Kodi!Hazina wamezipata wapi hizo pesa?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kodi!Hazina wamezipata wapi hizo pesa?
Serikali haina dini ila watu wake wana dini.Tanzania ni nchi inayoongozwa na serikali isiyo na dini. Ikiwa kila mwenye taasisi yake ya dini atataka apewe fedha hii na rais, rais ataweza kutoa hela sawa kwa wote?
Kwa nini serikali inajiingiza kwenye mamo ya kufadhili makanisa,wakati kuna kazi nyingi za serikali zinahitaji pesa?
Rais Nyerere alijitambulisha kama Mkatoliki. Alipokuwa Dar es salaam, kila siku asubuhi alikuwa akisali kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay. Tuliokaa Oysterbay tulimuona. Si Jumapili tu, kila siku.Endelea kuweka neno mkuu.
Kodi!
Ni wazi hielewi dhana ya utenganisho wa dini na serikali/siasa.Iyoo Mill 100 ni sadaka ya misa ya wototo broo katolik tupo another level
Sasa kama ni hivyo, unataka kusema rais atatoa hela zake binafsi na si za serikali?Serikali haina dini ila watu wake wana dini.
Saa 100 ni mfano wa rahisi asiyependa kuumiza kichwa kabisa na anaona njia ya rahisi yeye kujipatia ummarufu ni hiyo ya kugawa psa za wananchi hivyo hovyo Laiti kama angekuwa na uwezo wa kuzitafuta angeziheshimuHii si sawa,
Halafu rais ni nini maana Rais ni ofisi.... maana yake ni fedha za umma zile.
Ndio maana hata afya yake na ulinzi wake ni sisi wananchi tunawajibika.
Kwa nini wasifanye mambo ambayo ni ya msingi kama umeme na maji.... na elimu badala ya hizi takrima ndogondogo
🙏Hakika.
Politics...Tanzania ni nchi inayoongozwa na serikali isiyo na dini. Ikiwa kila mwenye taasisi yake ya dini atataka apewe fedha hii na rais, rais ataweza kutoa hela sawa kwa wote?
Kwa nini serikali inajiingiza kwenye mamo ya kufadhili makanisa,wakati kuna kazi nyingi za serikali zinahitaji pesa?
Maelewano gani kwani kulikuwa na kutoelewana kati ya Rais Samia na kanisa? Kupinga uuzwaji wa bandari haikumaanisha ugomvi wa kanisa na raisiRais Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya zoezi la kutabaruku Kanisa Katoliki Parokia ya Roho Mtakatifu, Babati mkoani Manyara ikiwa ni mchango wake kwa kanisa hilo.
Kwa niaba ya Rais, Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango ametoa kauli hiyo katika Misa Maalum ya kumwombea Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Nyerere.
Hii ina ashiria Amani na Nuru ya maelewano baina ya Serikali Ya Dr. Samia na Kanisa Katoliki, na hii ni baada ya miezi iliyopita Baraza la Maaskofu la Kanisa hilo Kutoa Waraka uliokuwa unapinga mkataba wa Serikali.
Binafsi nasema kila la Kheri, Mungu alisimamie Taifa letu la Tanzania.
Mpenzi wangu FaizaFoxy nitambatiza na kumpa jina la kikristo wakati wa ufunguzi wa hilo kanisa….! Naomba mmuchagulie jina 😂😂😂😂
Kanisa liikatae hii cheap bribe.Sasa kama ni hivyo, unataka kusema rais atatoa hela zake binafsi na si za serikali?
Kanisa huwa halikatai hata pesa za majambazi, zote zinaombewa tu.Kanisa liikatae hii cheap bribe.
Mgema ukimsifia sana pombe huitia maji.Rais Nyerere alijitambulisha kama Mkatoliki. Alipokuwa Dar es salaam, kila siku asubuhi alikuwa akisali kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay. Tuliokaa Oysterbay tulimuona. Si Jumapili tu, kila siku.
Alipewa shutuma kwamba anapendelea Wakatoliki.
Akasema serikali yake hata haijui mawaziri ni wa madhehebu gani, anajua tu wanavyoapa wanatumia kitabu gani. Alisema serikali haina haja ya kujihusisha na mambo ya dini. Alisema hata kwenye kuhesabu watu, serikali haikusanyi idadi ya watu gani ni wa dini gani, na kama mtu anatafuta habari hizo, aende kwenye taasisi za dini.
Nyerere hakuwahi kutoa hela za serikali hivi kwenye taasisi za dini, kwa sababu alielewa mipaka ya serikali na dini.
Nyerere hakuwahi hata kupanda mbele kwenye altare kanisani kusema neno kanisani kama rais.
Rais Mkapa naye alikuwa anakwenda kanisa la St. Immaculata Upanga, hakuwahi hata kupanda madhabahuni kutoa neno kama rais. Alielewa mipaka ya serikali na dini, separation of church and state/ religion.
Sasa hawa viongozi wetu wa sasa wanaosema wanamuenzi Nyerere, mbona tunawaona wanaondoka kwenye misingi ya Nyerere ya kukataa kuchanganya mambo ya serikali na dini?
Mimi, wewe na yule!Kodi kalipa nani?
Alikuwemo kanisani.Rais yupi wakati taarifa inasema kawakilishwa na makamu!
Maajabu haya! "Kwa niaba ya Rais, Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango ametoa kauli hiyo katika Misa Maalum ya kumwombea Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Nyerere."
Kwahiyo hiyo milioni 100 katoa nani?Mimi, wewe na yule!
Ni kutoka kwenye perdiem zakeNaomba niwekwe sawa.
Hizo fedha anatoa mfukoni kwake au ni za serikali?