Rais Samia Suluhu akiendelea kumkumbatia Majaliwa na Baraza lake Serikali yake haitofanikiwa, Hawana jipya

Mkuu wacha nikwambie jambo moja ambalo hilo kundi linajidanganya.

Huyu rais tuliye naye ni rais kamili wa JMT kiaheria na kama kuna mtu anajidanganya kuwa bado hatuna rais basi huyo atakuwa ameleweshwa na miluzi ya watu.
 
Pm muongo kuwahi kutokea katika historia ya nchi yetu! Anadanganya mpaka kwenye nyumba za ibada, Bungeni, nk.
All politicians are liars, big time! They told us he was alive kumbe ameisha kufa siku nyingi. Alitokaje Muhimbili Kwenda kwa mzena. Ilikuwa wanasuka mamma ya kugawana vyeo. Nashangaa JPM even survived 5 years. Hakuwa mwenzao maana he respected Mali za taifa. Nchi itaoza sasa. Lini maiti ikaaawa inapelekwa hapa kesho pale, maiti inabidi iheshimiwa siyo shoo, they wanted to show us how dead he was, walitaka tujoin in the celebrations.
 
Isiwe tabu; mwambie Samia abadirishe balaza lote la mawaziri, abadirishe na bunge, abadirishe na mahakama, na kwa kweli abadirishe na watumishi wote wa umma, na pia abadirishe na wananchi wote wa Tz na ardhi yao na kisha ashuke na vision yake na watu wake na nchi yake isiyokuwa na upako wa Magu😡!
Maana hao wote walikuwa wwnafuata maelekezo yaliyokuwa yanatoka kwenye serikali ya jiwe!
We shall always ❤️ and miss you our hero 💔 the hon Dr. JPM 🙏👊😭! Mungu tunaomba umpumzishe mpendwa wetu na shujaa wetu Mh Dr JPM mahala pema peponi penye raha ya milele na amani ya milele🙏🙏🙏
 
Mpumbavu kwenye ubora wako.

Mnalazimisha serikali iongozwe kupitia upuuzi wenu mitandaoni.

Serikali ni ya CCM, kubadili ama kutobadili Baraza la Mawaziri hakutabadili matakwa ya Ilani ya CCM.

Tulia, kunywa maji meza fundo fanya kazi
 
Vision gani unayoongelea wew?...mimi nijuavyo kuna national dvnt plan na ilani ya chama ambavyo ndio mwongozo ambao rais yeyote aingiapo madarakani anatakiwa aufuate
Kila mtu ana vision yake hata Samia ana yake kama wewe huna vision ni wewe.
 
Mpumbavu kwenye ubora wako.

Mnalazimisha serikali iongozwe kupitia upuuzi wenu mitandaoni.

Serikali ni ya CCM, kubadili ama kutobadili Baraza la Mawaziri hakutabadili matakwa ya Ilani ya CCM.

Tulia, kunywa maji meza fundo fanya kazi
Kama huna hoja sepa.
 
Majungu, Umbea na Fitina ndio Jadi yetu na hayo ndiyo yalituchelewesha kufikia Uchumi wa kati.

Sasa endapo tutarudi kwenye Ubora wetu wa kupika Majungu na Fitina huenda tukapiga hatua ndefu kurudi nyuma, ili wapika majungu na fitina washangilie kwa vicheko.

Sio kila mtanzania anaitakia mema Tanzania.
Baadhi ya wafanya biashara haswa wakwepa kodi, na wapiga dili kubwa.
 
Absolutelly !!! There is a need for house cleaning.
 
Nchi hii walimu walikua wawili watatu tu nao ni hayati Nyerere, Kambona na Seif. Mungu awalaze mahali pema peponi..
 
Watanzania watu wa ajabu sana njozi za Rais wewe zinakuhusu nini? Mngemuuliza basi mwenzake kwanini aliifuta tume ya mipango? Ile ndio ilikuwa national think tank. Hata dira ya taifa 2025 ilitengenezwa pale. Hivyo tangu hapo kila rais atafanya anavyojua yeye. Hamkuuliza wakati huo nauliza sasa. Mama ogelea unavyojua wewe nchi yenyewe ya mazwazwa.
 
Nafasi ambayo mama alitakiwa atumie nguvu zake ni kwenye kummpendekeza VP tu

Huko kwingine ingekua mimi ni Rais,ningeendeleza team ile ile niliyoikuta ningebadilisha

tu watu kama ingetokea nimeona kuna mapungufu flani sehemu,ila watu wanachotaka ni kuona

Baraza jipya la mawaziri,Ofisi zibadilishane waingie wanaowataka wao,nk ila nasema hivi mazaa endelea

Na boli mchezaji atatoka nnje ya uwanja akiwa majeruhi tu ila SUB zisizo na lazima haznaga guarantee ya kuipa team ushindi.
 
Unatokea mkoa wa Chato nini?
Subiri kwanza ukaguzi maalum wa CAG.
Gharama za ujenzi za hiyo miradi zatisha, hata za hiyo Chato International Airport ambayo iliyojengwa na kampuni yake bila ya kuidhinishwa na Bunge.
 
Kwani Rais Samia si anatokana na Baraza la Hayati Magufuli na walitengeneza na kuinadi Ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025 sasa mnataka vision gani tena chochote kinachofanyika kiko kwenye blueprint msimfitinishe Rais na chama chake na wananchi kwa maana ya muendelezo wa miradi na falsafa waliyoipigania yeye na marehemu.
 
Najua kabisa wewe una akili nyingi sana na unajaribu kuleta siasa za kilaghai kwani unajua Majaliwa anafuata mle mle yale aliyokuwa amepanga kuyafanya Hayati DKT MAGUFULI.Mwisho namshauri Mama yetu kipenzi cha Watanzania wanyonge hawa aendelee kufanya kazi na walewale kwani wamefanya kazi kubwa mpaka kufikia mahali tilipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…