Rais Samia Suluhu anakwenda kuzoa kura zote uchaguzi ujao

Rais Samia Suluhu anakwenda kuzoa kura zote uchaguzi ujao

Mama Samia suluhu Hassani hawaogopi wapinzani Bali anawaheshimu Kama ilivyo hulka yake ya kuheshimu kila mtu, Anawaheshimu hata wapinzani kwa kuwa anajuwa kuwa Taifa Hili litajengwa na sisi sote watanzania, lakini pia anaona haipendezi tukajenga Taifa ambalo limegawanyika mapande mapande,

Anataka kuona kuwa kila mtu anajivunia kuwa mtanzania, anataka kuona Kama kikijengwa kituo Cha Afya Basi kila mtu afurahi na kuona kuwa Ni chetu sote, anataka kuona mradi wa maji ukipelekwa mahali fulani unapokelewa na watu wote na kulindwa na watu wote

Anajuwa kuwa ili Hili lifanikiwe hatuna budi kujenga umoja wa kitaifa, anaona kuwa Ni lazima tuheshimiane na kupendana, anaona kuwa Ni lazima Basi ikitokea tunakosoana Basi Tukosoane kwa staha bila kuvunjiana utu wetu, anaona kuwa tunaweza tukaijenga Tanzania Yetu iliyo Bora pamoja na kuwa tunatofautiana katika baadhi ya misimamo yetu ya kisiasa

Ndio maana unaona akitoa fursa ya kuweza kukutana na kufanya mazungumzo na hata viongozi wa vyama vya upinzani ili kuzungumza nao na kukubaliana katika yanayowezekana na kutafuta muafaka katika yanayohitaji mjadala mpana

Anawaheshimu wapi?. Kama angekuwa anawaheshimu angefuta katazo la siasa.
 
Nishaona kuna magenge yameshaandaliwa kuongea PUMBA na yametapakaa sana mitandaoni. Topic zao zinajulikana sana, ukiona heading tu lazima unaweza kubashiri mleta mada ni flani. Hivi lini mtaleta uzi wenye kujadili changamoto za nchi kuliko haya mapambio ya kila siku? Nchi inavuliwa nguo na vijana watafuta teuzi, si ajabu wengi ni uvccm. Unaweza kusema ukienda huko akili zinabaki kwenye kabati linatembea dude wazi kichwani. Unaweza kukuta mnatoka semina ya sensa na kuona maisha mmeyamaliza 2025 wanastahili kura 100%
 
Nishaona kuna magenge yameshaandaliwa kuongea PUMBA na yametapakaa sana mitandaoni. Topic zao zinajulikana sana, ukiona heading tu lazima unaweza kubashiri mleta mada ni flani. Hivi lini mtaleta uzi wenye kujadili changamoto za nchi kuliko haya mapambio ya kila siku? Nchi inavuliwa nguo na vijana watafuta teuzi, si ajabu wengi ni uvccm. Unaweza kusema ukienda huko akili zinabaki kwenye kabati linatembea dude wazi kichwani. Unaweza kukuta mnatoka semina ya sensa na kuona maisha mmeyamaliza 2025 wanastahili kura 100%
Embu leta hizo unazosema changamoto ili ujibiwe na kupewa majibu
 
Mh mama Samia suluhu Hassani 2025 usidanganyike kuchukua fomu utaaibika.

CCM viongozi wanakundanganya , CCM wanachama wanakusema vibaya mno.

Sabuni ya Kufulia nguo kipande ni Tsh 1,200 /=
Kama huwezi ku afford kununua sabuni kipande Tsh 1,200 then wewe ni mvivu. Fanya kazi acha mjungu na utoto
 
Kama huwezi ku afford kununua sabuni kipande Tsh 1,200 then wewe ni mvivu. Fanya kazi acha mjungu na utoto

Mwenzako anaongelea mfumuko wa Bei wewe unaleta dharau. Usifikirie kila mtu anaishi Maisha unayoishi wewe. Tuwafikirie na wengine.
 
Hapana ndugu yangu, Naomba uelewe kuwa siyo tume inayokupigia kura, Bali wananchi ndio wanaokupigia kura, utapigiwa kura endapo una Sera na ajenda zinazo gusa maisha ya watu,

Kwa Sasa wapinzani na upinzani umepokwa hoja zote kwa mh Rais kufanyia kazi Kero mbalimbali zinazokuwa zinawatesa wananchi, watu wanaona juhudi za mh Rais katika kuboresha maisha yao, watu wanaona Rais anavyokosa hata muda wa kupumzika ili watanzania wapate maji Safi na salama, Elimu Bora, umeme wa uhakika na Bei nafuu, huduma za Afya zilizo Bora

Sasa utawaambia Nini watanzania juu ya mama Samia wakakuelewa kwa Sasa, utaanzaje kuwakusanya watanzania wamzomee Rais wao ambao kwao Ni mkombozi katika maisha yao

Watanzania wanaona namna mh Rais alivyo msikivu, Namna alivyo na Roho ya huruma Jambo linalomnyima usingizi akiona Kuna watu wanahitaji maji au kituo Cha Afya eneo fulani, Ndio maana unaona anavyopambana kuhakikisha kila Senti inayopatikana inakwenda kupunguza kero kwa wananchi
Ndugu yangu,wewe kama ni mwanachama na unadhanikia kwakuwa huko upande huo, nami nikili wazi tuko pamoja upande huo lakini sikubaliani na hoja zako dhaifu, yaani maisha yalivyopanda, kila uchwao watanzania wanabebeshwa misalaba ya ugumu wa maisha,katika tozo za muamala ya simu, leo tozo kwenye mabenki, gharama za usafiri juu, vyakula juu,mafuta ya kula juu, kila sehu juu, unakuja kushabikia na kupongeza serikali kwa stahi hiyo, basi wa utakuwa mlamba asali pia.
Narudia niko upande huo unaoshabikia,naheshimu mawazo yako lakini binafsi serikali imewafanya watanzania kuishi kwa kubahatisha huku fedha za umma zikitafunwa hovyo na huduma za huduma zikishuka mwelekeo wako ktk utendaji wake.
Note: 2025 namuona mheshimiwa kutogombea nafasi hiyo ya juu tena na sina imani iliyotumilika kama chama kitampitisha nafasi hiyo ya juu nchini kwakuwa amerithi kikatiba hadi kufika hapo alipo. Muda utaongea vinginevyo upinzani ukishindwa hapo,basi wafanye kazi nyingine.
 
Hata wapinzani wapewe nafasi yakuwa na wajumbe kutoka kamati kui yao kuwa katika tume ya uchaguzi bado hawawezi kumtikisa mh Rais, maana wanaopiga kura Ni wananchi na wananchi ndio hao ambao kwa Sasa wanamuunga mkono mh Rais
Talk for yourself....... Ni wananchi gani hao unaowasemea. Wapinzani pia ni wananchi. Kama una mahaba na Maza baki na mahaba yako.
 
Watanzania wengi Sana wameguswa na utendaji kazi wa mh Rais, embu niambie hapo ulipo Kama mh Rais hajakufikia, au hujaona shule , zahanati,vituo vya Afya, zikijengwa hapo mtaani kwako, vipi wewe siyo mkulima, Kama Ni mkulima hujasikia habari za mbolea za Ruzuku
Talk for yourself....... Ni wananchi gani hao unaowasemea. Wapinzani pia ni wananchi. Kama una mahaba na Maza baki na mahaba yako.
 
Watanzania wengi Sana wameguswa na utendaji kazi wa mh Rais, embu niambie hapo ulipo Kama mh Rais hajakufikia, au hujaona shule , zahanati,vituo vya Afya, zikijengwa hapo mtaani kwako, vipi wewe siyo mkulima, Kama Ni mkulima hujasikia habari za mbolea za Ruzuku
Nyie recruits wa Shaka .... mnatuharibia jukwaa letu kwa vipropaganda vyenu uchwara.
 
Nishaona kuna magenge yameshaandaliwa kuongea PUMBA na yametapakaa sana mitandaoni. Topic zao zinajulikana sana, ukiona heading tu lazima unaweza kubashiri mleta mada ni flani. Hivi lini mtaleta uzi wenye kujadili changamoto za nchi kuliko haya mapambio ya kila siku? Nchi inavuliwa nguo na vijana watafuta teuzi, si ajabu wengi ni uvccm. Unaweza kusema ukienda huko akili zinabaki kwenye kabati linatembea dude wazi kichwani. Unaweza kukuta mnatoka semina ya sensa na kuona maisha mmeyamaliza 2025 wanastahili kura 100%
Wivu utakuua Mzee..😬😬

.Wewe unadhani kwa nini asizoe kura zote Kwa mambo makubwa anayofanya?

Atazoa Lisu au Mbowe au? Ni hivi hata Mbowe awe Chibukati,Benson Kigaila awe IGP na mgombea awe Lisu ,Rais Samia atashinda saa tatu asubuhi..

Kazi inaendelea kila Kona ya Tanzania 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220818-073531.png
    Screenshot_20220818-073531.png
    170.4 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220818-091905.png
    Screenshot_20220818-091905.png
    157.7 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220818-091739.png
    Screenshot_20220818-091739.png
    116.8 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220817-214809.png
    Screenshot_20220817-214809.png
    113.1 KB · Views: 5
  • Screenshot_20220817-171225.png
    Screenshot_20220817-171225.png
    240.6 KB · Views: 4
Sidhani kama kuna mtanzania yupo tayari kuleta vurugu kwenye nchi yake kwa ajili ya kupigania maslahi ya wanasiasa labda wenyewe ndio wajitetee wenyewe. Mwanasiasa huwa hataki kutawaliwa anataka yeye ndio atawale ndio maana leo watasema kiongozi huyu mbaya akija mwingine naye mbaya ukimuuliza yupi ndio mzuri atasema yeye chama chake na wapambe wake
 
Watanzania wote tunaonekana hovyo kwasababu ya wapumbavu wachache
 
Ndugu zangu wahenga walishasema "nyota njema huonekana asubuhi", kwa kazi nzuri na ya kutukuka anayoifanya Mh. Rais katika kuijenga Tanzania mpya, ni dhahiri uchaguzi ujao utakuwa mwepesi Sana kwake kuweza kupita. Kwa Sasa hakuna mpinzani yeyote mwenye mwelekeo wala nguvu ya kuweza kuja kumtikisa Mh. Rais uchaguzi ujao.

Hii inatokana na ukweli kwamba upinzani ulikuwa unategemea makosa ya serikali ili upate ajenda na kujijenga, lakini Mama Samia Suluhu Hassani, punde tu baada ya kuapishwa ni Kama alikuwa analijua hilo. Kwa sasa ndani ya mwaka mmoja na miez kadhaa ameziba mianya yote na kuunyima upinzani ajenda na sera kwa serikali yake, kwa hiyo sasa hivi wapinzani wanashindwa wawaeleze nini wananchi, maana kila kitu kimeguswa na kufanyiwa kazi na Mh. Rais.

Ndio maana unaona wapinzani wengi sana wanamuunga mkono Mh. Rais kwa kazi kubwa anazofanya katika kuijenga nchi yetu. Hakika siasa ni sayansi na mama ameumaliza upinzani kisayansi kwa kufanya kazi wanayohitaji wananchi. Maana wananchi walichokuwa wanahitaji ni mtumishi wao, na kwa sasa Mama Samia Suluhu Hassani amepatikana, hivyo hawana muda tena na habari za vurugu, maandamano, makelele wala matusi kwa serikali.

Mama anaupiga mwingi, ni Mama hadi 2030 hapo ndiyo tutaanza mazungumzo baada ya kufika kituo hicho. Kikubwa ni maombi yetu kwa Mwenyezi Mungu ili amlinde na kumpigania Mh. Rais wetu, ampatie na kumjalia uzima na afya njema.
Labda atapata kura yako tu. Rais gani wa tz badala kutoa hela kwa matajiri kuendesha na kuendeleza nchi anatoza mitozo kwa watu wa chini huku taifa halielezwi kama zile kodi za madini zimeenda wapi. Kawasamehe barrick ile hela waliyoepa kodi ya makinikia utadhani ni wajomba zake.
Tumezoea mjamaa kuongoza nchi sio kuachia sekta binafsi kudhibiti serikali.
 
Kiongozi wa watu vs Mapaka👇😁😁😁

 
Back
Top Bottom