Rais Samia, kuna mtu mmoja tu hapa Tanzania anaweza kukusaidia kuuvuka huu mtihani wa DP World na TEC - muite, ongea nae, msikilize, ufanye atachosema

Rais Samia, kuna mtu mmoja tu hapa Tanzania anaweza kukusaidia kuuvuka huu mtihani wa DP World na TEC - muite, ongea nae, msikilize, ufanye atachosema

Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.

Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI kweli kwamba suala hili linazidi kuweka taswira mbaya sana nchini, na huenda linakukosesha usingizi kwa kuwa hukutarajia litafika huku. Nahisi pia kuna mambo ambayo hatujui, labda upande wa UAE-Dubai, yanayolifanya liwe gumu hata zaidi. Na usipoangalia mambo yatazidi kuharibika.

Sasa maraisi wa kabla yako wamewahi kupitia vipindi vigumu kama vyako. Raisi Mkapa kuna wakati kulikuwa na suala na rada ya BAE. Serikali ya Uingereza ikamsumbua sana. Akaomba huyu mtu nitakaekutajia mwishoni amsaidie kulitatua. Na matokeo ni kwamba huyu mtu alilitatua kwa namna ambayo ilimfanya Raisi Mkapa amheshimu sana, kwa kuwa alilitatua kwa namna ya hekima, na ufahamu wa hali ya juu, hata Uingereza wakamsifia kwa hekima zake kwa jinsi alivyolitatua.

Kisha wakati fulani uhusiano kati ya Raisi Kikwete na Raisi Kagame uliharibika sana, hata Raisi Kagame akatishia kumpiga Raisi Kikwete. Kuona hivyo, Raisi Kikwete ikabidi amuombe huyu mtu asaidie kulimaliza hili suala, na kwa mara nyingine akalimaliza kwa namna ya busara sana iliyorejesha uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda kwenye hali ya kawaida. Kutoka hapo Raisi Kikwete aliamua huyu mtu akae karibu yake katika ofisi ya Raisi ili azidi kumsaidia mambo mengine mengi.

Na labda nikuambie pia wakati fulani kulikuwa na suala la kupeleka boti za abiria kwenye ziwa Victoria, na mtangulizi wako Raisi Magufuli akagoma katakata kuzipeleka boti hizi kupitia barabara zetu. Hii ilileta mtafaruku sana kati ya mfanyabiashara maarufu nchini na serikali. Huyo huyo mtu ninaekuambia akaamua kuingilia kati na kuwasiliana na serikali ya Kenya. Kwa diplomasia yake serikali ya Kenya ilikubali kutatua tatizo hili. Jinsi alivyotatua tatizo hili ilimletea heshima sana kwa baraza la mawaziri Kenya na Tanzania, japo ilimfadhaisha sana Magufuli, wakati huo akiwa waziri katika serikali ya Kikwete, na kufanya awe na chuki nae, chuki aliyoiendeleza hata alipochaguliwa kuwa raisi.

Na labda utakuwa unajua kwamba huyu mtu aliingizwa katika serikali kutokana na ushauri wa Raisi Clinton kwa Mkapa. Raisi Clinton alishangaa sana kwamba kwa nini serikali ilikuwa haimtumii mtu huyu ambae Raisi Bill Clinton na Makamu wake Al Gore walimsifia sana kwa jinsi alivyoshughulikia kwa umakini mkubwa na busara za hali ya juu negotiations za climate change akiwa msemaji wa Group of 77 and China. Mkapa akawasikiliza.

Japo si mwanasheria, kuna wakati, Tanzania na nchi nyingine za mto Nile wakiwa katika mkutano wa kusign makubaliano ya Mto Nile, alizuia utiaji sahihi wa makubaliano hayo baada ya kugundua vipengele katika mkataba huo ambavyo mawaziri wa nchi nyingine hawakuviona. Vilikuwa vipengele ambavyo vilitoa faida kubwa kwa nchi moja ya mto Nile na kuondoa haki ya matumizi ya maji kwa nchi nyingine, vikiwa vimeandikwa kimaficho. Hizi nchi nyingine zikamsifia sana kwa umakini wake hadi kugundua hilo.

Kuna mambo mengi sana amefanya ambayo watu walimsifia kwa busara na hekima zake, ndani na nje ya Tanzania, siwezi kuyaweka yote hapa.

Mtu huyu anaitwa Prof. Mark Mwandosya. Muite, kaa nae, mwache akushauri kwenye hili jambo, na tekeleza atakachokuambia. Umekuwa ukiwasikiliza watu ambao wanakuambia nguo yako isiyoonekana inakupendeza sana - wanakudanganya na wanakupotosha wakidhani wanakuambia kile unachotaka kusikia ili uendelee kuwa nao. Mwite Prof. Mwandosya mkae nyie wawili tu kutafuta way forward juu ya jambo hili - na nakuambia utanitafuta kunishukuru kwa huu ushauri wa bure ninaokupa hapa. Kila la kheri.
Pamoja na huyu unayemsema hapa kuna chuma hiki kina roho wa Mungu na hakina udhehebu wala udini bali hunena maagizo ya yeye aliye juu akiite kitamuambia yampasayo kufanya nacho si kingine bali ni Mwl. Christopher Mwakasege. Azingatie sana hili maana aendapo kuna giza totoro kwake na ni hakika asipokuwa makini akiendelea kuendekeza machawa basi ataandika historia mbaya sana. Itakuwa heri endapo akilisikia neno hili la Mungu.
 
Mwandosya apeleke ushauri mwenyewe, asisubiri kuitwa
Huyo Huyo Mwandosya ambaye amekuwa mtetezi na mlinzinwa Katiba Mbovu na Mifumo mibaya Nchini?

Au kwa kuwa sasa hivi katemwa na serikali mnamtafutia ugali.
 
Pamoja na huyu unayemsema hapa kuna chuma hiki kina roho wa Mungu na hakina udhehebu wala udini bali hunena maagizo ya yeye aliye juu akiite kitamuambia yampasayo kufanya nacho si kingine bali ni Mwl. Christopher Mwakasege. Azingatie sana hili maana aendapo kuna giza totoro kwake na ni hakika asipokuwa makini akiendelea kuendekeza machawa basi ataandika historia mbaya sana. Itakuwa heri endapo akilisikia neno hili la Mungu.
Mzee wa kukusanya Mbegu ya sadaka tu hana lolote.

Hakuna mtumishi pale.

Nchi inaangamia kwa maovu na dhambi yeye yuko bize na
1. kupanda mbegu
2. mzaliwa wa kwanza
3. Sadaka
4.maono
5. Lango.
 
Kwani yeye hawezi kuchukua maamuzi mazuri hadi apate ushauri kutoka kwa mtu.Jibu lililobaki ni kurekebisha vile vipengele vya kilofa na kijuha ambavyo vimeelezwa haihitaji tena kurudiwa au aachane nao kabisa mkataba.kama hawezi kuchukua maamuzi ambayo hata mtoto wa miaka kumi angeweza basi itakuwa hatoshi kuwaongoza watanzania
Hili ndio jambo gumu kwa ccm
 
Haaminiki tena.
Ndo tatizo ambalo nchi yetu imefikia sasa huwezi kumuamini yoyote yule ambae amepewa dhamana ya kuongoza.

Viongozi wala kwa kamba zao (kwa ruhusa ya raisi, na pia watumishi wa umma wote ni wezi wakiiba mapato ya serikali na fedha za miradi mbalimbali.

Kama ni usafi nchi hii yahitaji "cleaning".
 
Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.

Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI kweli kwamba suala hili linazidi kuweka taswira mbaya sana nchini, na huenda linakukosesha usingizi kwa kuwa hukutarajia litafika huku. Nahisi pia kuna mambo ambayo hatujui, labda upande wa UAE-Dubai, yanayolifanya liwe gumu hata zaidi. Na usipoangalia mambo yatazidi kuharibika.

Sasa maraisi wa kabla yako wamewahi kupitia vipindi vigumu kama vyako. Raisi Mkapa kuna wakati kulikuwa na suala na rada ya BAE. Serikali ya Uingereza ikamsumbua sana. Akaomba huyu mtu nitakaekutajia mwishoni amsaidie kulitatua. Na matokeo ni kwamba huyu mtu alilitatua kwa namna ambayo ilimfanya Raisi Mkapa amheshimu sana, kwa kuwa alilitatua kwa namna ya hekima, na ufahamu wa hali ya juu, hata Uingereza wakamsifia kwa hekima zake kwa jinsi alivyolitatua.

Kisha wakati fulani uhusiano kati ya Raisi Kikwete na Raisi Kagame uliharibika sana, hata Raisi Kagame akatishia kumpiga Raisi Kikwete. Kuona hivyo, Raisi Kikwete ikabidi amuombe huyu mtu asaidie kulimaliza hili suala, na kwa mara nyingine akalimaliza kwa namna ya busara sana iliyorejesha uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda kwenye hali ya kawaida. Kutoka hapo Raisi Kikwete aliamua huyu mtu akae karibu yake katika ofisi ya Raisi ili azidi kumsaidia mambo mengine mengi.

Na labda nikuambie pia wakati fulani kulikuwa na suala la kupeleka boti za abiria kwenye ziwa Victoria, na mtangulizi wako Raisi Magufuli akagoma katakata kuzipeleka boti hizi kupitia barabara zetu. Hii ilileta mtafaruku sana kati ya mfanyabiashara maarufu nchini na serikali. Huyo huyo mtu ninaekuambia akaamua kuingilia kati na kuwasiliana na serikali ya Kenya. Kwa diplomasia yake serikali ya Kenya ilikubali kutatua tatizo hili. Jinsi alivyotatua tatizo hili ilimletea heshima sana kwa baraza la mawaziri Kenya na Tanzania, japo ilimfadhaisha sana Magufuli, wakati huo akiwa waziri katika serikali ya Kikwete, na kufanya awe na chuki nae, chuki aliyoiendeleza hata alipochaguliwa kuwa raisi.

Na labda utakuwa unajua kwamba huyu mtu aliingizwa katika serikali kutokana na ushauri wa Raisi Clinton kwa Mkapa. Raisi Clinton alishangaa sana kwamba kwa nini serikali ilikuwa haimtumii mtu huyu ambae Raisi Bill Clinton na Makamu wake Al Gore walimsifia sana kwa jinsi alivyoshughulikia kwa umakini mkubwa na busara za hali ya juu negotiations za climate change akiwa msemaji wa Group of 77 and China. Mkapa akawasikiliza.

Japo si mwanasheria, kuna wakati, Tanzania na nchi nyingine za mto Nile wakiwa katika mkutano wa kusign makubaliano ya Mto Nile, alizuia utiaji sahihi wa makubaliano hayo baada ya kugundua vipengele katika mkataba huo ambavyo mawaziri wa nchi nyingine hawakuviona. Vilikuwa vipengele ambavyo vilitoa faida kubwa kwa nchi moja ya mto Nile na kuondoa haki ya matumizi ya maji kwa nchi nyingine, vikiwa vimeandikwa kimaficho. Hizi nchi nyingine zikamsifia sana kwa umakini wake hadi kugundua hilo.

Kuna mambo mengi sana amefanya ambayo watu walimsifia kwa busara na hekima zake, ndani na nje ya Tanzania, siwezi kuyaweka yote hapa.

Mtu huyu anaitwa Prof. Mark Mwandosya. Muite, kaa nae, mwache akushauri kwenye hili jambo, na tekeleza atakachokuambia. Umekuwa ukiwasikiliza watu ambao wanakuambia nguo yako isiyoonekana inakupendeza sana - wanakudanganya na wanakupotosha wakidhani wanakuambia kile unachotaka kusikia ili uendelee kuwa nao. Mwite Prof. Mwandosya mkae nyie wawili tu kutafuta way forward juu ya jambo hili - na nakuambia utanitafuta kunishukuru kwa huu ushauri wa bure ninaokupa hapa. Kila la kheri.
Mh Rais nakushauri muite Mungu wa mbinguni Asabuhi, Mchana na Jioni maana yeye pekee ndie mshauri wa ajabu, komandoo na jemedari wa vita na uovu atakuskia, nena nae taratibu bila kuchoka, atakushika mkono na atakuonyesha njia, na hili nalo litapita...
 
Sijui hayo mengine ila uliposema eti kagame alitaka kumpiga kikwete ikabidi kikwete amuite mwandosya amsaidie umeongopa mkuu.
Sipendi kubishana na watu wasiojua kwa sababu ni kujitia ujinga, maana hata sijui unachobisha hapa ni nini. Ni kwa sababu ya watu kama wewe niliona ngoja niondoke JF. Unajikuta unabishana na mtu hajui, na hajui kama hajui, na kwa sababu hajui anabisha tu kama mjinga fulani hivi

Soma hizi post hapa chini za 2013 na 2021, ili uone wewe ni mtu wa aina gani, maana huenda ulikuwa unacheza uchi haya ya Nitampiga Kikwete yalipotokea


1692540734043.png

1692540867433.png
 
Sipendi kubishana na watu wasiojua kwa sababu ni kujitia ujinga, maana hata sijui unachobisha hapa ni nini. Ni kwa sababu ya watu kama wewe niliona ngoja niondoke JF. Unajikuta unabishana na mtu hajui, na hajui kama hajui, na kwa sababu hajui anabisha tu kama mjinga fulani hivi

Soma hizi post hapa chini za 2013 na 2021, ili uone wewe ni mtu wa aina gani, maana huenda ulikuwa unacheza uchi haya ya Nitampiga Kikwete yalipotokea


View attachment 2723017
View attachment 2723019
Kama ulitoka sababu hizi JF asee we toka tu. Huna cha maana zaidi ya kujiona unajua kumbe huna lolote

Sasa katika hayo uliyoambatanisha hapo ni wapi umeonesha kikwete alimtuma mwandosya akamsaidie kwa kagame?

Acha undezi basi. Usidhani unajua saaaaaana kumbe Potoma tu
 
akiwa waziri wa mawasiliano TTCL ilibinafusishwa Kwa kampuni iliyokuwa inamiliki Airtel kabla haijauzwa, mkataba ule ulikuwa hauna maslahi kwa Taifa lakini yeye kama waziri mwenye dhamana alikuwa anawakingia kifua.
Baadae iligundulika hiyo kampuni iligharamikia scholarship ya binti yake, Kwa kifupi kulikuwa na mgongano wa maslahi.
Tatizo watu mnarukia propaganda chafu za watu waliokuwa wakimchafua Prof. Mwandosya na mnajitoa akili kabisa. Kumbuka ni watu walipoona propaganda zao hazifanikiwi waliamua kumnywesha sumu ikabidi akae hospitali India miezi karibu sita.

Kama unafikiri Prof. Mwandosya ni mtu ambae angeweza kuhongwa "scholarship" ya mtoto wake ili auze shirika la umma basi huna akili za kukufanya uweze kufikiri. Na kumbuka sponsorship waliyoisema ni pale mtoto wake alienda South Africa study tour, wiki mbili sijui. Kwamba Mwondosya angeshindwa kumgharamia ticket ya economy na kukaa South kwa wiki mbili, ikiwa watoto wake wengine alikuwa akiwasomesha nje ya nchi kwa hela yake? Does it make sense to you?

Japo sina hela kama ya Prof. Mwandosya na mie sio waziri, ili kukuondoa ujinga ningeweza kukukatia ticket ya ndege kwenda South Africa ukakae wiki mbili unakula na kulala tu, ili siku nyingine usiamini kila unachoambiwa, na kukuonyesha kwamba kwenda South Afrika na kukaa wiki mbili ni kitu kidogo sana hata mfanyakazi wa kawaida anaweza kukimudu. Epuka dhana ya kuona ili upande ndege kwenda mahali kama South Africa lazima uwe tajiri kama Dewji na waziri hawezi ku-afford kumlipia mtoto wake safari ya South Africa inabidi ahongwe kuuza shirika ili mtoto wake aende South Africa study tour.
 
Kama ulitoka sababu hizi JF asee we toka tu. Huna cha maana zaidi ya kujiona unajua kumbe huna lolote

Sasa katika hayo uliyoambatanisha hapo ni wapi umeonesha kikwete alimtuma mwandosya akamsaidie kwa kagame?

Acha undezi basi. Usidhani unajua saaaaaana kumbe Potoma tu

Mbona hujauliza ni wapi Mkapa alimtuma Mwandosya? Yaani ulitaka Kikwete atangaze kwamba "jamaani eeeh, namtuma Mwandosya kwenda kusuluhisha ugomvi wangu na Kagame" ili magazeti yaandike?

Hebu tumia akili wewe. Unafikiri mie ningeandika kitu ambacho Samia hajui au hawezi kuuliza, na nikijua Kikwete pia anaweza kusoma? Nitatumiaje point kumshawishi Samia ambazo atajua sio za kweli? Kwamba umeshindwa hata kuwaza hili basi hufai hata kujibishana na mie katika hili. Ukiweza nenda kamuulize Kikwete, au muulize Kagame basi. Au muulize Samia basi, je ni kweli Mwandosya alifanya hili?

Na kuzidi kukuonyesha hujui, angalia hapa chini. Unaelewa kwa nini imeandikwa Mwandosya alitumwa "to learn on how Rwanda plans and implements social and economic services"? Popoma nani sasa?

1692543064883.png
 
Huu mkataba unapita tu hata asipomtafuta. Ukikaa kusikiliza watu sana yako hayataenda.
 
Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.

Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI kweli kwamba suala hili linazidi kuweka taswira mbaya sana nchini, na huenda linakukosesha usingizi kwa kuwa hukutarajia litafika huku. Nahisi pia kuna mambo ambayo hatujui, labda upande wa UAE-Dubai, yanayolifanya liwe gumu hata zaidi. Na usipoangalia mambo yatazidi kuharibika.

Sasa maraisi wa kabla yako wamewahi kupitia vipindi vigumu kama vyako. Raisi Mkapa kuna wakati kulikuwa na suala na rada ya BAE. Serikali ya Uingereza ikamsumbua sana. Akaomba huyu mtu nitakaekutajia mwishoni amsaidie kulitatua. Na matokeo ni kwamba huyu mtu alilitatua kwa namna ambayo ilimfanya Raisi Mkapa amheshimu sana, kwa kuwa alilitatua kwa namna ya hekima, na ufahamu wa hali ya juu, hata Uingereza wakamsifia kwa hekima zake kwa jinsi alivyolitatua.

Kisha wakati fulani uhusiano kati ya Raisi Kikwete na Raisi Kagame uliharibika sana, hata Raisi Kagame akatishia kumpiga Raisi Kikwete. Kuona hivyo, Raisi Kikwete ikabidi amuombe huyu mtu asaidie kulimaliza hili suala, na kwa mara nyingine akalimaliza kwa namna ya busara sana iliyorejesha uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda kwenye hali ya kawaida. Kutoka hapo Raisi Kikwete aliamua huyu mtu akae karibu yake katika ofisi ya Raisi ili azidi kumsaidia mambo mengine mengi.

Na labda nikuambie pia wakati fulani kulikuwa na suala la kupeleka boti za abiria kwenye ziwa Victoria, na mtangulizi wako Raisi Magufuli akagoma katakata kuzipeleka boti hizi kupitia barabara zetu. Hii ilileta mtafaruku sana kati ya mfanyabiashara maarufu nchini na serikali. Huyo huyo mtu ninaekuambia akaamua kuingilia kati na kuwasiliana na serikali ya Kenya. Kwa diplomasia yake serikali ya Kenya ilikubali kutatua tatizo hili. Jinsi alivyotatua tatizo hili ilimletea heshima sana kwa baraza la mawaziri Kenya na Tanzania, japo ilimfadhaisha sana Magufuli, wakati huo akiwa waziri katika serikali ya Kikwete, na kufanya awe na chuki nae, chuki aliyoiendeleza hata alipochaguliwa kuwa raisi.

Na labda utakuwa unajua kwamba huyu mtu aliingizwa katika serikali kutokana na ushauri wa Raisi Clinton kwa Mkapa. Raisi Clinton alishangaa sana kwamba kwa nini serikali ilikuwa haimtumii mtu huyu ambae Raisi Bill Clinton na Makamu wake Al Gore walimsifia sana kwa jinsi alivyoshughulikia kwa umakini mkubwa na busara za hali ya juu negotiations za climate change akiwa msemaji wa Group of 77 and China. Mkapa akawasikiliza.

Japo si mwanasheria, kuna wakati, Tanzania na nchi nyingine za mto Nile wakiwa katika mkutano wa kusign makubaliano ya Mto Nile, alizuia utiaji sahihi wa makubaliano hayo baada ya kugundua vipengele katika mkataba huo ambavyo mawaziri wa nchi nyingine hawakuviona. Vilikuwa vipengele ambavyo vilitoa faida kubwa kwa nchi moja ya mto Nile na kuondoa haki ya matumizi ya maji kwa nchi nyingine, vikiwa vimeandikwa kimaficho. Hizi nchi nyingine zikamsifia sana kwa umakini wake hadi kugundua hilo.

Kuna mambo mengi sana amefanya ambayo watu walimsifia kwa busara na hekima zake, ndani na nje ya Tanzania, siwezi kuyaweka yote hapa.

Mtu huyu anaitwa Prof. Mark Mwandosya. Muite, kaa nae, mwache akushauri kwenye hili jambo, na tekeleza atakachokuambia. Umekuwa ukiwasikiliza watu ambao wanakuambia nguo yako isiyoonekana inakupendeza sana - wanakudanganya na wanakupotosha wakidhani wanakuambia kile unachotaka kusikia ili uendelee kuwa nao. Mwite Prof. Mwandosya mkae nyie wawili tu kutafuta way forward juu ya jambo hili - na nakuambia utanitafuta kunishukuru kwa huu ushauri wa bure ninaokupa hapa. Kila la kheri.

Ushauri wako ni mzuri, kama mtu ana nia ya kushauriwa. Kuna watu ukiwashauri, wanaona kama unawaendesha au unawaamrisha nini cha kufanya. Ila kama kweli mtu anahitaji ushauri, huyo mtu ukimshauri anapokea ushauri.
 
Hapo ulipoandika kuna MTU MMOJA TU
Yaani Tanzania nzima yenye watu zaidi ya milioni sitini kuna mtu mmoja tu

Ndugu yangu Synthesizer ule uamuzi wa kutokuleta nyuzi hapa endelea nao mana mawazo yako yanakaribia kugota

Yeye kaona huyo mmoja ndo maana kamweka hapa. Kama kuna mwingine unayemjua au kama kuna mtu mwingine anamfahamu mtu ambaye anaweza kumshauri Rais, basi ni ruksa kuweka maoni yako hapa
 
Back
Top Bottom