Rais Samia atengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Raphael Chegeni

Rais Samia atengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Raphael Chegeni

Jamani huyu mzee kapata kazi ya mkataba wa miaka 5 nchi moja wapo bara la Asia toka shirika la UN anaenda kusimamia maswala ya fedha japo siyo ndo atakuwa mkuu,

Jaribu kutafakari unaweza acha kazi ambayo ushasaini mkataba kisa kazi ya kuteuliwa ambayo hujui hatma yako

Mzee alimuandikia mama barua na maelezo ya kutosha mama kamuelewa kateua mwingine

Kesho mniite mbwa kama mama asiposema ameombwa
Sawa ZOMBIE
 
Yaah CGP kuwa Mkuu wa Mkoa ni demotion tu
Akiwa CGP alikuwa anasimamia magereza na miradi yao nchi nzima, ndo ana manage mafungu yote ya Magereza sasa leo kuwa RC ni kwamba kashuka sana
Dah!...
 
Mama Samia ukiona Jina la Chegeni uchaguzi 2025 akigombea ubunge piga chini usirudishe
 
Kwanini hawezi kupewa?
Hizo ni nafasi za kitaalam aka watumishi wa serilikali yaani wale waliojariwa / wapo kwenye utumishi wa umma, tofauti na ukuu wa mkoa, wilaya na zingine zinazofanana na hizo ambazo mimi na wewe tunaweza tukapewa
 
acha ufyatu eti anapigiwa salute na wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama.
shule yako darasa la ngapi kwanza nisije nikakutendea dhambi kumbe std seven nikamkosea Mungu

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
Alichosema ni sahihi, labda tu chumvi alizoongeza. Mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa wanapigiwa saluti japo sio lazima.
 
nawashangaa wanao shangaa Rais kufanya mabadiliko...hilo ni jambo la kawaida kabisaaa na siajabu hata kesho trh 1 Siku ya kuapishwa wapo watakao tenguliwa.

hakuna jambo la ajabu hapa......
Marekani iliwahi kumteua waziri wa mambo ya nje lkn kabla hajaapishwa akatenguliwa,
mifano ipo kibao ktk mataifa mbalimbali duniani.
Unaleta stori za kishamba hapa ukidhani wewe ni mwerevu zaidi?
haya, tueleze huyo waziri wa kimarekani aliyewahi kuteuliwa na akatenguliwa ni nani na sababu zake zilikuwa zipi?

Kwa sababu mambo ya kipuuzi kama hayo usidhani yanafanyika kwingine kama ilivyo hapa.

Huyo waziri atakuwa kapitia bungeni, siyo kama hapa.

Acha ujinga wako.
 
nawashangaa wanao shangaa Rais kufanya mabadiliko...hilo ni jambo la kawaida kabisaaa na siajabu hata kesho trh 1 Siku ya kuapishwa wapo watakao tenguliwa.
wewe acha kuleta taharuki kwa wateule wapya chief Hangaya .....utasababisha wasilale usingizi this ninght ......
 
Rafiki yangu Mzee naona kawa demoted, ila ilikuwa ni dharau kwa jeshi la Magereza kuendeshwa na mtu kutoka JWTZ, Hayati Magufuli alikuwa ana maamuzi ya kipekee mno 😃

Kamishina wa Magereza ameondelewa naona mama anapanga safu yake vizuri kabisa, ndani ya miezi miwili hii huwenda wakuu wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama waliobaki wakaondolewa rasmi.
Wenye uhakika wa kuendeleza ni Diwani na Makakala wa Uhamiaji
 
Chegeni ana dharau mno hujiona yeye ndio yeye hataki ukuu wa mkoa anataka ubunge kamuulize Lowasa kilichomkuta baada ya kumdharau Kikwete Mwenyekiti CCM taifa akigombea uraisi aweza pita kura maini kugombea Uraisi CCM kuwa ana support kubwa!
Hata sielewi unachoeleza hapa ni kitu gani, na kinahusiana vipi na niliyoandika na wewe kuyajibu!

Kateuliwa kwa sifa zipi; na katenguliwa kwa sabau ya "dharau"?

Huo mfano wa Lowassa na Kikwete, hicho ndio kipimo cha utendaji kazi na taratibu za kupata viongozi?

Mbona nchi hii inakuwa ya kijinga jinga kiasi hiki?
 
Alikuwa boss wa magereza nchi nzima.Ukuu kamkoa kamoja. Kashushwa.
Sio Mara ya Kwanza Rais kufanya hivi rejea Meja Jenerali Mbuge Alikuwa Mkuu wa JKT akapelekwa RC Kagera, Kuna yule CP Andengenye Alikuwa CGF_Zimamoto akazingua baadae akaja kuwa RC Kigoma hadi Sasa


Kwa Mamlaka ameshuka sana, Kiutaratibu stahil zake atapata Kama alivyokuwa MT!!

Mama katoa mtu sahihi sehemu sahihi kapelekwa mtu sahihi sehemu isiyo sahihi kabisa!!


Jamaa kafanya mabadiliko na maendeleo makubwa sana ndani ya Jeshi la Magereza kwa kipindi kichache Sana!!
 
Siku chache baada ya Wakuu wa Mikoa wapya 9 kuteuliwa, Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Dkt. Raphael Masunga Chegeni

Amemteua Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, na ataapishwa na Wateule wengine kesho (Agosti 01, 2022)

Kabla ya uteuzi wa Rais, Meja Jenerali Mzee alikuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP)

View attachment 2310242

View attachment 2310215
Kwa mizania ya kawaida tu, huu uteuzi wa Major General kuwa Mkuu wa Mkoa sijauelewa kabisa.Tena huyu Major General alikuwa Mkuu wa Magereza.
Mizania haiko sawa, Major General na Mkuu wa Magereza yuko too senior kuwa Mkuu wa Mkoa.
Wajuvi hebu mnieleweshe hapa!
 
Kwa mizania ya kawaida tu, huu uteuzi wa Major General kuwa Mkuu wa Mkoa sijauelewa kabisa.Tena huyu Major General alikuwa Mkuu wa Magereza.
Mizania haiko sawa, Major General na Mkuu wa Magereza yuko too senior kuwa Mkuu wa Mkoa.
Wajuvi hanu mnieleweshe hapa!
Umri wa kustaafu umefika unataka aendelee kuwa major generali?
 
Back
Top Bottom