Rais Samia ampendekeza Profesa Janabi kuwa Mkurugenzi wa WHO-Afrika

Rais Samia ampendekeza Profesa Janabi kuwa Mkurugenzi wa WHO-Afrika

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza kwamba Profesa Mohamed Janabi atakuwa mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika katika uchaguzi utakaotangazwa na shirika hilo.

Rais Samia ameyasema hayo leo Desemba 10, 2024 baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali wateule wakiwemo Mawaziri na Manaibu wao.

Profesa Janabi ambaye ni Mshauri wa Rais masuala ya Afya na Tiba na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, atagombea nafasi hiyo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi Mteule, Dkt. Fastine Ndugulile aliyefariki usiku wa kuamkia Novemba 27, 2
024.
 

Attachments

  • 20241210_143953.jpg
    20241210_143953.jpg
    225.7 KB · Views: 3
Wewe lini utapatiwa kitengo uache kusumbua humu?
Mtu mjinga kama huyo utampa kitengo Gani ambacho anaweza kukundikia strategic plan hata ya siku Moja tu na baadae akuandikie report ya utekelezaji yenye mashiko? Huyu akiingia ofisini ni kububujikwa na machozi tu muda wote! Huyu hafai hata kuongoza kikao Cha familia bro, acha kimuongoza demu wake! Mana hakuna demu mwenye akili anaweza kuwa na zezeta kama hili ambalo 24/7 litakua ni kumsifia mamake tu!
 
Profesa janabi kugombea nafasi ya ndugulile who ni sawa na kunyoosha mikono juu ! Pr janabi hana ushawishi wowote kimataifa ni Bora tungechukuwa Damu changa ! Hamisi kigwangala angefaa sema kwa sababu hamisi viongozi wenzake wanamnyea sana ,kigwangala sijui aliikosea nini serikali hata huo ubunge hawamtaki ni basi tu kwakuwa hamna namna! Ila kigwangala makosa yake ni machache sana sema ndani ya ccm anamaadui wengi Sana , kigwangala kwa sasa ni Bora mara mia kuliko pr janabi sema kigwangala ni yatima ndani ya ccm kwa sasa
 
Profesa Janabi alikuwa Japan anapata hela ndefu sana JK akambembeleza arudi nyumbani sasa huyu anataka kumpeperusha tena.
 
Rais Samia Suluhu amesema wasifu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Mohamed Janabi unatosheleza kuingia kwenye kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya Ukurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika. Nafasi hiyo iko wazi baada ya Mkurugenzi Mteule Dkt. Faustine Ndugulile kufariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 27 Novemba, 2024 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu. Zaidi soma TANZIA - Dkt. Faustine Ndugulile afariki Dunia

Pia soma
- Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika

View attachment 3173647
Habari mbaya hii kwa Kigwangwala
 
IMG-20241210-WA0046.jpg

Ni kweli Rais amempendekeza Prof Janabi kwa ajili ya kugombea nafasi iliyoachwa wazi na Dr Ndugulile hivi karibuni. Nilikuwa naijua CV ya marehemu vizuri sana, lakini nina wasiwasi na huyu Profesa Janabi ambaye amepata umaarufu kwenue mitandao ya Jamii dhidi ya kulakula hovyo.

Awali alikuwa Daktari binafsi wa Rais wa awamu ya 4 Jakaya Kikwete kabla hajapata kuwa mkuu wa JKCI na kisha MNH.

Je ataweza kushinda kiti hicho kama Ndugulile?

Basi tupeni wasifu (CV) wake hapa
 
Profesa Mohamed Yakub Janabi ni Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili tangu Oktoba 2022 mpaka sasa. Kabla ya Hapo alikuwa Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Jakaya Kikwete.

Mwaka 2005 alichaguliwa kuwa daktari binafsi wa Rais mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Disemba 8 2024 ameteuliwa kuwa mshauri wa Raisi kwenye maswala ya afya, akiwa anaendelea na majukumu yake kama Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya taifa Muhimbili.

Elimu​

Dkt. Janabi amepata kusoma katika vyuo mbali mbali ndani na nje ya Tanzania. Vyuo hivyo ni pamoja na:-
  1. Kharkov Medical Institute (Russia)
  2. Liverpool School of Tropical Medicine (England)
  3. University of Queensland Medical School (Australia)
  4. Graduate School of Medicine Osaka University Hospital (Japan)
  5. Bergen University (Norway)
NYONGEZA

MKURGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili, Prof. Mohamed Janabi, juzi aligeuka kivutio kijijini kwake Mtakanini, Kata ya Msindo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma, ambako na timu yake ya wataalamu walikwenda kutoa huduma za afya.

Wananchi hao walifurahi kumwona mtoto wao ambaye ni maarufu kwa kutoa ushauri wa kutunza afya kwa kula vyakula vinavyofaa na umuhimu wa kufanya mazoezi, huku wakishukuru kwa uamuzi huo na kuomba muda zaidi kwa wataalamu kutoa huduma.

Daktari huyo bingwa ambaye amewahi kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), ni mzaliwa wa kijiji hicho ambaye elimu yake ya msingi alianzia kijijini hapo.

Prof. Janabi alikwenda kuungana na madaktari bingwa watatu waliokuwa wakiendelea kutoa huduma kwa wagonjwa wa moyo, kisukari, tezi dume na saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa gazeti hili, wananchi hao walisema wamefurahishwa na mtoto wa nyumbani kuwakumbuka na kutumia utaalamu wake na wenzake kwenda kuwasaidia.

“Tulimsubiri yeye na wataalamu wengine kwa hamu kubwa. Wamekaa nasi kwa wiki moja tunatamani wangeendelea kukaa nasi au kwenda kwenye vituo vingine. Tunatamani mpango huu uwe endelevu tupate alimu ya afya kama anavyotoa kwa wengine huko aliko,” alisema Cartas Nyoni.

“Profesa Janabi ni mwanetu, amekuja kwa muda mfupi tunatamani angekaa muda mrefu ili watu waelewe vizuri, tunawaomba wawe wanatutembelea wakiwa na vifaa vya kisasa kama walivyokuja navyo sasa. Wananchi wanyonge wamepata huduma vizuri na bure wangekwenda kwenye vituo vya afya, hospitali za rufani wangetozwa fedha nyingi, tunaomba huduma kama hizi kwa wananchi tunaoishi vijijini,” alisema.
 
Profesa Mohamed Yakub Janabi ni Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili tangu Oktoba 2022 mpaka sasa. Kabla ya Hapo alikuwa Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Jakaya Kikwete.

Mwaka 2005 alichaguliwa kuwa daktari binafsi wa Rais mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Disemba 8 2024 ameteuliwa kuwa mshauri wa Raisi kwenye maswala ya afya, akiwa anaendelea na majukumu yake kama Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya taifa Muhimbili.

Elimu​

Dkt. Janabi amepata kusoma katika vyuo mbali mbali ndani na nje ya Tanzania. Vyuo hivyo ni pamoja na:-
  1. Kharkov Medical Institute (Russia)
  2. Liverpool School of Tropical Medicine (England)
  3. University of Queensland Medical School (Australia)
  4. Graduate School of Medicine Osaka University Hospital (Japan)
  5. Bergen University (Norway)
Wikipedia.
 
Back
Top Bottom