Rais Samia: Bodaboda ni watoto wangu nitakwenda nao 2025

Rais Samia: Bodaboda ni watoto wangu nitakwenda nao 2025

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema anatambua kundi la vijana waliojiajiri kupitia bodaboda na yuko tayari kwenda nao mpaka 2025. Rais Samia Suluhu alizungumza hayo aliposimama kuzungumza na wakazi wa Usa River wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.

Vijana hao wa Bodaboda walionyesha kumuunga mkono Rais Samia na kusindikiza Msafara wake kuelekea Usa River kwa ajili ya kuzungumza na Wananchi, baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri.

Aidha madereva bodaboda wamesisitiza kazi yao sio ya laana lakini pia wameishukuru serikali ya Rais Samia kwa kuendelea kuwapa mikopo inayowawezesha kuwekeza kwenye shughuli nyingine kama kilimo na biashara.

FqdPZRCXgAEBpec

Image
 
Ila kila kitu kwenye siasa ni fursa, kila kauli ya mmoja inaweza badilishwa na kuwa fursa kwa mwingine. Ila mwisho wa siku mnufaikaji ni mwanasiasa.

Bado watu wa VICOBA nao kuambiwa pia ni watoto wake.

Siku raia watakapoamka na kugundua kuwa wao sio mitaji ya kura za wanasiasa nahisi hapo tutapata kiongozi mzuri. Kinyume na hapo ni mwendo wa kutumiana na kutupana tu.
 
Le.ma yupo sahihi nyie ccm wapumbavu Sana yaani mnataka kusemaje. BodA ni ajira
Mimi sio CCM ila nina akili ya kusema boda ni informal employment. Inasaidia watu kujikimu katika umasikini wao. Huwezi kuita laana.

Alitakiwa kuchunga ulimi wake akajenga hoja kwa tahadhari kubwa. Sasa yeye kasema ni laana? Laaana?!!!!
 
Mimi sio CCM ila nina akili ya kusema boda ni informal employement. Inasaidia watu kujikimu katika umasikini wao. Huwezi kuita laana.
Alitakiwa kuchunga ulimi wake akajenga hoja kwa tahadhari kubwa. Sasa yeye kasema ni laana? Laaana?!!!!
acha kAzi uje uendeshe boda
 
..yuko nao kivipi?

..Je, amewahi kutumia usafiri wa bodaboda?

..Je, serikali yake itaacha ma-V8 na kuanza kutumia bodaboda.
 
Back
Top Bottom