mazingira Bora ya kibiashara na kiuwekezaji,

Ni Rais Samia juu ya ushupavu na umadhubuti wake,Ni Rais Samia juu ya ujasiri na misimamo yake,Ni Rais Samia juu ya Dira na muelekeo wake ulio Bora kwa Taifa letu,Ni Rais Samia juu ya miradi mikubwa ya kimkakati Ni Rais Samia juu ya utolewaji wa huduma Bora za kiafya na kielimu,Ni Rais Samia juu ya uchumi jumuishi na kugusa kila mtu,Ni Rais Samia juu Ya Tanzania iliyo Bora na yenye kutoa matumaini yaliyo hai.

Rais Samia Mama yetu mpendwa ameamsha mioyo ya Uzalendo kwa Taifa letu,Rais Samia anajadiliwa na kupongezwa kwa kulileta Taifa pamoja na kuliweka katika vifua vya watanzania wazalendo,Rais Samia anatetewa na kupiganiwa na watanzania wengi,kila eneo ana wasemaje wa kumsemea mambo aliyo yafanya na kuyatekeleza kwa hiyari kabisa bila malipo.

Watanzania wanaonesha kuridhishwa na utendaji kazi wa mh Rais wetu mpendwa mama Samia,wanaonesha kukubaliana na hatua mbalimbali anazozifanya katika kuimarisha na kuupa Afya uchumi wetu,wana mpongeza kwa namna alivyoongeza makusanyo ya mapato mpaka kufikia Trioni mbili kwa Mwezi pasipo mavurumai na uhasama na wafanyabiashara.

Kila mmoja Anayo amani katika biashara yake na shughuli yake ya kiuchumi,kila mmoja ana matumaini na kesho yake iliyo Bora.,hakuna Mwenye wasiwasi juu ya biashara yake kuvamiwa au kufirisiwa kiuonevu,Hakuna kutunishiana misuli,Ni majadiliano na kuelimishana,Hakuna kuviziana Wala visasi,hakuna kukomoana Wala kunyanyasana. Rais Samia Ni kiongozi aliyeinuliwa na kupewa baraka zote kwa ajili ya kulivusha Taifa letu kuelekea Kanaan nchi ya Ahadi yenye maziwa na Asali.

Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627
Mkuu unatafuta udc? Ameiteka mijadsla ipi labda, watu wanalia maisha magumu wewe unatuletea mapambio hapa. Umekula maharage ya wapi wewe
 
Mkuu unatafuta udc? Ameiteka mijadsla ipi labda, watu wanalia maisha magumu wewe unatuletea mapambio hapa. Umekula maharage ya wapi wewe
Nilimwambia mwashambwa Lucas alete CV yake hapa ili tujipime tunajadili na mtu WA Aina gani! Hilo alilikimbia

Mjadala mkubwa kuhusu Rais mitaani.

-Kupanda kwa gaharama za maisha kiasi watu kushindwa kumudu mfumuko mkubwa wa Bei.
-Uduni wa huduma za afya hebu tuzama tu yaliyotokea Huko uyui ni reflection ya maeneo mengi nchini
-Gharama za mafuta zilizopaisha kila Aina ya huduma!
-Matabaka katika elimu (state schools, community schools) na elimu duni isiyomsaidia Mwananchi kuweza kukabiliana na changamoto za maisha, elimu Bure ambayo ni Bure kwa kwa kuwa ni Bure!
-Kukua haraka na kuongezeka kwa matabaka ya walio nacho na wasiokua nacho! (Hasa wanasiasa na wafanyabishara) huku kundi la wakulima na wafanyakazi likiwa katika dimbwi la maskini.

-UKOSEFU WA AJIRA BADO NI TATIZO SUGU na nchi imekua ya wachuuzi (machinga badala ya wazalishaji)
  • Hakuna sectorial linkage Kati ya kilimo na viwanda Ili kuongeza wigo wa Ajira na mnyoro wa thamani
  • Umeme usiokuwa wa hakika kuanzia mijini mpaka vijijini
  • Huduma za maji sio za uhakika mmebakia kusifu mega projects Ila kufikia watumiaji ni Siku mradi unazinduliwa.

Mambo ni mengi tukiyataja hayaishi!

Juzi nimesikia huko morogoro upatikanaji wa mbolea ni kupitia usajili kwa mitandao ya simu! (Eneo husika linalalamikiwa kufikiwa na network, vipi kuhusu kupanda kwa gharama za mawasiliano? )
- Matumizi mabaya ya fedha za umma kama serikali inavyojitapa kutangaza watu walitumia vibaya fedha za umma hatuoni hatua zozote za kisheria zikichukuliwa dhidi ya wahusika Ila tunaona wakihamishwa vituo vya Kazi!

Mwashambwa uandishi WAKO ni kama hii nchi ni Canada au Nchi iliyoendelea kupita nchi yoyote duniani! Kila kitu Kiko okay wakati Kuna watu wanajifungulia majumbani na wanafunzi wanakaa nchini!
 
Kaka yangu, kuna teuzi za juzi hapa bado mabandiko hayajajibu? Naona unaendeleza, endelea kulima tu...
 
Basi nimefuta kauli. Kumbe mkulima nlifikiri naongea na mtu aliyeenda shule. Samahan mkuu
Kwani unafikiri mstaafu kikwete halimi,mh pinda halimi? Kweli wewe Ni mtumwa wa akili na mawazo na Elimu yako haijakukomboa zaidi ya kukuongezea mzigo kichwani,Nini alikwambia kilimo kinalimwa na wasio na Elimu pekee? Au kwako kilimo na mkulima unakichukuliaje? Ulikuwa unawazidi Nini akina mzindakaya waliokuwa wakulima? Umewahi kumsikia sumri? Kweli wewe akili yako Ni finyu sanaa
 
Back
Top Bottom