Rais Samia: Msikubali wanaotaka kuanzisha chokochoko, pakichafuka ni wewe utakayekaa ndani

Rais Samia: Msikubali wanaotaka kuanzisha chokochoko, pakichafuka ni wewe utakayekaa ndani

Nilisha apa kuilinda nchi yangu mkuu, yeyote mwenye ujingaujinga ni kula ki......!
Hakika ULINZI NA USALAMA WA AMANI YA NCHI YETU NI JUKUMU LETU! Nyie chokochoko mtatuwia radhi binafsi sikubali kuichezea amani tuliyojaaliwa kuwa nayo.Il
 
Swala la katiba lina umuhimu wake... Na sisi watz siku tukiacha unafiki ndo inchi itasonga mbele..... Ni juzi tu mlikuwa mkilia lia magu hafati sheria leo hamtaki tena katiba?? Binafsi naitaka katiba na sio kwasababu za chadema"" ila i wish katiba mpya iwepo na ifute mamlaka ya raisi kutowajibishwa pamoja na viongozi wa wakuu wa nchi!!!! Yani hili ndo linanikera kwamba raisi haguswi, spika wa bunge haguswi, jaji mkuu wa serikali haguswi, DPP haguswi... Hii katiba haifai yani inawaruhusu wao kufanya watakavyo kwasababu hawaguswi!!! Kwa mfano hii kauli ya mama haifai ukiwa mkuu wa nchi lazima uwe na solution yakumaliza tatizo na wapinzani wako sio kutisha raia kwamba wataumia.... Kwa kauli hii raisi kwenye nchi za wenzetu unashitakiwa ni kauli yakichochezi hupaswi kuongea kwenye hadhara ya watu!!! Mamlaka ya raisi lazima yawe na mipaka na katiba ile kwasababu inchi kama ichi hatuna vision kila raisi anakuja na lake' atavyojisikia yeye ndo atafanya sio kwa mujibu wa sheria yani afate sheria!!! Tuone kuna umuhimu wa katiba lengo sio chadema kutawala au kutaka madaraka... Ije katiba mpya hata kama CCM itaendelea kuongoza ila katiba iwepo na waifate ili wasipofata sheria katiba iyo iyo iwawajibishe... Lakini hii iliyopo naona kama kila kitu ni ndio na imewabeba viongozi wakuu na ndo sababu wanaropoka tu!!! Kwakauli ya jana ya mama ina tofauti gani na mdude akiropoka kwenye majukwaa ya Siasa???

Sent using Jamii Forums mobile app
ndugu hakuna nchi inaweza kuongozwa kama unavyofikiri wewe never yaani kila mtu aongee la kwake raisalifuate? hakuna nchi ulimwenguni inayoweza kutawalika kwa mawazo kama unayoyafikiria rais kama rais mwacheni afanye au aongoze anavyoona inafaa lakini mtampima mwisho wa utawala wake hakuna rais anaweza kuwa madarakanai akaanza kuuwawatu bila sababu hakuna rais kichaa wa hivyo wewe unafikiri ni rahisi kweli rais awe anafuata mawazo ya kina lissu kina lemma kweli nchi itaenda siyo rahisi kama mnavyofikilia
 
Sio rahisi kama unavyosema mzee mzima

Hapa ni watu milioni 60 wanawaangalia mnavyotoa majibu ya kipumbavu...

Mtakataa ndio,kwa hoja gani yenye mashiko watu milioni 60 wawaelewe?

Hakuna majibu sahihi,mmeishia mipasho

Katiba Mpya ni muiba ambao hamkumaliziaga sababu ya matamaa yenu ya kutaka iwe ya kiCCM,sasa huu muiba umerudi kuwachoma

Raha ya tatizo ni kulifanyia suluhisho tena mapema..

Watch this space...
milioni 60 gani unayoongelea mkuu!? watu huku mtaani hawana habari na hiko unachosema, hawajali kabisa kuhusu katiba mpya. Hii mijadala ya mtandaoni kule haipo.
 
Kudai katiba mpya sio jinai, hayo ni madai halali. Huko kuumuzana kinatoka wapi? Na hata kama ni kuumizwa kwa ajili ya kudai katiba mpya, mbona uchaguzi uliopita bado watu wameuwawa kwenye uchaguzi, na kuachwa na vilema vya maisha kwa katiba hii hii?
Ukiambiwa ukubali kuolewa halafu katiba mpya itapatikana: utakubali?

Ho…
 
ndugu hakuna nchi inaweza kuongozwa kama unavyofikiri wewe never yaani kila mtu aongee la kwake raisalifuate? hakuna nchi ulimwenguni inayoweza kutawalika kwa mawazo kama unayoyafikiria rais kama rais mwacheni afanye au aongoze anavyoona inafaa lakini mtampima mwisho wa utawala wake hakuna rais anaweza kuwa madarakanai akaanza kuuwawatu bila sababu hakuna rais kichaa wa hivyo wewe unafikiri ni rahisi kweli rais awe anafuata mawazo ya kina lissu kina lemma kweli nchi itaenda siyo rahisi kama mnavyofikilia
Mimi sijasema raisi afate ya lisu ila nimeona kuna umuhimu wa katiba!!! Ushawai jiuliza kwann mstaafu jakaya kikwete alianzisha mchakato wa katiba?? Katiba ina mapungufu kibao katiba inayotumika niya mwaka 77.... Mambo mengi yamebadilika kwaiyo katiba inahitajika sisemi raisi afate mawazo ya lisu au whatever ila katiba niya muhimu ndo dira ya taifa mzee wangu.... Na pia hata yeye anatakiwa kuona umuhimu wa katiba mpya not kwasababu chadema wanataka ila kwa msingi wa taifa letu katiba lazima iwepo mabadiliko ni mengi" katiba ikibadilika na mifumo mingi yakizamani itakufa tutakwenda kisasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais Samia amewataka wananchi wa Morogoro wasikubali chokochoko zinazoanzishwa na baadhi ya watu.

Amesema hao wanaotaka kuanzisha vurugu wameshaandaa na wanajua watakavyojitibia ikitokea wamepata madhara.

Amewataka wananchi kutokubali na kutunza amani iliyopo. Amesema hayo akiwa Morogoro kwa ziara ya siku mbili.

NB: Possibly Rais anawaasa wanaotaka katiba mpya.



===

Rais Samia: Niwaombe sana tulinde amani, vijichokochoko vimeanza naomba msivipokee, wanaokuja na vijichokochoko walishajua matumbo yao yanajaaje, chakula chao wanatoa wapi, pesa za matibabu watatoa wapi, nawaomba wasije wakawaingiza kwenye huo mkenge”

Rais Samia: “Pakichafuka ni wewe utakayekaa ndani na Watoto wako na Mama Watoto na msijue chakula mnatoa wapi, msijue Mtoto akiumwa mtakwenda kumtibu na pesa gani, niwaombe sana tulinde amani yetu, Nchi yetu itulie tuendelee na maendeleo yetu

Pole Mama,
Kwa JINSI ulivyoanza vizuri nilikuwa nimeamini kabisa kuwa ulikuwa umejifunza kutokana na makosa uliyoyaona nabila shaka kuyashuhudia,
LAKINI yaonekana kuwa shetani yuleyule alieyumbisha nchi hii, aliyekuwapo ulipokuwa VP, tayari keshaanza kukuyumbisha na kuna kila dalili kuwa atakumaliza vilevile.
 
Imekula kwenu nyambaf nyie.

Tulishawaambia humu na tunaendelea kuwaambia, rais hana muda mchafu. Ana majukumu ya kuyatekeleza. Akutane na wapinzani ili iweje?
We endelea kushangilia tu Utafikiri wanaokufa affected ni watu fulani tu... Unafikiri kukiwa na tatizo wanaoathirika ni wa chama kimoja tu....!!?
 
Sheria za nchi tunatakiwa kufuata wote, isiwe watawaliwa tu.
Watawala nao wafuate sheria badala ya kutumia vitisho. Tumechoka haya miaka mitano iliyopita.
 
Salam zimfikie Mdude Nyagali sifa za kijinga zitamtokea puani. Ataenda jela peke yake sisi tutamuweka hashtag tu huku tunalala na familia zetu wakati yeye analala chini ya ulinzi.
Uzoefu unaonyesha kuwa watawala wasiopenda kufuata sheria wala katiba ni chanzo cha maumivu kwa raia wenye kufuata sheria kudai haki zao kisheria kwa kisingizio cha 'chokochoko'
 
Inakuwaje achanganye ya "Katiba Mpya", na huko "Kujiandaa kujitibia"?

Ina maana yeye Rais sasa, anakwenda kuwatia uoga wananchi wasidai katiba mpya (kufanya chokochoko) kwa vile hawajajiandaa watakavyotibu (majeraha)? watakayopata wakati wakidai haki hiyo?

Mbona haileti mantiki?
Hii ni dalili ya watawala kujiandaa kutofuata sheria kwasababu tu wameshikishwa mpini na wananchi.
 
Back
Top Bottom