Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Huwezi kupendwa na wote na huwezi kuchukiwa na wote !! That's life !!
Matendo yako yakiwa mazuri utaendelea kusiwa hata kama ulishakufa,lakini kama matendo yako yalikuwa mabaya utaendelea kubezwa hata kama ulishakufa.

Kumbuka Nyerere,Karume,Sokoine,Mandela,Kaunda,Nkrumah,Samora hao bado wanaimbwa kama mashujaa wa Afrika,lakini Idd Amin,Mabuto,Chiluba,Magufuri matendo yao yataendelea kuwahukumu.
 
Kwa kweli tukisema muacheni Mh Hayati Magufuli apumzike mahali aliko tunashambuliwa eti sisi ni sukuma geg! Jaman marehemu kwa heshima za Afrika huwa tunamwacha apumzike aliko kuliko kumsemea vibaya vibaya.

Leo nimesikia Mh Raisi akisema utawala wa awamu ya Tano ulitengeneza nidhamu ya uwoga kwa watumishi, kwa sababu ulikuwa ni Simba, alikuwa ukizingua anakungata ngwadu!

Sasa kwa Nini ustekeleze unavyotaka. Paspo kumsem mwenda zake?
Kwani kasema uongo?
 
Haya mambo yanasikitisha sana ila Pumzika kwa amani JPM, najua utakumbukwa kwa mengi mazuri.
 

"Tunasifiwa kwamba adjustments [maboresho] tuliyoyafanya awamu ya tano kidogo zimekuza heshima ndani ya utumishi wa umma.

“Heshima iliyokuzwa ni ya woga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ambaye alikuwa ukimgusa sharubu anakurarua. Lakini hata hivyo hatukukua kivile, heshima inayotakiwa iwe ya moyoni, kila mmoja aheshimu mstari wa mwenzie, hicho ndicho tunachokosa Serikalini.

“Kila siku unasikia Waziri kakwaruzana na Katibu…upande wetu tunaenda kuimarisha Chuo cha Utumishi na Chuo cha Uongozi ili kufundisha watu majukumu ya utumishi wa umma, lakini Baraza la Maadili likisimama kwenye sheria na kurekebisha maadili ya watenda kazi wa Tanzania, tutaenda vizuri,"- Rais Samia Suluhu akiwaapisha viongozi watule leo Aprili 2, 2022, Chamwino Ikulu, Dodoma

---

Hakika kila chenye mwanzo lazima kiwe na mwisho.

Kumbe zile sifa za ooo nchi imerudisha heshima kwenye sehemu za kazi ilikuwa ni nidhamu ya uoga tu.

Magufuli alikuwa anawatishia watu na wakawa wanaonyesha heshima ya uoga.
Kwa mtu ambaye anapenda na kuzingatia siasa za kistaarabu, haki, kiutu na maelewano, atauelewa kwa urahisi sana mtizamo wa kiungozi wa Rais SSH. Lakini wale kwangu pakavu tia mchuzi bado vichwani mwao wamebakia na kumbukumbu za siasa za kiharamia za awamu iliyopita.

Wakati msimamo wa Madam President ni kurithi na kuyaendeleza mazuri yote ya awamu zilizopita, baadhi ya wanufaika wa awamu iliyopita wanatamani ayaendeleze na mabaya yake pia.

Toka mwaka 2016 walijawa na dhihaka, majivuno na kejeli nyingi pale Watanzania wenzao walipipitia katika madhila makubwa. Waliwabeza na kuwasimanga, huku wakisema kila zama ina msahafu wake.

Wamekuwa wepesi wa kusahau na wagumu wa kuelewa zama zimebadilika ijapokuwa zilikuwa ni fupi ama zilifupishwa. Ni dhahiri sasa ni kuwa ukishindwa kukabiliana ama kupambana nao, ni vyema ukaungana nao.

Mwenye akili na busara anamuelewa sana Madam President, wewe ni nani ambaye huoni aibu ya kulazimisha vitu vilivyopuuzwa, kusahaulika na kutupiliwa mbali!?
 
Watu wanatafsiri vibaya sana ile kauli. Mbona iko sawa yeye alikuwa makamu wa Rais alikuwa anawaona watumishi walivyokuwa waoga badala ya kuwa na ufanisi. Uoga huondoa ufanisi na hufinya madhaifu ambayo yalipaswa kusemwa na kurekebishwa.
Tulifikia hatu ya kufunga akaunti za watu hovyo, yaani hata deni la Laki 5 mtu anafungiwa akaunti yake. Haikuwa nidhamu bali ulikuwa uoga.
Kwa hiyo sasa wana ufanisi?

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Huyu ni ndumilakuwili,mbona aku step down

Tuseme tu ukweli umejaribu kwenda kwenye taasisi za serikali ukaona huduma zao zikoje ukifananisha na simba wa chato huduma ilikuaje.
Anatikisa tu wezere lake hana lolote
 

"Tunasifiwa kwamba adjustments [maboresho] tuliyoyafanya awamu ya tano kidogo zimekuza heshima ndani ya utumishi wa umma.

“Heshima iliyokuzwa ni ya woga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ambaye alikuwa ukimgusa sharubu anakurarua. Lakini hata hivyo hatukukua kivile, heshima inayotakiwa iwe ya moyoni, kila mmoja aheshimu mstari wa mwenzie, hicho ndicho tunachokosa Serikalini.

“Kila siku unasikia Waziri kakwaruzana na Katibu…upande wetu tunaenda kuimarisha Chuo cha Utumishi na Chuo cha Uongozi ili kufundisha watu majukumu ya utumishi wa umma, lakini Baraza la Maadili likisimama kwenye sheria na kurekebisha maadili ya watenda kazi wa Tanzania, tutaenda vizuri,"- Rais Samia Suluhu akiwaapisha viongozi watule leo Aprili 2, 2022, Chamwino Ikulu, Dodoma

---

Hakika kila chenye mwanzo lazima kiwe na mwisho.

Kumbe zile sifa za ooo nchi imerudisha heshima kwenye sehemu za kazi ilikuwa ni nidhamu ya uoga tu.

Magufuli alikuwa anawatishia watu na wakawa wanaonyesha heshima ya uoga.
SIMBA WA YUDA NI YESU, jamani, acheni kufananisha na Magufuli.
 
Hata iweje hakutakiwa kumuongelea kihivi, kwa sababu Wananchi wengi akili zimefunguka kupitia awamu ya 5. Inashangaza ila inasikitisha sana kiongozi wetu kumtamka aliyekuwa yeye msaidizi. Wanafikiri watanzania ni wale wa kabla ya JPM

Duh!
Anafikiri kwa kusema mabaya ya mzee kutafanya wananchi wasione mazuri aliyoyafanya,
 
Huduma kwa sasa ni mbovu , lakini ndo hiyo nidhamu ya uwoga . Watumishi wali comply kwa kumuogopa mr tumbua tumbua.
Katika maisha ogopa sana kuishi maisha ya wewe kuogopwa , utazungukwa na watu wanafiki kupitiliza na watafurahia anguko lako muda wowote.
Hata kwenye familia zetu , nyumba zenye wazazi wakali mara nyingi ndo huzalisha machangudoa na mateja
Basi hujui kuongoza kama hutaki kuogopywa. Hakuna kiongozi mzuri asiyeogopwa, na iwapo una kiongozi wa namna hiyo basi hatekelezi majukumu yake. Hata dini zinatufundisha kumuogopa Mungu anayetuongoza.
 
Sio vizuri kumsema marehemu coz hawezi kujitetea, ila moyo wa mtu kichaka
 
Kwa mtu ambaye anapenda na kuzingatia siasa za kistaarabu, haki, kiutu na maelewano, atauelewa kwa urahisi sana mtizamo wa kiungozi wa Rais SSH. Lakini wale kwangu pakavu tia mchuzi bado vichwani mwao wamebakia na kumbukumbu za siasa za kiharamia za awamu iliyopita.

Wakati msimamo wa Madam President ni kurithi na kuyaendeleza mazuri yote ya awamu zilizopita, baadhi ya wanufaika wa awamu iliyopita wanatamani ayaendeleze na mabaya yake pia.

Toka mwaka 2016 walijawa na dhihaka, majivuno na kejeli nyingi pale Watanzania wenzao walipipitia katika madhila makubwa. Waliwabeza na kuwasimanga, huku wakisema kila zama ina msahafu wake.

Wamekuwa wepesi wa kusahau na wagumu wa kuelewa zama zimebadilika ijapokuwa zilikuwa ni fupi ama zilifupishwa. Ni dhahiri sasa ni kuwa ukishindwa kukabiliana ama kupambana nao, ni vyema ukaungana nao.

Mwenye akili na busara anamuelewa sana Madam President, wewe ni nani ambaye huoni aibu ya kulazimisha vitu vilivyopuuzwa, kusahaulika na kutupiliwa mbali!?
Kundi lote la sukuma gang wameishiwa pumzi sasa kazi yao ni kutukana tu.
 
Back
Top Bottom