Rais Samia akutana na Baraza la Maaskofu (TEC), Kilaini aelezea Historia yake na utaifishaji wa mashule 1970

Rais Samia akutana na Baraza la Maaskofu (TEC), Kilaini aelezea Historia yake na utaifishaji wa mashule 1970

Huu ni ukuu wa Kanisa Katoliki la Roma, wasabato na walokole na nyie tafuteni "platform" zenu ili muweze kukutana na Rais.
makanisa ya kilokole hayana mifuno, askofu huyo huyo, Mweka hazina huyo huyo, Mtafuta manunuzi ya kanisa huyo huyo, Mtunza stoo huyo huyo, Signatory wa benki huyo huyo, Mwenyekiti wa bodi ya kanisa huyo huyo, mwesabu sadaka huyo huyo..
 
makanisa ya kilokole hayana mifuno, askofu huyo huyo, Mweka hazina huyo huyo, Mtafuta manunuzi ya kanisa huyo huyo, Mtunza stoo huyo huyo, Signatory wa benki huyo huyo, Mwenyekiti wa bodi ya kanisa huyo huyo, mwesabu sadaka huyo huyo..
Hizo labda ni ministry ila so called walokole kama TAG/EAGT/FPCT wana mifumo kuanzia jimbo mpaka makao makuu na wana taasisi nyingi chini yao kma vyuo,vituo vya media,shule, hospitali,NGOs n.k so mifumo ipo. More so wanayo CPCT ambayo ni umoja wa makanisa yote ya kipentekoste Tanzania so obviously wana platform.
 
Hizo labda ni ministry ila so called walokole kama TAG/EAGT/FPCT wana mifumo kuanzia jimbo mpaka makao makuu na wana taasisi nyingi chini yao kma vyuo,vituo vya media,shule, hospitali,NGOs n.k so mifumo ipo. More so wanayo CPCT ambayo ni umoja wa makanisa yote ya kipentekoste Tanzania so obviously wana platform.


No big no hakuna viongozi wa hovyo kama TAG.
 
Huu ni ukuu wa Kanisa Katoliki la Roma, wasabato na walokole na nyie tafuteni "platform" zenu ili muweze kukutana na Rais.

[emoji871]Mhubiri 8:9
Hayo yote nimeyaona, nami nimetafakari moyoni mwangu kila kazi ambayo imefanywa chini ya jua, wakati ambapo mwanadamu amemtawala mwanadamu mwenzake kwa kumuumiza.+

[emoji871]Katika vita vya Har–Magedoni, Ufalme wa Mungu utaziharibu serikali zote za wanadamu zilizojaa ukatili na ufisadi.
 
Rais Samia Suluhu Hassan anatarajia kukutana na Baraza la Maaskofu Katoliki anzania (TEC) leo Juni 25, 2021

Rais atakutana nao katika Makao Makuu ya TEC, Kurasini



==========

5:30 Asubuhi: Rais Samia Suluhu ameshafika na kuimbwa wimbo wa Taifa, kinachoendelea kwa sasa ni utambulisho wa maaskofu

KILAINI AELEZEA HISTORIA YA BARAZA LA MAASKOFU TANZANIA
5:45 Asubuhi:
Anaeongea kwa sasa ni Askofu Method Kilaini na anaongelea historia ya baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania. Kilaini amesema Baraza la Maaskofu ndio uongozi wa Kanisa Katolika na lilianza na ujio wa Kanisa Katoliki mwaka 1860.

Askofu Kilaini amesema Wamisionari walikuja na mambo matatu muhimu ambayo ni kueneza dini, kutibu wagonjwa na Elimu.

Kilaini amesema waingereza walikuwa wanaitawala Tanganyika kwa udhamini wa Umoja wa Mataifa hivyo hawakutaka kuwekeza. Ndipo Kanisa lilipoamua kujaza Ombwe lililobaki ambapo mwaka 1928 waliwekeana sera kwamba msisitizo uwe Shule. Kilaini anaendelea kwa kusema maaskofu waliwekea sera endapo fedha ni kidogo na inabidi kuchagua kujenga shule au Kanisa, ni bora kuchagua shule na kuacha kanisa na ndio umekuwa msimamo wa kanisa hadi leo.

Kilaini: Mwaka 1956 wakaunda Rasmi umoja wa barza la maaskofu linaloitwa TEC na kati ya waliounda, askofu mwafika alikuwa mmoja, Laurian Rugambwa akiwa askofu wa Rutabwa na polpole waliingia mpaka sasa unaona nyuso za waafrika pekee.

Baraza hili liliendelea na sera hiyohiyo mpaka tulivyofika Uhuru mwaka 1961 na wakaunga mkono juhudi zote alizokuwa anazinya mwalimu Julius Nyerere.

Alivyofika mwaka 1969/70, Nyerere alisema naona mna shule nyingi lakini nataka ziwe za watu wote, akazitaifisha. Mwaka 1970 wakati anataifisha, Baraza la Maaskofu Tanzania lilikuwa na shule za msingi 1,420. Shule za sekondari 44, vyuo vya ualimu nane halafu shule za ufundi ambazo hazikutaifishwa za wavulana 15 na wasichana 48.

Na hizi zilizotaifishwa, mama utakumbana na hii historia katika utawala wako kwasababu mashule mengine yako katikati ya mission, mbele ni kanisa, nyuma ni nyumba ya mapadri na kushoto nyumba ya kanisa, sasa tukotuko lakini tunaenda vizuri, miaka mingi tumekwenda kwenda lakini kila mara inabidi kutia nguvu sana ili kuwaza kukaakaa kwasababu hiki cha katikati hiki ni kiserikali serikali na kilichozunguka ni kimisheni kimesheni, imekuwa ni changamoto kila mara.

Tunakushukuru mama, unapoongea Lugha yako tunaipenda, usione tumevaa mabarakoa wote hapa, maaskofu wanatabasamu sana hapa, ni kwasababu ya matamko yako unayatoa, wote wanafurahi.

Noma sana kiongozi
 
Back
Top Bottom