Rais Samia atua Tanzania, aongelea mafanikio ya safari yake Marekani

Kabla ya covid walikua wanakuja wangapi hiyo high season!?...ili tujue Kama royal tour imetulipa
Bado Tanzania hatupo vizurina ndio wasiwasi wa wengi ulipo.
Wenzetu wakitaka kuja huwa wanaangalia trevel advisory. Nchi yao inasema nn kuhusu nchi unayotaka kwenda
Kwa sasa hatupo vizuri kabisa na ndio maana idadi ya wanaokuja ni ndogo
 
Asante sana Mama, Pole kwa safari, na karibu sana Nyumbani Tanzania.

Nina machache
======
Tunaangalia uwezekano wa kuwa na ndege zitakazotoka moja kwa moja Dallas mpaka Tanzania kuleta wageni
Dreamliner yetu haiwezi kweli kufanya safari hizi?
Aidha, Rais Samia amesema akiwa ziarani amezungumza na Serikali ya Marekani na kunyoosha pale palipokuwa na changamoto, akisema "Sasa tupo vizuri, tunaenda nao vizuri sana"
Wapi palikuwa pamepinda, palipindapindaje na kusababisha changamoto, nani alipapindisha 'tumsonte kidole', mmepanyooshaje kiasi kwamba hatuna tena changamoto ya kupinda?

Rais Samia: Kuna kundi lilienda kufanya Mkutano na Meya wa Jiji la Dallas, na matokeo ya Mkutano ule ni kwamba wenzetu wamekubali na wana hamu wafanye undugu na Miji yetu
Watanzania tutanufaikaje na udugu wa jiji la Dallas na miji yetu, na hao Dallas watanufaikaje?
+++++
Mama haya maswali yakijibiwa na wasaidizi wako (wasiwe wale wanaojifanya wanakusemea, siku hizi wanaitwa jina sipendi kulitumia) walioko humu JF litakuwa jambo zuri sana.
====
Kwa mara nyingine Karibu sana nyumbani Mama yetu Mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. Na kazi iendelee.
 
Nimeuliza high season huja wangapi kabla ya covid,we unaniletea tangazo la tahadhari,we vipi!!?...sema huja wangapi ili wakipungua high season hii tuone kuwa royal tour haijalipa,hapo hatukulenga ilipe ghafla
 
Nimeuliza high season huja wangapi kabla ya covid,we unaniletea tangazo la tahadhari,we vipi!!?...sema huja wangapi ili wakipungua high season hii tuone kuwa royal tour haijalipa,hapo hatukulenga ilipe ghafla
Maswali muhimu haya. Royo tua ni biashara, tupange mahesabu mapema.
 
Ni sekta ipi inayoingizia nchi fedha nyingi ikiwa utalii ni pety!?...
Watalii Kuna au kutokuja sio sababu ya royal tour.
Watalii wengi wanaokuja huwa hawapendi kurudi tena Tanzania. Sababu zinazofanya wasirudi ndio tunapaswa kushughulika nazo.
Pili bado Tanzania hatupo kwenye nafasi nzuri ya kiusalama kwa watalii na ndio maana hawaji wengi. US wametuweka kwenye kundi la hatari
 
Nimeuliza high season huja wangapi kabla ya covid,we unaniletea tangazo la tahadhari,we vipi!!?...sema huja wangapi ili wakipungua high season hii tuone kuwa royal tour haijalipa,hapo hatukulenga ilipe ghafla
Royal tour hadi sasa haina impact kwa kuwa ndio imezinduliwa, na wao kuja kwao hakutegemi royal tour Bali usalama wao.

Somalia hata wazindue royal tour kila siku, watu hawataenda kwa kuwa hakuna usalama
 
Wewe ni mpuuzi tu usiyejua lolote,baada ya jakaya kuendesha kampeni ya kutangaza utalii ikiwemo kwenye ligi kuu ya uingereza,ghafla watalii wakifika milioni na kuwa sekta inayoingizia nchi pesa nyingi za kigeni,royal tour ni tangazo la biashara ya utalii wa Tanzania,siyo filamu Kama bongo movie
 
Tukitaka kujua mchango wake kupitia muvi turudi kwenye takwimu za watalii nchini let say za miaka mitatu iliyopita na kutoka sasa mpaka miaka mitatu ijayo ama mitano kama namba itaongezeka
 
Mbona hiyo hela ya utengenezaji wa hiyo Movie kila siku ni habr mpya mpya tunafichwa nini?

Jibu Rahisi ni kwamba TUMEPIGWA!

Happ Kuna uongo. Maana wafanyabiashara wa ndani na wa nje wamechangia billion 7 kwa ajili ya filamu. Return s kwao Ni Nini?. Maana mfanyabiashara hatoi pesa bure.
 
Nimeuliza high season huja wangapi kabla ya covid,we unaniletea tangazo la tahadhari,we vipi!!?...sema huja wangapi ili wakipungua high season hii tuone kuwa royal tour haijalipa,hapo hatukulenga ilipe ghafla
Maswali muhimu haya. Royo tua ni biashara, tupange mahesabu mapema.
 
Kampeni ya kutangaza utalii ilikua mwaka gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…