Rais Samia analazimisha kuizanzibarisha Tanganyika kwa nguvu

Rais Samia analazimisha kuizanzibarisha Tanganyika kwa nguvu

Brigadier Mwakanjuki RIP Mnyakyusa.

Abdallah Natepe RIP Mmakonde.

Omar Mapuri Mmakonde.

Tito Okello RIP Mjaluo wa Uganda.

Hao ni wamatumbi wanne kutoka huku bara ambao historia yao inaheshimika huko ZNZ, vijana wadogo humu JF jifunzeni kwanza historia yenu kabla hamjaandika chochote.
Hawa hawawezi kuhalalisha uteuzi wa wapemba kwenye nyadhifa mbalimbali na kuwarundika hapa Tanganyika wakati vijana wa Tanganyika hawana kazi.
 
Unguja na Pemba ukizichanganya kwa pamoja zina idadi ya watu wasiozidi milioni mbili, Kinondoni peke yake ina watu milioni mbili, kwanini huyo kiongozi kutoka bara aende huko Pemba eti akagombee nafasi ya uongozi?.

Muungano unalo somo la upendo alilotuachia Mwalimu Nyerere na Hayati Mzee Karume.
Kwahiyo ni muungano wenye macho na mipaka kwq baadhi ya watu wa upande fulani? Kwani mtu wa bara akienda kuongoza huko Zanzibar anaondoka na hicho kisiwa? Ni hivi, ni muungano outdated, ndio maana mtutu wa bunduki ndio unaufanya uendelee kuwepo. Muungano ambao kero haziishi huo sio muungano wa wananchi Bali wa viongozi.
 
Hawa hawawezi kuhalalisha uteuzi wa wapemba kwenye nyadhifa mbalimbali na kuwarundika hapa Tanganyika wakati vijana wa Tanganyika hawana kazi.
Vijana wa Tanganyika wapo milioni zaidi ya 60, hakuna ambacho wanaweza kusaidiwa na serikali yao kama hawatafuti kazi kwa juhudi zao wenyewe.

Pemba na Unguja zina watu milioni mbili sawa sawa na idadi nzima ya watu wa Kinondoni peke yake, tuachane na huu upuuzi wa ubaguzi hautusaidii chochote.
 
Hivi viongozi wapemba waliopo Tanganyika ni akina nani?
Ni wengi sana mkuu. Wamejaa kwenye vyeo vya DAS, RAS, wakurugenzi na wenyeviti wa bodi za mashirika na wakala zote za serikali.Mmojawapo ni yule mpemba bosi wa NECTA.
 
Vijana wa Tanganyika wapo milioni zaidi ya 60, hakuna ambacho wanaweza kusaidiwa na serikali yao kama hawatafuti kazi kwa juhudi zao wenyewe.
Matope! Kwa hiyo wewe unaona ni halali kwa wapemba kuteuliwa na Rais kujaza vyeo lakini vijana wa Tanganyika watafute kazi wenyewe? You cant be serious dude!
 
Kwahiyo ni muungano wenye macho na mipaka kwq baadhi ya watu wa upande fulani? Kwani mtu wa bara akienda kuongoza huko Zanzibar anaondoka na hicho kisiwa? Ni hivi, ni muungano outdated, ndio maana mtutu wa bunduki ndio unaufanya uendelee kuwepo. Muungano ambao kero haziishi huo sio muungano wa wananchi Bali wa viongozi.
Nimetoa mifano ya majina ya watu wa bara waliozaliwa na kukulia huko visiwani. Tito Okello aliyesimamia mapinduzi huko Unguja asili yake ni Uganda.

Hakuna wanachoweza kukifanya wananchi bila ya kuongozwa na viongozi.
 
Matope! Kwa hiyo wewe unaona ni halali kwa wapemba kuteuliwa na Rais kujaza vyeo lakini vijana wa Tanganyika watafute kazi wenyewe? You cant be serious dude!
Wapemba wapo wangapi?, mbona huwataji wasukuma aliowajaza marehemu JPM kwenye kila halmashauri?.
 
Misingi kibao ya Nyerere ilivunjwa na bado tuko vilevile na wapo waliodhani Nyerere akifa Tz tutachinjana lkn bado tuko vilevile, hivyo vitisho vimepitwa na wakati.
Watanzania ni wamoja, changamoto ipo kwa wanasiasa ambao ni wachache lakini wenye ushawishi mkubwa.
Hakuna mkulima, mfanyabiashara, mwanafunzi anayembagua mpemba huku bara, hata jobless wanaelewana tu.
Wale wanaotegemea jasho la hao wanaoelewana ndiyo shida.
Tunahitaji uongozi utakaoimarisha ushirikiano kwa faida ya wote.
 
Wapemba wapo wangapi?, mbona huwataji wasukuma aliowajaza marehemu JPM kwenye kila halmashauri?.
Kwa hiyo wewe unataka kuwe na mwendelezo wa uovu tangu enzi za JPM hadi sasa badala ya kukemea na kuutokomeza?
 
Kwa hiyo wewe unataka kuwe na mwendelezo wa uovu tangu enzi za JPM hadi sasa badala ya kukemea na kuutokomeza?
Uwezo wa kazi haujali rangi wala asili. Mbaguzi ndiye anayemtazama mtu anatokea wapi bila kutazama nini anachokileta kwenye ufanisi wa kazi.
 
Uwezo wa kazi haujali rangi wala asili. Mbaguzi ndiye anayemtazama mtu anatokea wapi bila kutazama nini anachokileta kwenye ufanisi wa kazi.
Mkuu tunazunguka halafu tunarudi pale pale. Rais Samia hana uhalali kisheria kuwateua wapemba kuja kujaza nafasi za watanganyika hapa Tanganyika. Hawa wapemba wana serikali yao ya mapinduzi. Warudi nchini kwao wakateuliwe na Mwinyi. Wasitegemee kubebwa na mzanzibar mwenzao (Rais Samia) kisa tu ana mamlaka ya utawala hapa Tanganyika. Umeelewa sasa?
 
Mkuu tunazunguka halafu tunarudi pale pale. Rais Samia hana uhalali kisheria kuwateua wapemba kuja kujaza nafasi za watanganyika hapa Tanganyika. Hawa wapemba wana serikali yao ya mapinduzi. Warudi nchini kwao wakateuliwe na Mwinyi. Wasitegemee kubebwa na mzanzibar mwenzao (Rais Samia) kisa tu ana mamlaka ya utawala hapa Tanganyika. Umeelewa sasa?
Wapemba wana haki ya kuishi na kufanya kazi popote ndani ya JMT, kuwa kwako inferior ni matatizo yako binafsi.

Tuliwahi kuwa na Mohamed Aboud akiwa CAG miaka ile ya Nyerere alikuwa ni mzenji na alichapa kazi vizuri tu. Wapo wengi tu wametoka huku bara na kufanya kazi huko visiwani, na hakuna lililoharibika.

Huwa mnapenda sana kuja na nyuzi za kuhamisha magoli, mlimshambulia Mbarawa kwa kazi anayoifanya pale uchukuzi na baada ya DP World kupata idhini ya kuwekeza bandarini, sasa mnahamia kwa wapemba, hamuoni kuwa mnapoteza muda wenu?.

Kusema huyu ni mpemba na huyu ni mgogo ni akili zile zile za kibaguzi tu, hazikusaidii wewe na haziisaidii Tanzania ya leo na ya kesho.

Magufuli alijaza ndugu zake wazinza, wakerewe, wanyantuzu kwenye halmashauri zote za Tanzania Bara, kila ukiingia ndani ya ofisi ni kisukuma kitupu kinachotawala, hayo hukuyaona na kuyaanzishia uzi?. Acheni kuendekeza roho ndogo za kibaguzi.
 
Tulizoea kuona wazaznzibar (maarufu kwa jina la wapemba) wametapakaa kila mahali hapa Tanganyika wakifanya biashara na shughuli nyingine za kiuchumi. Hili kama watanganyika hatuna shida nalo. Hawa ni wajasiriamali na watafutaji kama walivyo watu wa mataifa mengine waliomo hapa nchini. Tunao wachina, wahindi, wakenya, n.k, na haijawahi kuwa shida.

Kinachoudhi na kusikitisha zaidi ni kitendo cha Rais Dr Samia kuwachukua wazanzibar (hata wasiokuwa na vigezo) na kuwapa vyeo hapa Tanganyika wakati watanganyika hawana kazi. Ukitembelea kwenye ofisi za umma utashangaa kuona utitiri wa wazanzibar wakiwa wamepewa nyadhfa mbali kama vile wakurugenzi, DAS, RAS, wakuu wa mashirika ya umma, wenyeviti wa bodi mbalimbali, n.k. Rais anafanya haya yote kwa makusudi na kwa lazima huku akiwaacha watanganyika wakipuyanga bila kazi. Huu ni zaidi ya uhujumu uchumi.

Ndugu wanaJF na wananchi kwa ujumla, tuhuma hizi hazijaanza leo. Soma baadhi ya nyuzi zilizowahi kuwekwa humu kulalamikia upendeleo unaofanywa na mamlaka kwenye teuzi mbalimbali:

1. Teuzi za Rais Samia zina upendeleo?

2. Teuzi za Rais Samia kulikoni?

3. Wafahamu Wajumbe wa Bodi ya TCRA iliyovunjwa

Kelele za watanganyika kukosa kazi baada ya kuhitimu zipo dhahiri. Hata humu JF siku za karibuni kumekuwa na nyuzi nyingi zinazoonyesha wasomi wa Tanganyika kuhitimu vyuo vikuu na kuishia kufanya kazi za ovyo ovyo wakati kazi walizostahili kufanya zinagawiwa ovyo kwa wazanzibar. Nyuzi zifuatazo ni sehemu ya ushahidi huo:

1. Nimekutana na Degree Graduate wa HR kutoka Mzumbe anauza Pub

2. Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

3. Graduates wengi tunapitia wakati mgumu sana, sema jamii inaona kama hatujielewi

MAONI YANGU
Idadi ya watu wa Zanzibar (Pemba, Unguja na visiwa vingine) haipindukii milioni moja. Tanganyika ina idadi ya zaidi ya watu milioni 64. Sasa iweje Zanzibar yenye watu wachache kiasi hiki wananchi wake wapewe kipaumbele huku watanganyika walio wengi wanaendelea kusaga meno?

Ifike mahali katiba itamke bayana idadi ya nafasi wanazostahili wazanzibar (kwa kufuata uwiano wa idadi ya watu) badala ya kufanya teuzi kibubu na kusababisha malalamiko. Na tunapendekeza hili jambo liingizwe kwenye katiba mpya kabisa ili kukata mzizi wa fitna.

Nawasilisha.
Huyu mama ni mbaguzi wa kupindukia
 
Kwani tatizo liko wapi? Kwani walipelekwa znz?
Kama hamna tutulie tuwaache waliochaguliwa wapige kazi. Mzenji akiwa bosi sehemu kuna ubaya gani? Pemba sio sehemu ya JMT?.

Tunakuwa na roho mbaya za kijinga sana sisi watu wa huku bara, eneo la kilomita za mraba laki tisa tunaingia wivu na hasira eti kwa sababu ya wazenji wenye eneo linalolingana na wilaya moja ya mkoa wa Morogoro!.
 
Magufuli alijaza ndugu zake wazinza, wakerewe, wanyantuzu kwenye halmashauri zote za Tanzania Bara, kila ukiingia ndani ya ofisi ni kisukuma kitupu kinachotawala, hayo hukuyaona na kuyaanzishia uzi?. Acheni kuendekeza roho ndogo za kibaguzi.
Kwa hiyo wewe unatamani kuona ubaguzi (na nepotism) alioanzisha Magufuli unaendelea au unataka tuukemee na kuutokomeza?
 
Kama hamna tutulie tuwaache waliochaguliwa wapige kazi. Mzenji akiwa bosi sehemu kuna ubaya gani? Pemba sio sehemu ya JMT?.

Tunakuwa na roho mbaya za kijinga sana sisi watu wa huku bara, eneo la kilomita za mraba laki tisa tunaingia wivu na hasira eti kwa sababu ya wazenji wenye eneo linalolingana na wilaya moja ya mkoa wa Morogoro!.
Mkuu, bado hujaelewa somo. Hapa tunaongelea ukiukaji wa sheria wa Rais Samia kwa kututeulia wapemba waje kuwa DAS, RAS, nk hapa Tanganyika wakati sheria hairuhusu. Na wakati huo huo, tambua kwamba kuna vijana wengi wa Tanganyika wamehitimu vyuoni hawana kazi ilhali kazi zao zinagawiwa kwa wapemba kama pipi.
 
Kwa hiyo wewe unatamani kuona ubaguzi (na nepotism) alioanzisha Magufuli unaendelea au unataka tuukemee na kuutokomeza?
Tanzania sio ya kuongelea nepotism, kuna ardhi kubwa mno hatujaigusa tangu tupate uhuru, kuna maelfu ya fursa bado hayajafanyiwa kazi.

Ukimsakama SSH atakuja Mpango kutoka Kigoma na serikali nzima itajaa waha watupu.

Atakuja Mwigulu kutoka Singida na serikali nzima itajaa jamaa wa kinyiramba na kinyaturu, haya ni matatizo ya kiafrika ya miaka yote yapo katika nchi zote za bara hili.
 
Back
Top Bottom