Rais Samia akataa kutukuzwa, asema yeye hawezi kujilinganisha na Mungu

Rais Samia akataa kutukuzwa, asema yeye hawezi kujilinganisha na Mungu

Mzee Mwinyi ndio alikua wa kwanza kukataa kuitwa mtukufu na huyu Mama wapo waliopenda kuitwa Mungu na watumishi wao na waliona sifa ila mbele za Mungu ni kosa kubwa sana katika Imani ila ukiwa huna iman yeyote ni sawa tuu...
 
Hata Petro alikataa kuwa siyo mfuasi wa Yesu lakini matendo yake tu yalionyesha, hatuoni anavyoshangiliwa akitoka Ulaya watu wanaacha kazi zao kama vile ametoka mbinguni na kutumia gharama kibao za walipa kodi
Kupokewa kwa shangwe hakumfanyi kuwa 'Mungu'. Ni mbinu tu ya kutetea Reputation ya kiti cha urais. Pia ionekane anaungwa mkono. Imagine anashuka kwenye ndege yupo yeye tu na wachache alioongozana nao. Watajitokeza watesi wake fasta sana na kusambaza uzushi kwamba 'SAMIA HAKUBALIKI-arejea nyumbani kiyatima yatima' wakiambatanisha na 'ushahidi' wa picha. Hahahaaaaa.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Aonyeshe kwa vitendo..kupiga marufuku mapokezi na usindikizaji usio na msingi..kupiga marufuku sherehe yake ya kuzaliwa kufanywa maulidi ya taifa...apige marufuku hawa uvccm wanaojipendekeza na tuvimisemeo vyao vya nyuki wa mama n.k.

#MaendeleoHayanaChama
Nyuki gani waovyo hivyo.hao ni chawa sio nyuki.nyuki hawezi kua mjinga.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kupokewa kwa shangwe hakumfanyi kuwa 'Mungu'. Ni mbinu tu ya kutetea Reputation ya kiti cha urais. Pia ionekane anaungwa mkono. Imagine anashuka kwenye ndege yupo yeye tu na wachache alioongozana nao. Watajitokeza watesi wake fasta sana na kusambaza uzushi kwamba 'SAMIA HAKUBALIKI-arejea nyumbani kiyatima yatima' wakiambatanisha na 'ushahidi' wa picha. Hahahaaaaa.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
Nonsense
 
Kupokewa kwa shangwe hakumfanyi kuwa 'Mungu'. Ni mbinu tu ya kutetea Reputation ya kiti cha urais. Pia ionekane anaungwa mkono. Imagine anashuka kwenye ndege yupo yeye tu na wachache alioongozana nao. Watajitokeza watesi wake fasta sana na kusambaza uzushi kwamba 'SAMIA HAKUBALIKI-arejea nyumbani kiyatima yatima' wakiambatanisha na 'ushahidi' wa picha. Hahahaaaaa.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
Kwahiyo hao watu wakisema samia hakubaliki ndio itamuondolea yeye kua rais?.Huu sio wakati wakupiga mapambio ni wakati wayeye na watu wake kuifanya kazi waliyomba kwa ajili ya watanzania.na tutakuja kumpima kwa jinsi alivyotekeleza majukumu yake kama rais nasio kwajinsi alivyokua anapokewa na lundo la watu.Hii nchi bado ina mambo mengi yakufanya kuliko kulundikana kumpokea rais.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kuwa sawa na wengine sio kujishusha, bali ndo usawa wenyewe.

Unaposema utajitahidi kujishusha maana yake upo juu ya wengine na sio rahisi kuwa sawa hadi ujitahidi, hii itoshe tu kusema amejibu hoja ya Askofu tu ila utekelezaji sio guarantee.
 
Kwahiyo hao watu wakisema samia hakubaliki ndio itamuondolea yeye kua rais?.Huu sio wakati wakupiga mapambio ni wakati wayeye na watu wake kuifanya kazi waliyomba kwa ajili ya watanzania.na tutakuja kumpima kwa jinsi alivyotekeleza majukumu yake kama rais nasio kwajinsi alivyokua anapokewa na lundo la watu.Hii nchi bado ina mambo mengi yakufanya kuliko kulundikana kumpokea rais.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Hayo maigizo yanasaidia sana kulingana na aina ya jamii tuliyo nayo. Si unaona hata 'hayati' alivyokuwa anaigiza mabarabarani kwamba yeye ana 'huruma' sana,kumbe.... Kuna watu wanaokotwa sana kwa hayo 'maigizo'. Wapo watu hadi leo wanaamini 'hayati' alikuwa na huruma sana na alikuwa rais wa wanyonge kweli. Politics is an Art.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Utu tuvituko sijui tutaisha lini,Rais wa tz ujifananishe na Mungu..sasa kina Putin wajifananishe na nani...mapanki sijui asemeje.Hata kuandika hivyo juu ya Mungu wetu umekosea sana.Mwachen arelax mbona tunafanya madhambi mengi ila kauchuna tu,sijui mnamchokonoa ili atufanyaje sijui🙄🙄
 
Kauli inayoonyesha kuwa rais wa JMT hana makuu na hawezi kuwa kiongozi wa kupenda makuu na kujiinua kama Mungu.
Rais Samia akataa tabia ya kutukuzwa.

===

View attachment 2127410
Picha: Rais Samia Hassan Suluhu

Rais Samia Suluhu Hassan amesema hana tabia ya kutukuzwa wala kulinganishwa na Mungu na kwamba atajitahidi kuwa na hekima na uvumilivu wa kusikiliza maoni ya wengine.

Rais Samia amesema hayo leo Jumanne Februari 22, 2022 katika sherehe za Jubilee ya miaka yake 25 inayofanyika wilayani Ngara mkoani Kagera.

Alikuwa akijibu kauli iliyotolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge-Ngara, Severine Niwemugizi aliyeemuomba Rais Samia kutokubali kulinganishwa na Mungu kwa namna yoyote ile.

“Baba Askofu katika kufunga hotuba yako umeniasa mambo ya kukataa kutukuzwa na mimi nataka nikuahidi mbele ya umma huu kwamba, hii si tabia yangu na ninajitahidi kujishusha niwe sawa na wengine. Maana utumishi huu kama mipango ya Mungu ilivyo ameniweka hapa niwatumikie na siyo nijitukuze kwenu kwahiyo nitawatumikia,” amesema Rais Samia.

Amesema atajitahidi kuwa na hekima na uvumilivu na niwe na sikiko la kusikiliza yale yanayosemwa na wengine.

PIA SOMA:
- Askofu Niwemugizi amuomba Rais Samia asikubali kufananishwa na Mungu
Lakini hata kupenda kuwekewa mabango ya picha zake mabarabarani na kwenye viwanja vya ndege ni aina ya kujiinua na kujitukuza. Hakuna Rais mwingine ukiacha JPM aliyefanya haya, na ndiyo waungwana na wasio na unafiki kama Baba Askofu Niwemugizi wameona bora wamkemee. Tulizoea mabango kama hayo wakati kampeni cha uchaguzi. Au iseme kwanza na timu zake wameanza kampeni mapema?
 
Naona raia na hasahasa viongozi bado hawajaelewa kauli ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan

1667903467729.png

Picha toka maktaba : Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wakati wa Dhifa ya Kitaifa aliyomuandalia mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Botswana Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi tarehe 10 Juni 2021 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 
ANAUPIGA MWINGI limekuja kwa bahati mbaya?
 
Back
Top Bottom