Rais Samia akutana na Baraza la Maaskofu (TEC), Kilaini aelezea Historia yake na utaifishaji wa mashule 1970

Ushetani wake ni upi? na unatumia kipimo gani kupima ushetani wa kanisa kupitia mafundisho yake?

Alafu wewe ni muumini wa dhehebu gani ??
YESU KRISTO alisema, "Shetani ndiye baba ya uongo"

Sasa kama hujui basi fahamu kwamba kanisa katoliki linafundisha mambo ya "uongo". Kanisa hili lipo chini ya kivuli cha kuhubiri injili lakini injili inayohubiriwa ni ile ya uongo yenye lengo la kuwapotosha wanadamu na kuwafanya watumwa wa shetani.

Hili ni kanisa linaloongozwa na Ibilisi mwenyewe.

Ndugu, itafute KWELI na hiyo KWELI itakuweka huru. Soma Ufunuo 18:4-5
 
unaongea kwa kua sio mkatoliki au kwa kua hujanufaika moja kwa moja na ukatoliki lakini umekuzwa na kupata akili kwa uwepo wa kanisa katoliki.Kule kwenu kama sio kanisa katoliki maisha yangekuwaje? Heshimu aliyewakuza.Kanisa limelilea taifa lilipokua halijiwezi kutoa huduma sasa mmekua mnakua jeuri.Kama sio shule za kanisa akina mkapa,kikwete,makamba wangesoma wapi?Tazama maeneo ya wananchi wanaoshi karibu na parokia maisha yao yalivyo na unafuu.
Mama aache kutafuta huruma za kisiasa kwa hao wakatoliki,wanafanya biashara walipe kodi
 
Tatizo la waumini wa madhehebu madogo kama yako hata kielimu uelewa wenu ni mdogo.Haujui hata aina ya vitabu vya kibiblia Haujui hata mazingira ya uandishi wake ila unajikuta unaijua Biblia kindaki ndaki [emoji23][emoji23][emoji23] Elimu elimu elimu
Mimi siandiki ili kubishana, bali naandika ili niwasaidie wale wanaotaka kuijua KWELI ili hiyo KWELI iwaweke HURU.

Wewe huyajui "Maandiko". Udogo wa kanisa siyo hoja. Hata YESU KRISTO alisema "kundi lake litakuwa dogo".

Endelea kudanganywa na kulevywa na mvinyo ya huyo KAHABA.

Soma Ufunuo 17:8
Kanisa katoliki ndilo kanisa linaloongoza duniani kuua watakatifu wa MUNGU. Soma historia ya utawala wa Rumi na utaona jinsi kanisa lilivyoua maelfu ya watu waliokuwa wanaishika INJILI ya KWELI.
 
Kama huwezi kutofautisha kati ya Vatican na Rome basi uelewa wako wa Biblia na vifungu ulivyovinukuu hapa ni mdogo sana. Soma Basic theology na basic philosophy ndiyo utajua maana ya hayo maandiko.
 
Injili ya kweli ni ile inayohubiriwa na wanaofufua watu hewa,wanaowafanya waumini wajihisi matajiri bila kufanya kazi eti wasubiri muujiza wa Mungu,wanaowauzia watu Maji ya Chupa za Bharesa kwa shilingi 2000,vitambaa vyeupe kwa shilingi 3000 nk..eti vina Muujiza.Kanisa katoliki halifundishi watu kuishi kwa hisis hisia bali linawafundisha watu kuishi katika mazingira halisi ya ubinadamu,kuwatengeneza watu kuwa msaada kwa jamii na sio makupe,kua na uwezo wa kufikiri wao wenyewe na sio mchungaji kufikiri kwa niaba yao.Kuishi Maisha ya kumtegemea Mungu kwa kuwa na misingi bora ya familia ili kua Raia wema na sio kuishi kama kwale au njiwa.
 
Ndio maana nikasema elimu ni muhimu sana hata katika masuala ya kiimani.Kwa hiyo wewe unahisi unaijua Biblia na maandiko kuliko Padre aliyesomea Falsafa ya Biblia kwa miaka zaidi ya 10 tena kwa uongozi wa roho mtakatifu? Kweli itakayokuweka huru ni kuijua dhambi na kuikimbia wala haihusiani na kanisa katoliki.Wewe unawafahamu watakatifu wakatoliki? Unafahamu historia ya wafiadini? Mt. Stefano? Mt. Karoli Lwanga na mashahidi wa Uganda? Jibu ni huwajui [emoji23][emoji23][emoji23] Uko busy na ufunuo wa Elen G White na kununua maji ya upako!
 
Umeandika vyema kabisa!
 
Ni jambo la busara kuacha kutumia salamu zote za kidini katika mikutano yoyote turudi kama tulivyokuwa zamani ziko njia nyingi za kuanza kwa mikutano. Ndugu wageni waalikwa, .... na .... inafuatwa protocol basi huku tuache kwenda siko kabisa.
Nakubaliana na wewe sioni mantiki ya kutoa salamu nyingi za kidini ambazo haziongezi wala kupunguza chochote.
 
Kama huwezi kutofautisha kati ya Vatican na Rome basi uelewa wako wa Biblia na vifungu ulivyovinukuu hapa ni mdogo sana. Soma Basic theology na basic philosophy ndiyo utajua maana ya hayo maandiko.
Wewe ulisema Vatican haihusiani na Roma, sasa nimekuwekea ushahidi wa wazi unakuja na hoja ya "theology".

Ndugu yangu tambua kwamba akina Paulo, Petro, Yohana n.k. hawakusoma "theology" lakini walijaliwa kuzijua "siri" za Ufalme wa MUNGU.

"basic theology and philosophy are foolishness to GOD. It is written in 1 Corinthians 3:19

"For the wisdom of this world is foolishness to God. As the Scriptures say, “He traps the wise in the snare of their own cleverness.”

ROHO MTAKATIFU ni zaidi ya "theology" na elimu yoyote ile ya kidunia.
 
Nadhani ndio mtaji wa wanasiasa, kuhakikisha makundi yote anayawin possibly ndani kwa ndani anakereketwa 😂😂
 
Huo ufunuo mim naweza sema ni dini ya Taoism wewe unasemaje?
 
Mkuu tunarudi pale pale uongo wa mafundisho ya kanisa katoriki unapima kutumia ithibati ipi??

Nashangaa unaleta habari za ufunuo sasa huo ufunuo unaeleza vipi uongo juu ya mafundisho ya kanisa katoriki?
 
Eti ile kujiita jiwe walijua hatakufa!!!sasa na leo Mama alivyo maliza suala la bandari ya bagamoyo, ndiyo huko yapo yana galagala tu!!
 
Mwendazake alikuwa ni shetani aliyejificha nyumba ya ucha Mungu feki ndio maana Mungu wa kweli aliamua kumzamisha ili nchi ipate kupumua.
 
Mkuu tunarudi pale pale uongo wa mafundisho ya kanisa katoriki unapima kutumia ithibati ipi??

Nashangaa unaleta habari za ufunuo sasa huo ufunuo unaeleza vipi uongo juu ya mafundisho ya kanisa katoriki?
UKWELI ni nini?

Kweli ni NENO la MUNGU na hilo NENO limeandikwa kwenye Biblia. Sasa kipimo cha "uongo" ni KWELI.

Kanisa katoliki linafundisha kinyume kabisa na KWELI ya NENO la MUNGU.
Soma Wagalatia 1:6-9
 
Kwa dini ya Kislaam, Yesu au Issa ni miongoni mwa Mitume wa Mwenyenzi Mungu. Kuamini na kuheshimu
Mitume ni mojawapo wa nguzo za Imaan kwenye Uislaam!
 
UKWELI ni nini?

Kweli ni NENO la MUNGU na hilo NENO limeandikwa kwenye Biblia. Sasa kipimo cha "uongo" ni KWELI.

Kanisa katoliki linafundisha kinyume kabisa na KWELI ya NENO la MUNGU.
Soma Wagalatia 1:6-9
Mkuu leta hayo mafundisho ya uongo ya kanisa katoriki?

Na unauhakika gani kwamba kifungu hicho kinaongea kuhusu kanisa katoriki kuhusu mafundisho yao? Mimi naweza sema kifungu hicho kinazungumzia mafundisho ya uongo ya dini ya Taoism
 
Baba wa uongo wamedanganya kitu gani Leta hayo mafundisho mkuu sio kuleta ufunuo ufunuo
 
Mkuu leta hayo mafundisho ya uongo ya kanisa katoriki
Nilishaandika kila kitu kuhusu mafundisho ya kanisa katoliki yanayopingana na "Maandiko".

Nenda kwenye jukwaa la Dini kule utakuta post zangu kuhusu "uongo" wa kanisa katoliki. Ni mambo mengi sana tena sana.

Kwa mfano, angalia Amri kumi za MUNGU zinazofundishwa na kanisa katoliki halafu linganisha na zile zilizoandikwa kwenye kitabu cha KUTOKA 20:1-17

Halafu soma ISAYA 8:19 Kumbukumbu la torati 18:11 uone ni jinsi gani MUNGU amekataza kuwaomba "wafu" lakini kanisa lako linafundisha na kuamini katika kuwaomba wafu.

Soma Mathayo 23:9 halafu uniambie ni kwanini Kiongozi wa kanisa lako unamwita "baba mtakatifu".

Hayo ni machache tu nimekudokeza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…