Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 13,417
- 23,310
maso pa kyindi tumvumilie tu Polepole kwa kuwa anatumia uhuru wa maoni ulioruhusiwa na Rais SSH mwenyewe alipopokea madaraka ya kuongoza Nchi baada ya yule Dikteta kufariki na kuzikwa Chato.Wakati sisi wana CCM tulielewa vyema maana ya Rsis kuwaasa mawaziri wake kutoingiliana kimamlaka na utendaji alipoongea na baraza lake la mawaziri, kwa uwazi, wengine wameamua kumwekea Mama Samia maneno mdomoni, kwa maana hasi na isiyostahili utumishi wa umma.
Polepole, mbunge wa kuteuliwa na Rais Samia amekuwa akimnanga Mama Samia kila apatapo nafasi hiyo, na kumpinga Mama waziwazi.
Mimi mmoja wa tulioukubali, kuupokea na kuunga mkono utawala wa Awamu ya Sita, naona huyu Polepole ni msaliti, apigwe chini.
Polepole, kama Ndugai wana mipango ambayo haiko wazi.
Wakae nje ya uongozi ili mambo yao wakayasuke vizuri.
Watanzania hatukuzoea kunyimwa haki ya kujieleza kama alivyoiminya Mwendazake Magufuli