Rais Samia: Haiwezekani jeshi lifanye mauaji na lijichunguze lenyewe

Rais Samia: Haiwezekani jeshi lifanye mauaji na lijichunguze lenyewe

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
1643967739491.png


Rais Samia Suluhu Hassan amezungumzia mauaji yaliyotokea Mtwara ambapo maafisa wa Jeshi la Polisi wanatuhumiwa kuhusika na mauaji ya mfanyabiashara Mussa Hamisi ambapo Jeshi limeunda kamati kuchunguza tukio hilo.

Rais amesema haiwezekani Jeshi kutuhumiwa kisha liunde kamati ya kujichunguza lenyewe, hivyo amesema amemuagiza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aunde kamati nyingine kuchunguza tukio hilo.

Amesema taarifa ya kamati ya polisi inayochunguza tukio hilo, italinganisha na taarifa ya kamati huru itakayoundwa na Waziri Mkuu.

Ameyasema hayo akiwa njiani akielekea Mwanza.

=======

Pia soma:
Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7 (25/01/2022)

Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022 (26/01/2022)


Kiundwe chombo huru cha kusimamia Jeshi la Polisi (25/01/2022)

 
" Haiwezekani jeshi lifanye mauaji na lijichunguze lenyewe" hii kauli imebeba ujumbe mzito sana, sijui Sirro bado anafanya nini ofisini mpaka leo.

Hapo nampongeza Rais, ni sahihi jeshi haliwezi kujichunguza, ila muhimu na hiyo kamati huru iliyoundwa na serikali iwe huru kweli wanasiasa wasiachwe wakaingilia maamuzi yake.

Nasema hivyo nikitambua mahusiano yaliyoko kati ya jeshi la polisi na wanasiasa wa CCM, inawezekana uhusiano wao hauishii kulindana kwenye chaguzi pekee unakwenda mbali zaidi, hawa wasije kuingilia kazi ya kamati iliyoundwa.

Napendekeza hiyo kamati iundwe na kuongozwa na watu huru wasio na mahusiano na siasa au wanasiasa, sio Waziri Mkuu.
 
Back
Top Bottom