Rais Samia amemaliza ziara ya Mkoa wa Geita bila kuruhusu wananchi kuuliza maswali?

Rais Samia amemaliza ziara ya Mkoa wa Geita bila kuruhusu wananchi kuuliza maswali?

Kero zao wapeleke kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi ndiyo wawakilishi wa Rais
Mfano, January Makamba amewatapeli wananchi wanaletewa umeme na ametenga Bilioni 57 hadi leo hakuna Hata senti tano umetolewa na hakuna kilichofanyika, wananchi wakamwambie mkuu wa mkoa au wilaya Ili hali Rais kafika Geita?

Kama hataki maswali mnakusanya wanachi kuwaambia nini Sio mtumie Tv na radio wananchi wakae nyumbani kumsikiliza?
 
Mfano Rais ameambiwa Barabara ya Geita kwenda Kahama ni kms 58 na imewekwa kwenye Ilani ya ccm vipindi viwili na haijafanyiwa kazi hakujibu chochote.

Pili ameelzwa suala la kuigawa wilaya ya Geita vijijini kupata wilaya mpya ya Busanda wananchi wanatembea kms 107 kupata huduma hakujibu chochote.

Tatu makamba kudanganya wananchi kuhusu upatikanaji wa umeme Kwenye maeneo ya uchimbaji wa dhahabu mama hajasema ni Lini pesa zitatolewa ili kazi ianze na kila siku ni maneno matupu.

Ninajiuliza mkoani Geita ni nini wamepata au kufanikiwa kutokana na ziara ya Rais ?
 
Mfano Rais ameambiwa Barabara ya Geita kwenda Kahama ni kms 58 na imewekwa kwenye Ilani ya ccm vipindi viwili na haijafanyiwa kazi hakujibu chochote...

Sh57 bilioni kupeleka umeme kwa wachimbaji Geita​

Muktasari:​

Wizara ya Nishati imetenga Sh57 bilioni kwa ajili ya kupeleka umeme kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu mkoani Geita.

Mwanza. Wizara ya Nishati imetenga Sh57 bilioni kwa ajili ya kupeleka umeme kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu mkoani Geita.

Akizungumza leo Jumamosi, Oktoba 10, 2022 kwenye mkutano wa hadhara unaofanyika katika viwanja vya Kalangalala mjini Geita, Waziri wa Nishati, January Makamba amesema huo ni mpango mahususi wa wizara hiyo kuwapelekea umeme wachimbaji hao wanaotumia majenereta katika utafutaji wa madini hayo.

“Tumetenga jumla ya Sh57 bilioni kupeleka umeme kwa wachimbaji wadogo, kati ya hizo Sh7 bilioni ni kupitia REA katika maeneo 39 na Sh50 bilioni ni za Tanesco kupeleka umeme katika maeneo ambayo wachimbaji wadogo wanahitaji,”amesema Makamba.

Amesema wamepeleka umeme mwingi (Megawati 90) mkoani Geita kuliko unaohitajika kwa sababu matumizi yatakua na umeme utakaohitajika miaka ijayo tayari utakuwepo.

“Sisi kama Wizara kwa muongozo na maelekezo yako tumeamua kuweka mkazi mahususi kwa kitu tunakiita gridi ya Magharibi.

“Yaani kwa upande wa mikoa ya Kanda ya Ziwa na Magharibi kuwe na gridi yake mahususi ambapo tutajenga vituo vingi zaidi vya kupokea umeme, tutajenga njia nyingi zaidi za kusafirisha umeme na tutazalisha umeme mwingi katika mikoa hii,” amesema

Amesema kwa sasa mipango ya kuzalisha umeme katika mikoa hiyo ambayo ina fedha ni karibu megawati 400 ambapo gridi hiyo itakuwa inajitegemea ili yakitokea matatizo ya umeme eneo hilo lipate umeme wa kutosha.
 
January Makamba ni muongo sana. Tunataka Fedha hizi zitolewe Kesho Jumatatu Ili tuwe na Imani na Mama Samia vinginevyo tunarudi Enzi ya mzee Makamba na JK wake
 
Not everything is for everyone. Usikilizaji wa kero za wananchi moja kwa moja uliwezwa na Magufuli tu. Huyu wa sasa mtamuonea tu, mhurumieni.
EfKjCp3X0ActKyg.jpeg
 
Nimeona maajabu Mkoa wa Geita.

Kila Rais anakopita haruhusu wananchi watoe yaliyo moyoni mwao kwa nini?

Ukweli wananchi wana kero nyingi ambapo JPM alikuwa anawasikiliza na watu kuuliza sasa mikutano imekuwa kinyume.

Sio kila kero unapeleka kwa Mh. Rais, yaani kila mwananchi aanze kusema kero yake kwa Mh. Rais, huo utakuwa sio mkutano na muda unatoka wapi? Wasaidizi wa Mh. Rais wako kibao na wabunge wa Geita wapo..

Alafu kero zingine waambieni baba na mama zenu, acheni ujinga. Sio kila kero kwa Mh. Rais, hiyo sio
 
Acheni kumtetea mama yenu. Kwa ufupi ni mweupe mno hawezi jibu chochote, hata akiulizwa bajeti ya nchi ni shilingi ngapi utakuwa mtiti.

Jana anazindua barabara cha kushangaza hajui hata urefu wa barabara hiyo, hadi kauliza wasaidizi wake wakataja urefu. Nchi hii tunapitia magumu mengi sana.
 
Sio kila kero unapeleka kwa Mh. Rais, yaani kila mwananchi aanze kusema kero yake kwa Mh. Rais, huo utakuwa sio mkutano na muda unatoka wapi? Wasaidizi wa Mh. Rais wako kibao na wabunge wa Geita wapo..

Alafu kero zingine waambieni baba na mama zenu, acheni ujinga. Sio kila kero kwa Mh. Rais, hiyo sio

wewe mburura kweli . hujui kuna kero hushindikana huku chini sababu ya kujuana na kuogopana. na rais huja kumaliza palepale hukuona jpm alivyokuwa anayamaliza uwanjani , au wewe ni mkenya haishi tz
 
Nimeona maajabu Mkoa wa Geita.

Kila Rais anakopita haruhusu wananchi watoe yaliyo moyoni mwao kwa nini?

Ukweli wananchi wana kero nyingi ambapo JPM alikuwa anawasikiliza na watu kuuliza sasa mikutano imekuwa kinyume.

JPM alikuwa hasikilizi kero bali ilikuwa inaandaliwa watu wanamuuliza maswali ya kutafutia kiki za kisiasa. Ilikuwa ikitokea bahati mbaya akauliza mtu ambaye hajapangwa, alikuwa anaishia kumkejeli na vitisho. Yale maigizo tulikuwa tunayoana.
 
Acheni kumtetea mama yenu. Kwa ufupi ni mweupe mno hawezi jibu chochote, hata akiulizwa bajeti ya nchi ni shilingi ngapi utakuwa mtiti.

Jana anazindua barabara cha kushangaza hajui hata urefu wa barabara hiyo, hadi kauliza wasaidizi wake wakataja urefu. Nchi hii tunapitia magumu mengi sana.

Simtetei mama, ila dhalimu alikuwa bingwa wa kupika data, usishangae akitaja kilomita za uongo.
 
Nimeona maajabu Mkoa wa Geita.

Kila Rais anakopita haruhusu wananchi watoe yaliyo moyoni mwao kwa nini?

Ukweli wananchi wana kero nyingi ambapo JPM alikuwa anawasikiliza na watu kuuliza sasa mikutano imekuwa kinyume.
Maswali majibu yake wanayo watendaji wa mitaa/vitongoji- kwangu mimi hao ndio serikali
 
Simtetei mama, ila dhalimu alikuwa bingwa wa kupika data, usishangae akitaja kilomita za uongo.
Dhalimu ndio nani? Mada inamhusu mama yenu, wewe unakwenda kwa wasiohusika. Hakika Jembe bado linawatesa. Kila kukicha na usiku hamlali mnatafuta mapungufu yake tu. Sawa, lakini haibadili kitu. Legancy yake itabaki maana aliyoyafanya hamuwezi kuyabadilisha wala kumnyang'anya. Hakika kaacha legacy kubwa.

Mkitaka kumpoteza ni kukaa kimya na kuacha kutaja jina lake na matendo yake, vinginevyo mkiendekea hivi hata wajukuu wenu watakuta umaarufu wake uko juu na hapo ndipo mtakapo jua hamjui.
 
Back
Top Bottom