voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,545
- 11,935
Huyu mama anatuona watanzania wote kama majuha.Jambo hilo alipigiwa kelele sana Hayati Magufuli ajabu Samia naye amekuwa na aina ileile ya ufujaji mali za umma kwa safari zisizo na maana yeyote za huko kwao Zanzibar.
Ki hafla kidogo tu tunaendelea kushuhudia hudhurio lake huko!
Tunakoelekea huenda Samia atatumia ndege yetu kubwa kwenda kuhudhuria mchezo wa kuruka dama wa wanawake huko Zanzibar.
Tumseme sasa ili u Zanzibar aachane nao maana dalili zi wazi huyo mama anapenda sana show za huko kwao.
Hakuna sababu yoyote muhimu iliyomfanya kwenda Zanzibar kwa maadhimisho ya siku ya wanawake.
Labda tu alitaka kumfunika Mwinyi kwa utenguaji wake kuondoa wazembe serikalini tofauti na yeye anaewaambia wale urefu wa kamba zao.