Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

Muhimu wangepewa stahiki zao waondoke lakini sio kufanya walichofanya, kwanza itakuwa walipewa kazi kwa kubebana/kujuana wakawaacha wenye sifa waliostahili kazi hiyo hii ni dhambi hata kwa Mungu.

Hao jamaa ni wahalifu na walistahili kufikishwa mahakamani kwa uhalifu wao lakini sio kupewa nafasi wakasome wakati wapo waliokwisha soma na hawana ajira wanahangaika mitaani.
Acha roho mbaya ndugu yangu.
 
Kwahiyo kughushi cheti si kosa kisheria au sijaelewa vzr.

Kutoboa Mwafrika haitakaa itokee.

Kwamba umeghushi umekatwa halafu serikali inakupongeza.

Sasa yule aliyekuwa anatibu watu isivyo kiutaratibu yeye ana mkosi.

Ni kama tunaenda na pweza wa utabiri
Mkuu suala hili no complex ,tumshukuru tu Mama kwa Hilo ,hapoilipo umehudumiwa na watu wengi Sana was Aina hiyo!inawezekana hata aliy3msaidiaa mama yako kujifungua. Alikiwa na Vyeti Feki!
Acha walipwe Manisha yaendelee!
 
Kuwarudisha kazini ni kuwakatili vijana walioko mitaani bila ajira ambao wamehitimu kwa mujibu wa sheria, na pia kuhamasisha uvunjaji sheria kwenye sekta ya elimu(kugushi).

Kuwasaidia, wangewalipa mafao yao yawe kama mtaji wa kujiajiri ili vijana ambao hawana mtaji wala ajira wachukue hizo nafasi zao.
Hapo wangeua ndege wawili kwa jiwe moja.
 
Kuwarudisha kazini ni kuwakatili vijana walioko mitaani bila ajira ambao wamehitimu kwa mujibu wa sheria, na pia kuhamasisha uvunjaji sheria kwenye sekta ya elimu(kugushi).

Kuwasaidia wangewalipa mafao yao yawe kama mtaji wa kujiajiri ili vijana ambao hawana mtaji wala ajira wachukue hizo nafasi zao.
Hapo wangeua ndege wawili kwa jiwe moja.
Rais ndiye mkuu wa utumishi nchini na ana mamlaka ya kuajiri yeyote anayemtaka

Kama hilo hutaki nenda kadai katiba mpya ili imuondolee rais mamlaka hayo
 
Kwahiyo kughushi cheti si kosa kisheria au sijaelewa vzr.

Kutoboa Mwafrika haitakaa itokee.

Kwamba umeghushi umekatwa halafu serikali inakupongeza.

Sasa yule aliyekuwa anatibu watu isivyo kiutaratibu yeye ana mkosi.

Ni kama tunaenda na pweza wa utabiri
Hata kama kughushi cheti ni kosa kisheria, DPP ana mamlaka ya kuipeleka kesi mahakamani au hata kutoipeleka. Au hata akiipekeka ana mamlaka ya kuachana nayo akiamua. na DPP ni mteule wa rais

Kama hupendi mfumo huo wa ssa wenye loopholes nyingi kwenye kutekeleza sheria ungana na wanaodai katiba mpya ili hilo liwezekane
 
Muhimu wangepewa stahiki zao waondoke lakini sio kufanya walichofanya, kwanza itakuwa walipewa kazi kwa kubebana/kujuana wakawaacha wenye sifa waliostahili kazi hiyo hii ni dhambi hata kwa Mungu.

Hao jamaa ni wahalifu na walistahili kufikishwa mahakamani kwa uhalifu wao lakini sio kupewa nafasi wakasome wakati wapo waliokwisha soma na hawana ajira wanahangaika mitaani.
Magufuli angekuwa hai angekuuliza utamlipaje stahiki mtu aliyeidanganya serikali na kujipatia ajira na mshahara kiudanganyifu?

Kama unataka kutekeleza sheria basi inabidi uwe bandidu kotekote yaani, hakuna mafao wala kurudishwa kazini.

Ila wewe ukiona bora alipwe mafao tu, mwingine ansona bora arudi kazini tu

Ni mtizamo tu wa kila mmoja
 
Kuwarudisha kazini ni kuwakatili vijana walioko mitaani bila ajira ambao wamehitimu kwa mujibu wa sheria, na pia kuhamasisha uvunjaji sheria kwenye sekta ya elimu(kugushi).

Kuwasaidia, wangewalipa mafao yao yawe kama mtaji wa kujiajiri ili vijana ambao hawana mtaji wala ajira wachukue hizo nafasi zao.
Hapo wangeua ndege wawili kwa jiwe moja.

Kama una umri angalau miaka 45 utaelewa kuwa mfumo wa zamani wa ajira ulichukua drs la saba wengine mpaka darasa la nne.

Baadae wakawalazimisha waendelee na hapo sasa mtu ana miaka 40 hawezi kwenda shule kumkariri grasshoper na matundu yake ndo mambo ya kununua majina, kufoji n.k yakaingia.

Lile tukio ilikuwa ni kubana matumizi ya serikali, inawezekana hata yeye hakupenda ila alilazimika ndo maana hapakuwa na mpango wa replacement kuziba nafasi.

walipowaondoa maofisini waliobaki walijiongeza wakiendelea kuwasiliana na waliofukuzwa wakitafuta ushauri wa nini wafanye wapi na kwanini.

Ukiachana na udaktari, hizi field nyingine nyingi experience ni kila kitu kwenye kazi. Huwezi ondoa mtu ana experience ya 20 years or more kazini eti ana cheti feki halafu umlete graduates hapo afanye kazi zake. Ndo maana jeshi halikuguswa. Huwezi mtoa mhasibu mkuu wa kikosi ulete graduate afanye kazi zake.

Kuna watumishi walioitumikia hii nchi kama tutabadilishana na graduates watahitajika graduates 20 kujaribu kuufikia utendaji wa mtu mmoja na hawatoufikia.

Kwa sasa serikali idhibiti mfumo wa ajira wanaostaafu wawapishe wenye elimu sahihi ila kuwaondoa lilikuwa kosa.
 
Inaonyesha mambo mengi labda alikua hakubaliani nayo, alikua anatetea ugali wake, who will blame her?
Nje ya siasa, hakuwa na taaluma nyingine? Kama huwezi kusimamia haki kwenye level ya chini, unaweza kusimamia haki ukipewa mamlaka yote ya nchi? Kulikuwa na madhara gani kutoka siasani kwa ground za kutokukubaliana na uonevu na udhalimu unaofanywa, au hata uvunijfu wa sheria?

Wanasema, kutokujua sheria hakukuondolei kosa! Anakubali kuwa watumishi hao wameghushi nyaraka za serikali?

Ni lini imehalalishwa kughushi nyaraka za serikali?

Kati ya watumishi 4000 waliofukuzwa, wangapi wamefungua kesi kudai kuonewa? Ziwe zimesikilizwa au hazikusikilizwa, ngapi zimesajiliwa?

Tuishie kusema, TAKUKURU na POLISI hawatoshi, hawana meno. Genge la mahamakama na wanasheria ni wachumia tumbo kama aliyelinda ugali wake!

Nitaamini kuwa HAKI imetendeka/inatendeka ikiwa Seth, Rugemalira, Maimu na wapigaji wengine wakifungua kesi dhidi ya serikali kwa udhalilishwaji waliofanyiwa, uonevu, kunyimwa uhuru na yafananayo, wadai na fidia.

Msiba amedhalilisha watu, anapaswa kulipa watu mabilioni, serikali imedhalilisha watu na wengine kufungwa bila kosa, wahanga kimya!

Bado nipo nipo sana.
 
Ninapendekeza lazima kila mtu yeyote atakyetaka kugombew nafasi yoyote kuwe na kipimo cha utimamu wa akili..

Hii nchi imechezewa sana
 
Kwahiyo kughushi cheti si kosa kisheria au sijaelewa vzr.

Kutoboa Mwafrika haitakaa itokee.

Kwamba umeghushi umekatwa halafu serikali inakupongeza.

Sasa yule aliyekuwa anatibu watu isivyo kiutaratibu yeye ana mkosi.

Ni kama tunaenda na pweza wa utabiri
Elimu yenyewe haina maana!cheti kina maana gani sasa!!kama form six leaver anaweza fundisha vizuri tu kuliko hata mhitimu wa chuo cha ualimu!!!!Hata form six failure anaweza kufunzwa udaktari tu na akawa deep tu bila kujali ufaulu wake!!?
 
Ni wazi kabisa mtu akifoji kitu official huyu ni mualifu na adhabu yake inaweza kuwa kifungo mpaka miaka7.

Hamna kitu kinasikitisha kama mtu unahangaike kusoma kwa bidii pamoja na changamoto zote unakomaa, halafu ajira aje kupewa mtu ambaye kaamua kutumia shortcut ya kufoji vyeti, hii haiko sawa.

Nilitegemea Hawa watu wawe mfano wa onyo la kughushi vyeti lakini ndio kwanza wanarudishwa kazini, ni sawa na mtu aliefungiwa account yake benki alipokamatwa akingiza noti feki ila sasa anasamehewa na zile noti feki zinahesabiwa kuwa orijino.

Vijana kibao wapo mitaani wamesoma kwa shida ili kumaliza degree / masters, kiukweli hawatendewi haki hawa vijana, Binafsi sikuwa fan wa magufuli lakini kuna mambo machache sana aliyoyafanya nilikuwa upande wake likiwemo hili swala la kuchomoa wanao ghushi vyeti,

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora imetangaza kuwarejesha kazini Wafanyakazi zaidi ya elfu nne (4000+) ambao waliondolewa kazini kutokana na kugushi vyeti katika maeneo mbalimbali lakini sasa kwa huruma ya Rais Samia watarejeshwa kazini kwa sharti la kuwa wawe wamejiendeleza kielimu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora Mohamed Mchengerwa amesema "wale walioweza kujiendeleza ambao ni zaidi ya 4100 tayari wamerejeshwa kazini, pia tunao Watumishi 1150 ambao hawakufanikiwa kujiendeleza maana yake hawana sifa za kutosha kuendelea kuitumikia Serikali japo walikua ni Watendaji wazuri”

Rais Samia alishatuagiza kwamba hawa 1150 kutokana na utendaji wao uliotukuka Watumishi hao wote walipwe haki zao na stahiki zao kama vile wapo kazini kwahiyo watalipwa"
Hongera sana mama Samia
 
Back
Top Bottom