Rais Samia amemaliza ziara ya Mkoa wa Geita bila kuruhusu wananchi kuuliza maswali?

Rais Samia amemaliza ziara ya Mkoa wa Geita bila kuruhusu wananchi kuuliza maswali?

Dhalimu ndio nani? Mada inamhusu mama yenu, wewe unakwenda kwa wasiohusika. Hakika Jembe bado linawatesa. Kila kukicha na usiku hamlali mnatafuta mapungufu yake tu. Sawa, lakini haibadili kitu. Legancy yake itabaki maana aliyoyafanya hamuwezi kuyabadilisha wala kumnyang'anya. Hakika kaacha legacy kubwa.

Mkitaka kumpoteza ni kukaa kimya na kuacha kutaja jina lake na matendo yake, vinginevyo mkiendekea hivi hata wajukuu wenu watakuta umaarufu wake uko juu na hapo ndipo mtakapo jua hamjui.

Jina la nani limetajwa hapo au unajishuku?
 
Mfano Rais ameambiwa Barabara ya Geita kwenda Kahama ni kms 58 na imewekwa kwenye Ilani ya ccm vipindi viwili na haijafanyiwa kazi hakujibu chochote.

Pili ameelzwa suala la kuigawa wilaya ya Geita vijijini kupata wilaya mpya ya Busanda wananchi wanatembea kms 107 kupata huduma hakujibu chochote.

Tatu makamba kudanganya wananchi kuhusu upatikanaji wa umeme Kwenye maeneo ya uchimbaji wa dhahabu mama hajasema ni Lini pesa zitatolewa ili kazi ianze na kila siku ni maneno matupu.

Ninajiuliza mkoani Geita ni nini wamepata au kufanikiwa kutokana na ziara ya Rais ?
Mkuu wa mkoa alitangaza zawadi ya ng'ombe 2, na kilo 100 za mchele kwa Rais, bado umasikini, Maradhi na ujinga vinatuandama
 
Kwani katiba inasemaje kuhusu ilo? Kiongozi
 
Nimeona maajabu Mkoa wa Geita.

Kila Rais anakopita haruhusu wananchi watoe yaliyo moyoni mwao kwa nini?

Ukweli wananchi wana kero nyingi ambapo JPM alikuwa anawasikiliza na watu kuuliza sasa mikutano imekuwa kinyume.
 
wewe mburura kweli . hujui kuna kero hushindikana huku chini sababu ya kujuana na kuogopana. na rais huja kumaliza palepale hukuona jpm alivyokuwa anayamaliza uwanjani , au wewe ni mkenya haishi tz
 
Kero zao wapeleke kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi ndiyo wawakilishi wa Rais
 
Sio kila kero unapeleka kwa Mh. Rais, yaani kila mwananchi aanze kusema kero yake kwa Mh. Rais, huo utakuwa sio mkutano na muda unatoka wapi? Wasaidizi wa Mh. Rais wako kibao na wabunge wa Geita wapo..

Alafu kero zingine waambieni baba na mama zenu, acheni ujinga. Sio kila kero kwa Mh. Rais, hiyo sio
Acha upopoma,rais ni mtumishi wa wananchi na unaposema eti Kuna wawakilishi mbona kwenye swala la mradi inayojengwa chini ya KIWANGO hatuoni hao wawakilishi wakienda kuonyesha izo kasoro mpaka waziri mkuu aende ivi watu km wewe mlizaliwaje Tanzania?rais kusikiliza wananchi wako ni jambo zuri Niko inapopata ufahamu wa nn kinachoendelea huko na wore tunajua wazi hao unaowaita wawakishi wanavyofanya kazi.kwanza kuwaoma tu mziki wake sio mchezo
 
JPM alikuwa hasikilizi kero bali ilikuwa inaandaliwa watu wanamuuliza maswali ya kutafutia kiki za kisiasa. Ilikuwa ikitokea bahati mbaya akauliza mtu ambaye hajapangwa, alikuwa anaishia kumkejeli na vitisho. Yale maigizo tulikuwa tunayoana.
Na yeye awe na wakupangwa tumuome akijibu
 
Hana muda wa maigizo ya kitoto.
Kwahiyo mkuu ulifuatilia wale watu waliyokuwa wanaeleza kero zao kwa Magufuli na ukagundua kuwa waliyokuwa wanaeleza sio kweli ni uongo tu?
 
Kwahiyo mkuu ulifuatilia wale watu waliyokuwa wanaeleza kero zao kwa Magufuli na ukagundua kuwa waliyokuwa wanaeleza sio kweli ni uongo tu?

Kwanza huo ni utaratibu wa kawaida wa wanaccm, lakini huo ulikuwa ni utamaduni wa Magufuli kupanga wetu ili ionekane anasikiliza wanyonge. Na ikitokea ukapewa nafasi ya kuuliza kisha ukamuuliza asichopenda alikuwa anaishia kukushushua na kukudhalikisha. Unakumbuka mtu aliyeambiwa abaki na mavi yake nyumbani? Unakumbuka yule aliyehoji tatizo la maji akamwambia ametumwa kuvuruga mkutano wake?
 
Magufuli alikuwa anawapanga watu wamuulize maswali aliyiyaandaa,alikuwa bonge la msanii
 
Kwanza huo ni utaratibu wa kawaida wa wanaccm, lakini huo ulikuwa ni utamaduni wa Magufuli kupanga wetu ili ionekane anasikiliza wanyonge. Na ikitokea ukapewa nafasi ya kuuliza kisha ukamuuliza asichopenda alikuwa anaishia kukushushua na kukudhalikisha. Unakumbuka mtu aliyeambiwa abaki na mavi yake nyumbani? Unakumbuka yule aliyehoji tatizo la maji akamwambia ametumwa kuvuruga mkutano wake?
Hujajibu lakini kwamba ulifuatilia watu waliyoeleza kero zao na ukagundua haikuwa kweli ni mchongo tu?
 
Sio kila kero unapeleka kwa Mh. Rais, yaani kila mwananchi aanze kusema kero yake kwa Mh. Rais, huo utakuwa sio mkutano na muda unatoka wapi? Wasaidizi wa Mh. Rais wako kibao na wabunge wa Geita wapo..

Alafu kero zingine waambieni baba na mama zenu, acheni ujinga. Sio kila kero kwa Mh. Rais, hiyo sio
Wewe ni mlamba asali uchwara tu, kwani Mbona Jembe aliwasikiliza na kutatua kerozao papo kwa papo.

Hao wateule nao ni binadamu wanamapungufu mengi tu,angalau mkuu akiruhusu anaweza kujua mambo yaliyojificha na kuyatolea maamuzi ama miongozo.
Tatizo ni usubutu wa kuwawajibisha wasio wajibika.
 
Nimeona maajabu Mkoa wa Geita.

Kila Rais anakopita haruhusu wananchi watoe yaliyo moyoni mwao kwa nini?

Ukweli wananchi wana kero nyingi ambapo JPM alikuwa anawasikiliza na watu kuuliza sasa mikutano imekuwa kinyume.
Unamkumbuka kijana wa makambako? raisi wa wanyonge aliagiza polisi wamshughulikie kisa kuinua bango tu? hamkusema kitu mlikenua.
unayakumbuka mabango ya TABORA uwanja wa Alhasan mwinyiiii? wananchi wale waliambiwa wakalalie na waume zao...... unakumbuka unakumbuka
 
Dhalimu ndio nani? Mada inamhusu mama yenu, wewe unakwenda kwa wasiohusika. Hakika Jembe bado linawatesa. Kila kukicha na usiku hamlali mnatafuta mapungufu yake tu. Sawa, lakini haibadili kitu. Legancy yake itabaki maana aliyoyafanya hamuwezi kuyabadilisha wala kumnyang'anya. Hakika kaacha legacy kubwa.

Mkitaka kumpoteza ni kukaa kimya na kuacha kutaja jina lake na matendo yake, vinginevyo mkiendekea hivi hata wajukuu wenu watakuta umaarufu wake uko juu na hapo ndipo mtakapo jua hamjui.
jembe la kua na kuteka watu lisilo wapenda
RIP Anzory Gwanda
 
Back
Top Bottom