Rais Samia bado anapotoshwa, hajapata washauri wenye weledi

Rais Samia bado anapotoshwa, hajapata washauri wenye weledi

Baada ya Rais Magufuli kufariki, Tanzania tumepoteza mwelekeo tulitegemea mama atakuwa kiongozi ila nimeshangaa nae kawa mwanasiasa anafanya maamuzi kufikiria uchaguzi wa 2025.
Chini ya Magufuli tulikuwa tunaelekea shimoni sasa hivi haieleweki tunaenda wapi ?
 
Covid-19,imesababisha uchumi wa dunia kusinyaa,kwa hiyo IMF kwa kuliona hilo, ndiyo iletenga mabillions ya dola ili kusaidiwa mataifa yenye uhitaji kupambana na COVID-19,ili mataifa hayo yarejee kwenye uzalishaji.
Mashariti ya mkopo ilikuwa kupambana na kutokomeza covid-19,(Chanjo,vifaa tiba na miundo mbinu ya afya), mataifa mengi yaliyotangulia kuchukua mkopo huu,wao walenga kutimiza sharti hili la IMF.
Lakini Tanzania, ndiyo wakajenga hoja kuwa,ili kutokomeza covid-19,ni dhana Pana,siyo kununua chanjo na vifaa tiba (mitungi ya gesi).bali linaanzia na wafunzi wa Shule za msingi na sekondari ambao,wanabanana madarasani au kukaa sakafuni,au kupanda daladala kila siku kwa ukosefu wa mabweni,Ni vema wakapata madarasa ya kutosha, madawati na mabweni na vitanda,kwa kufanya hivi,tutakuwa tunapambana na maambukizo ya covid-19.
Serikali iliona kuwa ili kupambana covid-19,inahitaji maji tiririka,kwa kwa kuwa Tanzania,miji na vijiji vingi havina maji safi,kwa hiyo walio Ni busara sehemu ya fedha hizo zielekezwe kwenye maji Safi.
Mwisho, ndiyo mapambano halisi ya covid-19,kwa kujenga vituo vya afya,magari, mitungi ya gesi, mitambo ya kupima maradhi nk.
Kwa kuwa Tanzania,ilifanyia maboresho ya mashariti ya mkopo,ilibidi Mtukufu Rais akutane na Rais wa IMF na Rais wa IMF Kanda ya Africa,kuwashawishi,na hatimae kuridhia kufanya marekebisho ya mashariti ya mkopo.

Ushauri
(1). Pamoja na IMF kuridhia maboresho ya mashariti ya mkopo Ni vema serikali,ikatimiza madhumuni ya mkopo,kutokomeza covid-19,ili dunia ianze uzalishaji
(2). serikali Ni vema ikaajiri watumishi wa kutosha kwenye hivyo vituo vya afya na hospital, watakao toa huduma hizo, vinginevyo Ni kazi bure,kuna Upungufu wa madaktari na wauuguzi,na watalaam wengine,lakini wataalaam hao wako madaktari wote watakao maliza intern waajiriwe Mara moja,Kama ilivyo kuwa mwaka 1978, wakati wa vita ya Uganda, wanafunzi ambao walikuwa JKT kwenye mafunzo na mgambo walikwenda mstari wa mbele.
(3). Serikali iwalipe posho ya majanga (risk allowance) wafanyakazi wa sekta ya afya,wanao fanya kwenye kitengo Cha magonjwa ya milipuko.


(4).Tunatahadharisha,hayo majengo na mashiñe zisije kuwa mapambo, badala ya kufanya kazi iliyokusudiwa.
 
Unahaki ya kuwa na maoni hayo ila ni vyema kufahamu kwamba maamuzi ya serikali mara nyingi hufanywa baada ya mchakato mrefu unaohushisha watu wengi. Siamini kwamba kila kitu kinafanywa kiurahisi kama mtoa mada alivyo eleza
 
S
Rais bado ananua ndege cash wakati uchumi unapumlia mashine?

Rais anakopa kujenga madarasa ambayo hayalipi Kodi Wala kulipia mikopo.

Unakopa pesa ili kununua barakoa seriously pesa za kulipa huo mkopo zitatoka wapi?

Unatakiwa kukopa kutengeneza project kubwa kama SGR na Bwawa la umeme Rufiji na miradi ya barabara na maji ambayo italeta matokeo in long-run.

Project zote za Afya na elimu zilitakiwa kuwa funded na pesa za ndani Kama tuna uwezo wa kukusanya trion 1.8+ tunakwama wapi?

Nilitegemea pesa zote za covid19 zingeelekezwa kwenye Utalii, Kununua mazao yote ya wakulima walioanguka, Kuweka ruzuku kwenye mbolea ili wakulima walime Tena, Kuanzisha project za kilimo Cha umwagiliaji ili kuwa na uhakika wa chakula, Kutafuta masoko ya mazao ya wakulima nje na kufufua viwanda na biashara zilizokufa.

Imagine mfuko wa mbolea 50kg Ni laki moja wakati gunia la mahindi Ni elfu 30 halafu unaenda kulipia cash ndege billion 500. Wakati 80% Ya watanzania wapo kwenye kilimo!!

Mama Samia bado hashauriwi vizuri ama anajishauri vibaya wengi tuliaminishwa Magufuli hashauriki kumbe hata washauri hakuna Kuna watu wa kujikomba kwa watawala tu.
Samahani mkuu hivi za madarasa sio zile za matozo Tena??? Eeeh eeeh!
 
Back
Top Bottom