Rais Samia mteue Dkt. Ashatu Kijaji kuwa Waziri wa Fedha na Mipango

Rais Samia mteue Dkt. Ashatu Kijaji kuwa Waziri wa Fedha na Mipango

Hujui kitu ww, uchawa ushakuharibu, Ashatu na Mwigulu who is smart? Kumbe ww hujui kitu kabisa, ulijua Mh. Rais kumteua Dr. Mwigulu na kumpa Wizara ya Fedha, ulidhania kakosea au hakujua ni mtu smart and brilliant? Ashatu is no way ukamlinganisha na Mwigulu, sbb uchawa umekujaa, hujui kitu
Jay One wewe ndiye hufahamu. Dkt Ashatu ni mwenye akili nyingi na muadilifu. Ukipata wasaa wa kukaa naye hata dakika moja utagundua, she is unique sana. Ana maono na mitizamo chanya ya maendeleo.
 
Prof Malima alizushiwa mengi lakini alikuwa mtu Makini na muadilifu
Sana, sema Prof. Kigoma alijiingiza mambo ya dini yakamharibu na ku impair uwezo wake kazi kama ilivyo kwa Prof. Asad
 
Jay One wewe ndiye hufahamu. Dkt Ashatu ni mwenye akili nyingi na muadilifu. Ukipata wasaa wa kukaa naye hata dakika moja utagundua, she is unique sana. Ana maono na mitizamo chanya ya maendeleo.
Uongozi ni talanta bila kujali wingi wa akili!
 
Nakupa historia ya wizara

Hiyo 20 years kuna Mramba, Mkullo,, Sada Mkuya na Dr Mpango!

Chagua mwenyewe hapo!
... katika hao ni yupi aliwahi kuwapa wananchi raha? Mzee wa kufakamia nyasi Rais apate mwewe?
 
Hana uwezo kabisa, Dr. Mwigulu ndio mzuri kwa mbali sana, there is no way ukamlinganisha na Ashatu, kwanza Ashatu hata ktk uwaziri wowote ule tu ni mzigo kabisa. Hivi vyeti sijui PhD ni thesis tu, a long essay or dissertation sio kwamba inakuonyesha uko so exceptional, Dr. Mwigulu yuko vizuri sana, hata ukiacha PhD yake, ila he is smart. Kama Ashatu kakutuma mwambie tumekataa.
PhD ni Thesis, Long essay na Dessertation tu.

Hapo nimekuelewa Sana Mkuu.
 
Kama ni usomi anaweza mzidi Mwigulu kweli?

Ni msomi ndio ila hawezi na hajui kujieleza kwa hiyo hata changamoto kama hizi za Uchumi hajui kuongea.

Nimemuona mara nyingi kwenye mikutano ya Ziara za Rais ameahindwa kutolea maelezo ya mambo ya kupanda Kwa bei za vitu na yeye ndio mhusika kwenye hiyo wizara ya viwanda na Biashara..

Pamoja na Chuki zenu sijamuona Waziri wa Fedha wa kumzidi Mwigulu kwa sasa hata yule Mchaga ndio kabisaa ataishia kupaniki na kujing'ata ulimi bure..

Hizo nafasi nyeti zinahaitaji uwe na uwezo wa kujieleza ambao Mwigulu anao na mara nyingi ametoka kutetea sera zake..

Mwisho uchumi unapimwa Kwa matokeo sio blaa blaa blaa zenu.
Mwigulu huwa anajieleza au anaeleza uongo?
Yaani unajitokeza kutetea mpigadebe na porojo anazoungaunga Mwigulu ndo unataka kutuamijisha Uzuri wake eti anajua kujieleza? Sisi tunataka maelezo ya kuhalalisha uongo au utendaji uliotukuka? Kumbe kuna watu bado mnafurahia porojo za Kisiasa na mnataka kuaminisha Wananchi kiongozi mzuri ni yule anayejua kujieleza hata kama hakuna contents kwenye maelezo yake?
 
Mwigulu anamuhujumu samia, ataelewa keshachelewa aliambiwa toka mwanzo kaweka pamba asitulilie 2025
 
Nimekuelewa hapo kwamba mara nyingi tuu nimemuona kwenye mikutano ya Rais akijiuma uma..

Kuwa intelligent ni kitu kingine na isitoshe amewahi kuwa Waziri Naibu Waziri wa Fedha..

Hana huo uwezo wa kujieleza kudefend mazingira ya siasa na weledi kwa pamoja kumzidi Mwigulu..

Unadhani wanaomteua Mwigulu toka zama za Kikwete ni Wajinga?
Mwigulu ana tija gani kwenye hizo wizara alizowahi pita.Hana tofauti na kigwangala na makamba zero results
 
GTs,

Nina maoni:

Naona kabisa Mh. Rais akimteua Dkt Ashatu Kijaji kwa nafasi ya waziri wa Fedha na Mipango itakuwa vema kwa uchumi wetu.

Sababu:
1. Dkt Ashatu ni msomi na mbobevu katika masuala ya mipango na fedha.
2. Dkt Ashatu ni muadilifu na mwenye maadili
3. Dkt Ashatu ni mcha Mungu na ana hofu ya Mungu hivyo atamshauri Mama kwa maslahi ya watanzania
4. Dkt Ashatu ana uzoefu wa kuongoza wizara ya Fedha na Mipango na ktk kipindi chake akiwa naibu waziri tulishuhudia uchumi ukiimalika.
5. Dkt Ashatu anauwezo mkubwa sana kiakili siyo tu darasani lakini pia ktk mahusiano na watu.

Naamini huu uzi Mama atausoma au wasaidizi wake wamfikishie. Watanzania tunamtaka Dkt Ashatu!
Kila unachokiona pale hakipo kibahati mbaya kwaiyo tulia uvutishwe pumzi ya moto.
 
Mwigulu huwa anajieleza au anaeleza uongo?
Yaani unajitokeza kutetea mpigadebe na porojo anazoungaunga Mwigulu ndo unataka kutuamijisha Uzuri wake eti anajua kujieleza? Sisi tunataka maelezo ya kuhalalisha uongo au utendaji uliotukuka? Kumbe kuna watu bado mnafurahia porojo za Kisiasa na mnataka kuaminisha Wananchi kiongozi mzuri ni yule anayejua kujieleza hata kama hakuna contents kwenye maelezo yake?
Uongo kama upi hasa ambao huwa anaeleza? Naona unahemka kwa mihemko ya genye.
 
Acha utoto Mzee ,VP ni mshauri namba moja wa Uchumi wa Rais pamoja na Mwigulu na huyo huyo Dr.Kijaji sasa unaposema mifumuko isingekuwepo kwani hawapo sasa hivi?

Unaweza zuia mfumuko wa Bei ikiwa bidhaa ni chache?
Unaondoa vikwazo kwenye uzalishaji
 
Back
Top Bottom