Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Attachments

  • IMG_0974.jpeg
    IMG_0974.jpeg
    54.6 KB · Views: 1
Za uraisi, anaomba kwa wabunge wabunge wanaenda kumuombea kwa raia anakua hapati shida ya kukutana na raia wenye ziki na matatizo mengi yasiyoisha
Hata asipoomba kabisa hizo kura italeta tofauti gani,
Magufuli alifanya mikutano mingapi ya kampeni mwaka 2020 huko Kusini??
 
Ni hopeless person and can not share love and hope to people. Leaders are meant change things and offer immediate solutions to issues. Hopefully ako low sharpness kwenye brain
Alichosema Rais ni kweli,
Na kama ni kweli basi sijaona haja ya yeye kusimama hapo.
 
Sababu ya msingi ya Rais kusimama barabarani ni nini hasa, huku ni kutokujitambua na kutojua uwajibikaji, in rare occasion chipping from the grassroots it's a good thing, a big shame and worse empty mind
Rais anaweza kusimama popote,
 
Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

Kidumu CHAMA CHA MASELA
ukoloni mamboleo umetupa UHURU wa bendera,tuone kufuru za wenye HELA.
 
Kwani akisikiliza alafu akaliacha kwa RC,kuna shida gani?
Moja ya sifa ya Kiongozi bora ni kusikiliza!
Ili mawasiliano yakamilike,lazima kuwe na feedback kutoka kwa hadhira.
Communication ni 2 way process,na siyo 1 way.
 
Kilichomsimamisha njiani ni nini kama sio mataizo binafsi ya wananchi? Kwanini ana sima simama njiani ikiwa anaogopa maswali? Kwanini ana simama simama?
Kazi ya Rais sio kutatua matatizo binafsi ya raia. Kazi ya Rais ni kushughulika na kuzungumzia mambo ya kitaifa na kimataifa sehemu yoyote anayoona inafaa kufanya hivyo.
 
Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo kama shukrani ya kutimiza ahadi ya kufanyia kazi dukuduku lake na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.



Point za bure zinapotea.
 
Kwani akisikiliza alafu akaliacha kwa RC,kuna shida gani?
Moja ya sifa ya Kiongozi bora ni kusikiliza!
Rais katika nchi kubwa kama hii akianza kusikiliza kesi za mirathi, ugomvi wa mke na mume, kuibiana kuku n.k tutafika kweli??
 
Sasa yeye Rais kasimama pale kwenye kadamnasi kufanya nini,si angepita speed na kuwapungia mkono!
Rais anaweza kusimama popote kama vile raia mwingine yeyote anavyoweza kusimama popote.
 
Tungejiuliza kwanza kwanini kuwe na wananchi wengi wanaotaka kumweleza rais shida zao wakati ngazi za chini kuna wateule wa rais chungu nzima! Hili ndilo tatizolinalotakiwa kutatuliwa. Wabunge kwa nini hawatimizi majukumu? Wakuu wa wilaya nk kwa nini hawatekelezi majukumu? Jibu ni kuwa hawajioni kama wanawajibika kwa raia. Wanajiona kuwa rais ndiyo bosi wao. Bila kubadisha mfumo ni bure.
Unakuta mwananchi keshafikisha kero zao kwa ngazi za chini na ameshashugulikiwa ila unakuta hajaridhika anataka aende kwa Rais..Hilo lilijitokeza mara nyingi awamu ya Magufuli ambapo unakuta wamama waalishindwa kesi na rufaa zote kwenye ngazi za chini wakafanya vituko kwenye mikutano ya Magufuli wakidai kuwa wamedhulumiwa, kumbe hawakuwa na haki na wao ndio walikuwa wakosaji
 
Huwezi kuongoza nchi kubwa kama Tanzania kwa mfumo wa Rais kusikiliza matatizo binafsi ya watu nchi ikasonga mbele.

Wenzetu wanaojua maana ya Rais, waziri mbunge inapofanyika town Hall meeting watu wanauliza, wanatoa malalamiko yao mapendekezo kwa masuala ya mtaa, mji, jimbo au taifa. Sio malalimiko ya umenyang'anywa kiwanja na tajiri au umefukuzwa kazini ambayo ni masuala ya polisi na mahakama.
Kama ameenda hasikilizwi,afanyeje?
Kwanza, kwanini mnaweka assumption kuwa anataka kuongea mambo personal.Wengine huwa Wanaongea mambo ya Hospitali, Barabara,umeme nk,vitu ambavyo viongozi wa sehemu husika hawavifanyii kazi.
Unakumbuka ile shule ya Ubungo ilivyokuwa ovyo,watu wakarusha clip,Rais Magufuli akaiona na kuagiza ijengwe mara moja na ilijengwa.Je,wangekaa kimya ingejengwa?
Viongozi wa Tanzania Wilayani na Mikoani ni wazembe sana,Kwaiyo kwa Rais unayeijua tabia ya viongozi wako ni lazima utumie njia mbadala pia kujua matatizo ya Wananchi.
 
Back
Top Bottom