Rais Samia kufanya ziara ya siku mbili Nchini Kenya kuanzia 04|05|2021

Rais Samia kufanya ziara ya siku mbili Nchini Kenya kuanzia 04|05|2021

Shida ni pale mama anapoona mtangulizi wake hakuwa sahihi kwa kila kitu na sasa hivi anafumua mpaka visivyostahili Kenya akiwachekea atajutia badaye jamaa wanafiki sana mama Mungu akupe maarifa uwe shujaa
Magufuli alikuwa kichaaa, muache mama SSH afumue kila kitu.

Unaanzaje kuwekeana bifu za KIJINGA na nchi mnapakana kwa kilometres zaidi ya 1,000, nchi ambayo Ina zaidi ya makampuni 200 yamewekeza nchini kwako?

Yule pimbi Mwendazake ndiyo maana Mungu kampoteza mapema maana tungefika hata 2023 Tanzania ingekuwa nchi ya HOVYO sana.

Unahitaji kutokuwa na akili kunipinga
 
JK aliwahi kusema ni mjinga tu asiyeweza kuona faida za ushirikiano kati ya Kenya na Tanzania. Alipoingia JPM hakutaka kuchezewa, walipoleta dharau za ile list ya mataifa yenye kuingia nchini mwao mwaka jana kuhusu corona, TCAA ikawapa jibu la jeuri ikizifungia ndege zao pia.

Natumaini Rais Samia hatakubali uungwana wetu ututukanishe huko tuendako.
 
Nimesoma comment zenu nyingiiii sana wengi wanaona kama SSH amekurupuka kwenda kenya kwa sabb wakenya ni wajuaji sana lkn mm nasema hapana kwa sabb wanasema kubali wito kataa ujumbe mm naona tumpe nafasi tu mama then tumpe muda tuone results.....!!
 
Mualiko gani ule wa harakaharaka. Hawakusubiri hata SSH azoee mazingira ya ikulu? Nadhani hata baadhi ya milango ya ikulu alikuwa hajaigusa bado wamesha mtuma sijui Amina nani vile maana mama yule alikuwa anaongea kwa kuhema utadhani alitembea kwa miguu kutokea Nairobi.
Ambacho hukijui ni kwamba raisi lazima asafiri. Raisi asiyesafir huyo ni mshamba na aliyepitwa na wakati.
Soma vizur Economic diplomacy mzee.
 
Mualiko gani ule wa harakaharaka. Hawakusubiri hata SSH azoee mazingira ya ikulu? Nadhani hata baadhi ya milango ya ikulu alikuwa hajaigusa bado wamesha mtuma sijui Amina nani vile maana mama yule alikuwa anaongea kwa kuhema utadhani alitembea kwa miguu kutokea Nairobi.
hahah. kenyatta noma sana alimtumia samia suluhu mama Amini ambae pia anavaa hijabu ili amlegeze samia
 
M
Magufuli aliwadhibiti vizuri sana Manyang'au..
Samia asilegeze
Mkuu, mie kiukweli siwapendi hawa jamaa kwa tabia yao ya kudandia kila kilicho chetu kiuchumi kukifanya kuwa chao. Siku moja nilikuwa nasikiliza radio moja ya nje ya kimataifa nikamsikia mzungu mmoja akihojiwa kuhusu uelewa wake kwa nchi ya Tanzania, akasema yeye alikuwa akiifaham Tanzania kama ni sehemu ya Kenya.
Kama mie ningekuwa Raisi wa nchi hii ningeielekeza nchi yetu ijikite sana na nchi zilizomo SADC. Wametulia hawana makandokando hata amani ni ya hali ya juu.
 
Shida ni pale mama anapoona mtangulizi wake hakuwa sahihi kwa kila kitu na sasa hivi anafumua mpaka visivyostahili Kenya akiwachekea atajutia badaye jamaa wanafiki sana mama Mungu akupe maarifa uwe shujaa
Ziara hii ni nafasi kwetu kujua yeye ni kiongozi wa namna gani.

Naona amaamua kujipambanua kungali mapema sana.

Tunasubiri kuona.
 
Mwaliko uliletwa haraka haraka, kana kwamba kuna dharura!

Sasa mama ameamua kuitikia mwaliko huo wiki ijayao. Haieleweki yaliyokuwemo ndani ya barua ile iliyowasilishwa kwake Dar es Salaam yalihitaji atembelee haraka hivyo; bila shaka ni ya manufaa makubwa kwao; na pengine na kwetu pia hadi mama akaona asichelewe zaidi.

Ni mwezi juzi tu, March, hawa jamaa walipokataza mahindi ya wakulima wetu yasiende kwao kwa visingizio vya kuwa yana 'mycotoxins', uamzi waliofanya kibabe na wakustukizia, kumbe ulikuwa ni uamzi uliotokana na kulinda maslahi ya wakulima wao zaidi kuliko athari za afflatoxins..., hivi huko kwao mahindi ya wakulima wao hayana tatizo hilo!

Na huko miaka ya nyuma je, walipokuwa wakila mahindi yetu, walikufa wangapi? Sisi tunaokula hayo mahindi, miili yetu ni sugu? Uamzi huo haukuwa wa kiungwana kwa jirani unayeshirikiana naye katika biashara.

Siyo hivyo tu, hawa jamaa ni wazuri sana wa kulaumi na kulalamikia wengine huku wao wakijiona kuwa ndio kipimo kinachotakiwa kutumiwa na majirani zao.

Sukari, maziwa mayai, kuku wa Uganda wamezuia kuingia kwao wakilinda wazalishaji wao, huku wao wakihimiza Uganda inunue bidhaa kutoka kwao.

Sasa angalia wanavyomkaribisha mama atakapotembelea -

Wanaandika: Tanzania President to visit Kenya this week.

"She has the responsibility of correcting the continuous tariff between the two neighbouring countries."

Kwa hiyo ni wajibu wa mama kurekebisha, wao hawana linalowahusu!

Wakati mama Samia akitembelea huko, ni vema awe na uelewa mpana kuhusu majirani zetu hawa. Hawa tumetoka nao mbali sana, na bila shaka historia yote anaifahamu vyema.

Ni vizuri pia ajikumbushe wenzake (marais) walivyoshughulika na hawa majirani. Asije akajikuta yeye anasakamia tu toka kwa huyo mwenzake ambaye anajulikana kuwa kizabinazabina mkubwa. Hana msimamo yupo kila mahala, akijiuza na kuwachimba wenzake.
Kahangaika sana na EPA, akitaka tutumbukie tu humo kwa manufaa yake bila kujali sisi tutafaidika vipi. Anatafuta kuingia kwenye mikataba ya kibiashara na mataifa mengine, bila kujali uhusika wake katika jumuia yetu...

Bila shaka haya yatakuwa ni sehemu ya maongezi kati yao, na pengine mama naye kajiandaa ipasavyo.

Tutamsikiliza kwa makini.

====

By Aggrey Mutambo
Senior Diplomatic Writer

Nation Media Group

What you need to know:
If the visit goes ahead as planned, the Tanzanian leader will be coming to Nairobi nearly five years since her predecessor made a similar visit.

Tanzanian President Samia Suluhu is likely to visit Nairobi this week in a trip laden with diplomatic significance.

If the visit goes ahead as planned, the Tanzanian leader, who took over from John Pombe Magufuli following his death in March, will be coming to Nairobi nearly five years since her predecessor made a similar visit.

The trip was confirmed by two diplomats familiar with the arrangement.

She has the responsibility of correcting the continuous trade tiffs between the two neigbouring countries.

In a speech to Parliament last week, President Suluhu told legislators that her administration will pursue economic diplomacy with partners in the region and across the world, signaling intent to repair relations with the outside world.

“If you call it a change, then it will be a renewed effort on economic diplomacy,” she said, referring to better ties with the East African Community, Southern Africa Development Community and the recent Africa Continental Free Trade Area (AfCTA).

Collaboration
President Suluhu’s policy, she pledged, will run on a smoother domestic programme to attract investors, while sustaining relations with key partners the country trades with.

She thinks her diplomats must work better at making the country attractive rather than being an island.

“Our diplomatic staff have to be competent in striking deals in investment and trade promotion as well as seek strategic partners in tourism”, she said.

The itinerary of the planned Kenyan trip had not been made public by Saturday with officials indicating there were still final touches to be made. But the Sunday Nation understands she intends to meet with business lobbies in Nairobi, after holding talks with President Uhuru Kenyatta to discuss bilateral issues.

Renewed trust
This would be her first State visit since taking power, although she has already made an official trip to Uganda where the two countries signed a multi-billion-dollar oil pipeline deal with French oil giant Total and China’s CNOOC.

Frequent non-tariff wars with Kenya have slowed down trade to an average of Sh40 million a year, down from Sh64 billion during Jakaya Kikwete’s era.

Nairobi has indicated renewed trust in the organs of the East African Community whose secretariat is now headed by Kenyan, Dr Peter Mathuki. “We intend to sort out the issues through the established organs of the EAC,” said Johnson Weru, PS for Trade when asked on Kenya’s plan to eliminate the trade wars.

amutambo@ke.nationmedia.com

UPDATES:

Tanzania President Samia Suluhu Hassan is set to jet into Kenya Tuesday, May 4th, for a two-day State Visit.

According to @StateHouseKenya,H.E Pres. Uhuru Kenyatta will receive H.E Pres. Suluhu at State House.
Nadhani haya mambo hayataki jazba, sisi na Kenya sio maadui ila wahasimu wa mambo ya nani bora ambalo ni jambo zuri kama litaleta faida za kiushindani lakini sisi sio maadui kabisa. Simba na Yanga sio maadui wahasimu tu ndio kama sisi na Kenya. Kenya ndio nchi inayoongoza uwekezaji mkubwa kwetu ni number moja sasa huyo sio adui, nakumbuka maneno ya Kikwete aliyaongea hata yeye ni kichaa tu anaweza kuvunja uhusiano sababu tumeshikana sana kiuchumi sasa Mama anarekebisha tu tulipokosea mambo binafsi ya urafiki na Odinga hayana tija na sisi maslahi ya nchi mbele. Kenya wanatuhitaji na sisi tunawahitaji. Mama weka mambo sawa leo hakuna hata bus linaenda Kenya au kuja huku biashara zitaendaje.
 
Ntatofautiana na wanaobeza hii ziara kwa wakenya, mimi naunga mkono asilimia 100 Kenya ni muhimu sana kwa uchumi wetu na sisi ni muhimu sana kwa uchumi wao.
Bahati mbaya watu hawaelewi investment ya wa Kenya hapa kwetu wanaongoza Africa. Sisi sio maadui ila tunashindana kwa maendeleo ni jambo zuri na Mama anaenda kuweka mambo sawa cross border business lazima irudi kama kawaida tulikuwa na ndege za Kenya 6 times a day leo sijui mara 3 kwa wiki na uhakika tutaanza kuona biashara tena kwa wingi na sote tunahitajiana sana tu.
 
Nani kashabikia kujifungia.
Kwani Kenya ndio dunia pekee? DRC, Malawai, Zambia, Mozambique, Uganda, Rwanda, Burundi, Comoro, na kwingineko, huko hakuna dunia?
Hizo nchi zote ulizozitaja wamewekeza nini hapa kwetu kwenye Foregn direct investment? Kenya wamewekeza kiasi kikubwa hapa kuliko nchi yoyote ya Africa. Mama kesho anaenda kuweka mambo sawa biashara irudi wewe labda unaongelea wale wanunuzi wa Kariakoo. Hawa wana inject FDI nchini ndio kipimo cha uchumi kukua. Kikwete alishasema haya ni kichaa tu anaweza kuharibu uhusiano huu. Mama yuko vizuri anajuwa waliteleza wapi. Kumbuka Nairobi ni hub ya mashirika yote makubwa wana office zao pale huwezi kudharau hilo ukaenda Lilongwe au kucheza ndombolo Kinshansa.
 
Nadhani haya mambo hayataki jazba, sisi na Kenya sio maadui ila wahasimu wa mambo ya nani bora ambalo ni jambo zuri kama litaleta faida za kiushindani lakini sisi sio maadui kabisa. Simba na Yanga sio maadui wahasimu tu ndio kama sisi na Kenya. Kenya ndio nchi inayoongoza uwekezaji mkubwa kwetu ni number moja sasa huyo sio adui, nakumbuka maneno ya Kikwete aliyaongea hata yeye ni kichaa tu anaweza kuvunja uhusiano sababu tumeshikana sana kiuchumi sasa Mama anarekebisha tu tulipokosea mambo binafsi ya urafiki na Odinga hayana tija na sisi maslahi ya nchi mbele. Kenya wanatuhitaji na sisi tunawahitaji. Mama weka mambo sawa leo hakuna hata bus linaenda Kenya au kuja huku biashara zitaendaje.
Nimekusoma kwa taratibu nikuelewe vizuri.

Sasa ni hivi, na napenda hata wewe unielewe ninachoamini mimi.

Kenya na sisi ni majirani, hakuna chochote tunachoweza kufanya juu ya hilo, daima tutakuwa majirani.

Majirani wanaweza kuwa majirani wema na wakaelewana na kutakiana mema; hata kama hapawezi kukosekana mikwaruzo ya hapa na pale, kama ilivyo kwa ndugu wanaoishi nyumba moja.
Hili nalo linaeleweka.

Kama majirani, na hata bila kuwa majirani, tunaweza kufanya biashara kati yetu kwa misingi ya kibiashara bila kujali tu marafiki au sio marafiki. Natumaini hili nalo hata wewe unalielewa.
Ndiyo, katika biashara kuna ushindani, kama ilivyo katika michezo, kama hiyo ya Simba na Yanga uliyo itolea mfano. Lakini, katika hilo la ushindani ndipo panapoweza kuanzia tatizo. Kuna kufanyiana mambo mabaya ili ushinde. Kuna washindani wa namna hiyo, na kama kweli unaamini hili haliwezekani, basi hapa ndipo tofauti yako inapoanzia.

Nchi zetuhizi, kihistoria ina mitizamo kinzani toka zamani, sijui kama ni tabia za watu au vipi? Kisiasa pia tunatofautiana sana kati yetu na hawa majirani zetu. Huwezi kufumba macho na akili kabisa usizione tofauti hizo kati yetu.
Sisi hatukuwa na tabia ya kunyang'anyana, hadi hivi karibuni, na ukabila haukuwa tatizo kwetu, haya mambo kwa upande wa pili ni hali ya kawaida sana.

Siwezi kuorodhesha tofauti zote zinazotutofautisha kati yetu, lakini kama una msimamo wa wazi huwezi kukosa kuzijua tofauti hizo.

Kwa hiyo, naomba unielewe, sikatai tufanye biashara, biashara kama itanoga, tutaanzia hapo kujengeana imani na hayo mengine ya udugu na urafiki.

Huwezi kuniita ndugu au rafiki huku ukitafuta njia za kuniangusha. Kama wewe huoni mbinu hizo, usidhani wengine nao hawazioni.
 
Hizo nchi zote ulizozitaja wamewekeza nini hapa kwetu kwenye Foregn direct investment? Kenya wamewekeza kiasi kikubwa hapa kuliko nchi yoyote ya Africa. Mama kesho anaenda kuweka mambo sawa biashara irudi wewe labda unaongelea wale wanunuzi wa Kariakoo. Hawa wana inject FDI nchini ndio kipimo cha uchumi kukua. Kikwete alishasema haya ni kichaa tu anaweza kuharibu uhusiano huu. Mama yuko vizuri anajuwa waliteleza wapi. Kumbuka Nairobi ni hub ya mashirika yote makubwa wana office zao pale huwezi kudharau hilo ukaenda Lilongwe au kucheza ndombolo Kinshansa.
Sasa hili la kuwekeza naona limekutoa akili kwelikweli.
Kwa hiyo kwa vile amewekeza unataka sasa tufanyeje, si hivyo kumbe anafanya biashara?
Sasa unalilia nini hapa. Tufanye nini cha ziada?

Sasa angalia usivyokuwa na ufahamu. Kwa hiyo hizo nchi nyingine tuendelee kuziweka pembeni kwa vile hawawekezi? Hii ni akili ya namna gani hii!

Huyo anayewekeza, mbona juzi kayakataa mahindi yetu kwa kisingizio tu cha kuwa na sumu. Umejaribu kulifikiria hilo? Hawa wakulima wetu huwaonei huruma, wewe unaangalia 'investment' pekee? Huo ndio uhusiano unaoutafuta hapa?
 
Back
Top Bottom