Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

Huyo Mama ana kiburi na dharau sana!
 
Ni kusikiliza kero za Wananchi kutoka Kwa mbunge wao na kuwasalimia
Kwa hiyo hapa alikuwa anaongea na Mbunge? Kwanini ana simama njiani si ana namba za mbunge si angempigia?

Wewe kichwa maji?
 

Attachments

  • IMG_0974.jpeg
    IMG_0974.jpeg
    54.6 KB · Views: 2
Ili iweje? Rais hawezi kusikiliza kero za mtu mmoja mmoja, na hata akisikiliza hawezi kufanya maamuzi hapo kwa hapo, maana inawezekana huyo mwananchi akawa anapotosha pia. Kama yule mama wa Tanga alivyompotosha Magufuli
Kwani akisikiliza alafu akaliacha kwa RC,kuna shida gani?
Moja ya sifa ya Kiongozi bora ni kusikiliza!
 
Kwanini asingetembea tuu hadi Nagwanda kuhutubia tuu au uwanja wa Ilulu kuhutubia? Kilichomsimamisha njiani ni nini?
Au kama anaona Tanzania ni kubwa arudi kwao Zanzibar akaongoze wachache. Au Tz igawanywe, kanda ya ziwa iwe taifa linalijitegemea. Kwa kifupi huyu ni rais wa matajiri. Maskini watasubiri sana.

Kwa mfano hapo angekuwa ni rostam au tajiri fulani ana hoja yake binafsi, angeacha kumsikiliza?
 
Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

Lost a chance to get it from the horse's mouth. What a waste?
 
Sasa kilichomfanya asimame njiani ni nini? Kwanini asingelikwenda moja kwa moja uwanjani?[emoji23][emoji23][emoji23]
Rais anaweza kusimama popote anapotaka
 
Sasa pale kasimama kufanya nini!?....kama anajua Mbunge yupo, why bother kusimama barabarani kusikiliza kero za wananchi?...mimi naamini kuna wananchi wameshazunguka ngazi za chini na hawapati msaada, Kiongozi wa nchi akisikiliza hizo special cases,anaweza kutoa msukumo mwananch asaidiwe.
Lakini pia malalamiko mengi kwenye eneo yanampa Rais picha pana juu ya uwezo wa viongozi aliowateua katika eneo husika.
 
Kwani akisikiliza alafu akaliacha kwa RC,kuna shida gani?
Moja ya sifa ya Kiongozi bora ni kusikiliza!
Maana ya kuwa na wasaaidizi au kuwa na viongozi wa serikali ni nini?

Wewe umewahi shuhudia wapi rais akisikiliza kero za mtu mmoja mmoja hapa duniani? At huyo wa marekani ushawai sika?
 
Ni kweli Rais hawezi kusikiliza kero za mwananchi mmoja mmoja, itakuwa jau sana .... mwingine kapigwa na mumewe anataka kesi apeleke kwa Rais, tutamaliza saa ngapi?
Tungejiuliza kwanza kwanini kuwe na wananchi wengi wanaotaka kumweleza rais shida zao wakati ngazi za chini kuna wateule wa rais chungu nzima! Hili ndilo tatizolinalotakiwa kutatuliwa. Wabunge kwa nini hawatimizi majukumu? Wakuu wa wilaya nk kwa nini hawatekelezi majukumu? Jibu ni kuwa hawajioni kama wanawajibika kwa raia. Wanajiona kuwa rais ndiyo bosi wao. Bila kubadisha mfumo ni bure.
 
Ule mtindo wa Magufuli ulikuwa ni upumbavu tu kwa wananchi wapumbavu. Hakukuwa na leadership pale. Hivi Rais mmoja utawezaje kumsikia kila mwananchi?

Endelea hivyo hivyo Samia na wala usiingie mtego wa kugawa hela barabarani
Sasa kwani na huyu anaendeleza huo unaoitwa upumbavu wa kusimama njiani? Alisimama kuongea na nani hapa kama sio hao wananchi ambao hataki kujibu maswali yao hata moja? Au wakuuliza maswali hakuandaliwa?
 

Attachments

  • IMG_0974.jpeg
    IMG_0974.jpeg
    54.6 KB · Views: 2
Hapana, Rais anatakiwa ashughulike na mambo ya kitaifa. Huyo raia unaweza kukuta analalamikia kesi ya mirathi ya familia yao au kucheleweshwa mshahara kazini kwake.
Sasa yeye Rais kasimama pale kwenye kadamnasi kufanya nini,si angepita speed na kuwapungia mkono!
 
Back
Top Bottom